Ukiwa na moyo dhaifu usifungue ni ajari mbaya boda boda

ukweli ni kwamba taratibu zinakiukwa sana hivi kweli haya maisha tutafika? katika hili la ajali kila mmoja ni mzembe kwa kiwango chake kuanzia sisi abiria ,madereva ,watu wa usalama na wazembe wakuu ni hiyo serikali ambayo inapaswa kuweka misingi inayotakiwa,,,,
 
529058_328682440512117_100001110916827_789575_1404827954_n.jpg


Ni lini watanzania tunakabiliana na ajari za kizembe zinazo sababisha vifo visivyo tarajiwa?
Hii ni ajari imetokea maeneo ya ubungo kama unavyo ona dereva na mteja wa boda boda walilambwa na gari.
Je swala la usalama barabarani linaitaji kuwa swala la mtambuka?
Je Trafic polisi wameshindwa kazi za kusimamia usalama barabarani?
Kuna haja kuwepo na usalama shirikikishi barabarani pindi dereva anapo vunja sheria za barabarani raia wamkamate na kumfikisha sehemu husika badala ya kusubili Trafic ndo amkamate?
Taifa linapoteza nguvu kazi, vijana wanakufa vifo vya kizembe sana barabarani.
Inalilah wainalilah lajuun!!
 
....Ni huzuni sana! Hata hivyo, nani alaumiwe?! Je, ni Wachina waliyetengeneza TOYO, SUNLG na pikipiki nyingine? Au, tuseme hizi ndio "ajira" kwa vijana wa Tanzania ambao hawatayarishwi kwa mafunzo maalumu ya matumizi ya vifaa vya moto (motor bikes) na sheria, kanuni na taratibu za matumizi ya barabara (kwa usalama wao na vyombo wanavyotumia)? Nadhani tuna wajibu wa kuchunguza kwamba ajali nyingi zinazotokea barabarabi zinazowahusisha madereva (vijana) wa BODABODA (PIKIPIKI) zinasababishwa na ukosefu wa weledi (maarifa + ujuzi (ustadi) + maadili) ya matumizi ya vyombo vya moto na matumizi ya barabara. Tuna wajibu kama taifa kuhakikisha kwamba vijana wanapojiajiri kwenye sekta ya uchukuzi wanaandlaiwa kabla ya kuingia kwenye kazi hiyo.
 
....Ni huzuni sana! Hata hivyo, nani alaumiwe?! Je, ni Wachina waliyetengeneza TOYO, SUNLG na pikipiki nyingine? Au, tuseme hizi ndio "ajira" kwa vijana wa Tanzania ambao hawatayarishwi kwa mafunzo maalumu ya matumizi ya vifaa vya moto (motor bikes) na sheria, kanuni na taratibu za matumizi ya barabara (kwa usalama wao na vyombo wanavyotumia)? Nadhani tuna wajibu wa kuchunguza kwamba ajali nyingi zinazotokea barabarabi zinazowahusisha madereva (vijana) wa BODABODA (PIKIPIKI) zinasababishwa na ukosefu wa weledi (maarifa + ujuzi (ustadi) + maadili) ya matumizi ya vyombo vya moto na matumizi ya barabara. Tuna wajibu kama taifa kuhakikisha kwamba vijana wanapojiajiri kwenye sekta ya uchukuzi wanaandlaiwa kabla ya kuingia kwenye kazi hiyo.

Umenena mkuu lakini nafikiri usafiri huu ungesimamishwa kwa sasa ili uwekewe mazingira mazuri ya kazi vinginevyo ni maafa tu.
 
529058_328682440512117_100001110916827_789575_1404827954_n.jpg


Ni lini watanzania tunakabiliana na ajari za kizembe zinazo sababisha vifo visivyo tarajiwa?
Hii ni ajari imetokea maeneo ya ubungo kama unavyo ona dereva na mteja wa boda boda walilambwa na gari.
Je swala la usalama barabarani linaitaji kuwa swala la mtambuka?
Je Trafic polisi wameshindwa kazi za kusimamia usalama barabarani?
Kuna haja kuwepo na usalama shirikikishi barabarani pindi dereva anapo vunja sheria za barabarani raia wamkamate na kumfikisha sehemu husika badala ya kusubili Trafic ndo amkamate?
Taifa linapoteza nguvu kazi, vijana wanakufa vifo vya kizembe sana barabarani.
Hii picha sio ya Ubungo na ajali hii haijatokea Tanzania. Mleta thread athibitishe
 
Aisee hii inatisha mnajua huyo mwenye t shirt ya mistali amekatika kiuno kabisa, hebu angali miguu yake na kiwiliwili vilivyo utagundua, huo mguu wenye boot ni wa kushoto! inatisha sana wakuu.
 
Mungu awarehemu!! Ndio Athari za Nchi Kutokutaliwa kwa utaratibu wa Sheria!! Wamebaki wachumia Tumbo Tu!! Mimi ninachojua Sheria ya Usalama barabarani Inaweza Kusimamia kitu fulani!! Hasa tunaposema PUBLIC TRANSPORT!! LAZIMA SUALA LA USALAMA LIZINGATIWE!! SASA NANI WA KUSIMAMIA HILI!! WAZIRI HUSIKA ANAFANYA KAMPENI!! Eh Mungu Turehemu!!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Aaa kama ni boda boda wache wafe tu.
Hawa jamaa ni kero kubwa sana.
Na wao hujiona wapo juu ya sheria ,hawakosei,na wanajua kila kitu, nahujifanya wanaumoja na ushirikiano sana.

Wanashinda wanakunywa viroba,banana na kuvuta bangi akitokea tu mteja wanapakia mwendo mdundo mziki mkubwaa hata apigiwe horn vip hasikii wala kuelewa.
 
lakini andhani madereva wa bodaboda ni notorious zaidi. Ukiangalia vituko wanavyofanya barabarani, ni vya hatari sana. Nawashangaa sana wanapokuwa kwenye trafic lights jinsi wanavyoshindana na magari!

hili huwa nali0na xana hapa jijini dar,kwenye juncti0n zenye taa
 
Ajali ni ajali tu...ndio maana ikaitwa ajali!

Hapana Mkuu. Ajali nyingi hasa za kwetu zinaepukika kabisa. Imeitwa ajali kwa sababu "an accident or mishap is an unforeseen and unplanned event or circumstance, often with lack of intention or necessity. It most often implies a generally negative outcome which may have been avoided or prevented had circumstances leading up to the accident been recognized, and acted upon, prior to its occurrence."

Bodaboda ni tatizo Tanzania. Sijui hata ni kwa nini bodaboda zimeruhusiwa.
 
Suala la boda boda na bajaj litaendelea kuwa kero na hatari kwa maisha ya Watanzania.. Bahati mbaya Serikali iliruhusu biashara hii bila ya kufanya maandalizi.. Hebu tuwaangalie hawa madereