Ukodishaji wa ndege za serikali, Risiti za Salma Kikwete

kiama chao ndo kimefika hivyo, wafa maji kinana na wenzake wamebaki kutapatapa tu.
 
Mambo ya Ajabu sana haya...

Hiyo Risiti ukiiangalia kwa makini utagundua ina walakini...

1. Haisemi imetolewa lini.

2. Ililipiwa lini

3. Imelipwa na nani

4. Je inawezekana kukodisha ndege ya serikali kabla ya malipo maana inaonekana kukodishwa kulifanyika 28/08/2010 na malipo yakafanyika 31/08/2010

5. Risiti pia haizungumzii ni ndege gani imekodishwa kama ambavyo ilikuwa described na akina slaa inasema air fleight number... sasa kwa wanao fanya kazi airport watakubaliana kwamba fleight number inategemea na siku ndege inaposafiri ndo itajulikana...

6.Nilifikiri kwamba serikali inapiga marufuku matumizi ya dollar... sasa iweje leo hii malipo hayo yafanyike kwa dollars ... kwa nini sasa they dont practise what they preach?

7. Usd 15000 Kwa masaa matano? Kwa kazi gani anayofanya huyo mama... hii inaonesha kwamba hawa watu ni anasa tu..Dollar elfu 15 kwa kazi gani anayofanya maana WAMA ni charity tu na sidhani kama sisi wachangiaji wa hiyo charity tungeruhusu matumizi makubwa ya ku-hire private govt jet ya namna hiyo... huu ni mfano mmbaya wa public figures kama hawa... they are setting dangerous examples...hata kama ingelipiwa na CCM... hili pia haliko wazi maana inasema tu Secretary General Chama cha mapinduzi.. sasa sijui ni yeye aliyelipa au ni CCM ... Kama alikuwa analipa wa niaba ya CCM basi tisiti ingeandikwa received from CCM for accounting purposes ndani ya serikali na huko CCM Kwenyewe.

8. Mwihso Mbona hatujawahi ambiwa kwamba ndege ya serikali ni ruksa kukodi kwa watu binafsi wakiwemo serikali mbadala (wapinzani)?

Ni hayo tu wakuu... free to make additional observations.

Hayo matumizi ya dola badala ya shilingi kwa serikali na kwa malipo ya ndani nayo ni skendo fulani kwanini watumie USD kwa malipo ya ndani
 
Hiki ndicho nilichotaka kusema kwa sababu nilikuwa na mashaka sana na mpangilio wa namba za risti hizo, ila nikakwama katika kutafuta sheria iliyotunga agency hiyo. Nilitaka kujua pia majukumu ya agency hiyo kisheria; nimetafuta pale Bunge nikachoka na kukata tamaa. Ila nina wasiwasi mkubwa sana na legitimacy ya invoice hizo alizoonyesha Kinana na uhalali wa matumizi ya ndege hizo kwa shughuli za binasfi; nilikuwa ninaamini kuwa ndege zile zinakodishwa na wizara kwa shughuli za kiserikali tu, ila nilitaka kujiaminisha kwa kusoma sheria inasemaje.

Kilichonishangaza zaidi ni lile pengo liliopo baina ya invoice hizo mbili katika kipindi cha wiki mbili tu ukichukulia kuwa wao wanaandika invoce zao kinyume nyume, utadhani kuwa Agency hiyo ina biashara nyingi sana kiasi cha kuwa na wateja zaidi ya 500 kwa wiki!!

kwa taratibu za ukusanyaji kodi wa TRA, hiyo agency tayari iko kwenye matatizo ya kutumia vitabu viwili kwani hizo ni dalili za kukwepwa kodi. pia Profoma ilitakiwa kuonyesha kiwango cha VAT inayopashwa kulipwa! Sasa tunahitaji kuona wamelipa kodi kiasi gani ktik kipindi chote hiki kutokana na fedha walizopokea kutokana na kukodisha ndege zao.
Kinana asifanyie mzaha hili maana malipo yanaendana na kuandikwa kwa genuine receipts!
 
Halafu hizo sio risiti ni hati za madai (proforma invoices) ambazo hazina maana kuwa malipo yamefanyika. Kinana anatakiwa kutuonesha stakabadhi za serikali. Hata mimi naweza kupewa 'hati ya madai' na nikaamua kutokulipa na kutopata pata huduma niliyohitaji! Lakini Salma anatuonesha proforma invoices bila risiti za serikali na huku amekwishatumia ndege hiyo!!!!!!!

Kinana lete na risiti haraka! Ili ni tatizo la ushemeji, ilibidi aongee Kikwete, mumewe na sio nyie mashemeji!!!!!!
 
Kwa kweli likizo hii ya X-mass nataka kuikodisha, jamani narudia tena kuomba utaratibu wa kuikodi na bei!
.
Mwanamayu,
Nijuavyo mimi, Shirika la Ndege za Serikali, halikodishi ndege zake kwa shughuli zozote zisizo za serikali.

Wakati wa Wiki ya Utumishi wa Umma, toka kwenye viwanja vya CCM Kirumba mjini Mwanza, Afisa Mtendaji Mkuu wa TGFA, alisema ndege za serikali, hazikodishwi!.

Sasa kama CCM nayo ni serikali, naamini by kesho ataissue statement kufafanua hili.
 
Kinachotakiwa Kinana akaonyeshe mahakamani kama risti ni za kweli au kugushi itajulikana si vitabu vitaletwa, na vile vile watuambie walianza lini kukodi ndege za serikali ina maana serikali inafanya biashara ya kukodi. Mimi nafikiri Chadema wasonge mbele tu wapeleke suala hili mahakamani ili waendelee kuwaweka CCM kwenye defensive position wakati wote wa kampeni.

Mkuu watachoma moto ofisi ya Wakala wa Ndege sasa hivi. Vitabu vyote vitapotea, sasa ushahidi utatokea kwenye majivu? Kwa serikali hii hakuna baya linaloshindikana!
 
Ni invoice kwa Katibu Mkuu wa CCM. Kuna matatizo haya:

(1) Kitengo cha ndege za serikali si cha biashara. Hakina kibali cha kufanya biashara.

(2)Serikali ya CCM hairuhusiwi kufanya biashara na CCM. Kunakuwepo na conflict of interest.

(3) Sidhani Mtendaji Mkuu wa hicho kitengo angeandika USD 15,000/=. Hiyo alama" /= " ni kifupisho cha "shilingi".
hiyo kwenye red naomba clarification, kwasababu nakumbuka tulishawahi kuambia kile kitengo kinaweza kukodisha ndege kwa watu binafsi
 
Kaaaaaaaaaaaaaaazi kweli kweli, real CCM ni mafisadi na wapenda mambo ya kifahari.Najiuliza vitu kadhaa
1.Chopper 3 kwa kampeni.
2.Ndege kwa Salma.
3.Mabango ya picha kubwa za JK nchi nzima tena yenye gharama kubwa.
4.Misafara mizito ya magari kila kampeni inapofanyika.

Je Nyerere, Mwinyi na Mkapa walikampeniwa na wake zao au kutumia Chopper 3, Magari na Mapicha kibao nchi nzima? JK hatufai maana hadi kampeni zake zinaisha nchi itakuwa maskini kama anajiamini asingetumia hio mihela yote.

Je gharama za uchaguzi ni kwa wapinzani tu maana CCM wameshaover use mpka sasa, NEC wapo au wamekaa kimya kwa kuwa wao wamewekwa na JK?

Tufanye nin?

Huu ni mwaka wa mageuzi, hatuwezi kumchagua chama kinachotumia vibaya fedha za walala hoi kujikampenia, kwani najua CCM hawana uwezo wa kuwa na hela nyingi hizo za kugharamia uchaguzi kwani vyanzo vyao vyote vya mapato vinaliwa na viongozi wa CCM mawilayani.
Shime wanaJF tulione hili na litukere na tuamua kuwang'oa CCM tumechoka kupewa umaskini kwa manufaa ya wengine.
 
Mkuu watachoma moto ofisi ya Wakala wa Ndege sasa hivi. Vitabu vyote vitapotea, sasa ushahidi utatokea kwenye majivu? Kwa serikali hii hakuna baya linaloshindikana!


Anachoonyesha Kinana ni Hati ya Madai (invoices). Naomba nieleweshwe na wenye ufahamu wa hizi taratibu za ununuzi. 'HATI YA MADAI' inakuwaje risiti?
 
Huku kutapatapa kunaweza kuwapeleka kubaya sasa. Ina maana serikali inafanya biashara ya kukodisha ndege? Na hizo fedha zinapelekwa kwenye account gani? Namna nyingine ya kujibu mambo inatia mashaka umakini wa hawa watu. Imefikia mahali kuwa nchi hii inaendeshwa kwa matakwa ya mtu na familia yake. Serikali inafanyaje biashara ya kukodisha ndege? Ina maana ikitokea mtu akataka kukodi ile convoy ya magari ya Rais kwa ajili ya harusi inawezekana? Hawaachi kutushangaza kwa kweli...


Good question. Katika kikao cha bunge cha bajeti sijawahi kusikia Wizara yoyote, au taasisi, au whateve, wakitoa taarifa ya "MAPATO YATOKANAYO NA KUKODISHA NDEGE YA SERIKALI" I stand to be corrected, kama kuna mtu ana hiyo taarifa ya Hansard Please!
 
Kinana alisema jana kwamba Mama Salma anafanya kazi nzuri sana kwa CCM na mikutano ya kampeni anayofanya ni ya "ndani" sio ya hadhara. Mimi nadhani tuachane na hili kwani sidhani kama litampunguzia kura Dr Slaa. Urais ni TAASISI ambayo familia ya Rais huwezi kuitenganisha nayo. Afya ya JK ni mgogoro na huyu mama analijua zaidi hilo na mjue tu kwamba ana-play role kubwa zaidi ya hiyo mnayoiona kwenye majukwaa.

Mkuu,

Kwenye uchaguzi kila kura moja ina count towards ushindi. Kwa hiyo ukisema haiwezi kumpunguzia kura Dr Slaa, hapo unafanya makosa.

Pili, ni swala lililowazi kwamba chama tawala hakitakiwi kutumia resources za serikali kwenye kampeni zake. Iwapo mabango ambayo yamepigwa Ikulu imeamuliwa yatolewe kwa kuwa tu inawezekana waliopiga picha hizo ni waajiriwa wa serikali. Je, matumizi ya ndege ya serikali kwa mtu ambaye anawafuata wapiga kura na kuwahamasisha ili wakawahamasishe na wengine, bado unaona kwamba hakuna madhara? Mimi sikubaliani na wewe kwenye hili.

Tunapodharau vitu kwa kuona kwamba havina madhara, tuna create irresponsibility kwa wahusika na baadaye inakuja kuonekana ni mazowea. Hapo ndio unakuja muendelezo wa matumizi mabaya ya mali ya umma.
 
Nadhani Kinana amelewa madaraka na sasa hajui analolifanya, kutuonyesha risiti haitoshi - watueleze hizo gharama zinalipwa na nani? Mama Salma anatumia misafara ya magari ya Ikulu kwa bajeti ipi? Anapewa mapokezi ya viongozi wa serikali kwa gharama za walipa kodi, au hata hao anazo risiti za matumizi yao?
 
.
Mwanamayu,
Nijuavyo mimi, Shirika la Ndege za Serikali, halikodishi ndege zake kwa shughuli zozote zisizo za serikali.

Wakati wa Wiki ya Utumishi wa Umma, toka kwenye viwanja vya CCM Kirumba mjini Mwanza, Afisa Mtendaji Mkuu wa TGFA, alisema ndege za serikali, hazikodishwi!.

Sasa kama CCM nayo ni serikali, naamini by kesho ataissue statement kufafanua hili.

Sure. Hata mimi niliwahi kupata hayo maelezo kutoka kwa maafisa. Lakini kwa kuwa CCM ndo Serikali tegemea huo ufafanuzi toka kwa mkuu wataasisi muda wowote kuanzia sasa. Hii ndiyo Tanzania; si bure Zanzibar wanapaki virago vyao!
 
Kinana alisema pia kwamba Dr Slaa na Prof Lipumba wanajiita "RAIS" kwenye baadhi ya mabango yao ya kampeni. Hili nalo limekaaje?
 
Anachoonyesha Kinana ni Hati ya Madai (invoices). Naomba nieleweshwe na wenye ufahamu wa hizi taratibu za ununuzi. 'HATI YA MADAI' inakuwaje risiti?

An invoice is a statement of what you owe for the item(s) and usually terms of payment. A receipt is something that indicates what you paid. An invoice is not a receipt unless it indicates that you paid (by credit card or is otherwise marked "paid" by the party that issued the invoice).

If you paid by cash, you should have gotten a receipt or had the invoice marked "paid". A "cash" invoice might assume to be paid unless there are other terms for payment on the invoice.
 
Walete walete walete haoooo......!!!! Za mwiziiiiii.......aroooobaaiinniiiiii.....!!! Mtu akikushauri utende jambo baya mwambieeeeeee.......watanzania wa leo hawapeeendiiiiiii.....!!!!!

Kinana na wazee wa CCM ambao mnafikiri bado watanzania ni washamba wasio na uwezo wa kunyambua mambo, pateni habari kuwa siku hizi watu wanatazama mambo kwa jicho la umakini. Msikurupuke kiasi hicho, mnafoji hata mtoto wa STD I anashtukia...!! Mimi sijawahi kusikia document yoyote ya kihasibu ya ndani ya shirika ikiwa ina sequence inayoenda kinyume yaani kuanzia mbele kurudi nyuma.

Duuuuuhhhhhhh.....!!! Kura muibe na kuibiana na kutudanganya pia...!!............??????? Noooooooo plzzzzzzzzzzzzz....!!! Mwaka huu mtapiga sana safari kwa babu, lakini nchi lazima muiachie. Watu wanamuomba Mungu aliye mkuu....!!!
 
risiti (invoice) iliyotolewa tarehe 31/08/2010 ikawa na serial no. 00868727
tarehe 14/09/2010 ikawa na serial no. 00867609

Hapa hata mjinga huwezi mdanganya kirahisi kihiivyo
Ndo tatizo la kupeleka dili za kufoji Kinondoni mngeniletea mm niwafanyie kazi hapo Gerezani.
 
mambo ya ajabu sana haya...

Hiyo risiti ukiiangalia kwa makini utagundua ina walakini...

1. Haisemi imetolewa lini.

2. Ililipiwa lini

3. Imelipwa na nani

4. Je inawezekana kukodisha ndege ya serikali kabla ya malipo maana inaonekana kukodishwa kulifanyika 28/08/2010 na malipo yakafanyika 31/08/2010

5. Risiti pia haizungumzii ni ndege gani imekodishwa kama ambavyo ilikuwa described na akina slaa inasema air fleight number... Sasa kwa wanao fanya kazi airport watakubaliana kwamba fleight number inategemea na siku ndege inaposafiri ndo itajulikana...

6.nilifikiri kwamba serikali inapiga marufuku matumizi ya dollar... Sasa iweje leo hii malipo hayo yafanyike kwa dollars ... Kwa nini sasa they dont practise what they preach?

7. Usd 15000 kwa masaa matano? Kwa kazi gani anayofanya huyo mama... Hii inaonesha kwamba hawa watu ni anasa tu..dollar elfu 15 kwa kazi gani anayofanya maana wama ni charity tu na sidhani kama sisi wachangiaji wa hiyo charity tungeruhusu matumizi makubwa ya ku-hire private govt jet ya namna hiyo... Huu ni mfano mmbaya wa public figures kama hawa... They are setting dangerous examples...hata kama ingelipiwa na ccm... Hili pia haliko wazi maana inasema tu secretary general chama cha mapinduzi.. Sasa sijui ni yeye aliyelipa au ni ccm ... Kama alikuwa analipa wa niaba ya ccm basi tisiti ingeandikwa received from ccm for accounting purposes ndani ya serikali na huko ccm kwenyewe.

8. Mwihso mbona hatujawahi ambiwa kwamba ndege ya serikali ni ruksa kukodi kwa watu binafsi wakiwemo serikali mbadala (wapinzani)?

Ni hayo tu wakuu... Free to make additional observations.

Wakuu mbona!!!!!!!!!!!!!!!!. Hiyo ni hati ya Serikali ya madai au Govrnment bill kwa ajili ya kukodisha ndege. Hati hiyo ilitolewa 31.08.2010 kwa ajili ya ukodishaji wa ndege ya serikali iliyokodishwa na ccm kwa muda wa saa 5 tarehe 28.08.2010. Nadhani hayo mambo mengine ni tafsiri za hisia. Wakala wa ndege za serikali anakodisha ndege kama ilivyo temesa ambao wanahusika na ukodishaji wa magari ya serikali. Yule anayetaka macedes benz au royce royce etc waone. Wako pugu rd mkabara na kamata. Wakala wa ndege wa serikali wao wapo pale sokoine karibu na kituo cha meli ziendazo zanzibar.

Sasa hoja ni nini? Kama hawajalipa basi tuzungumzie hilo. Naomba kutoa hoja.
 
Back
Top Bottom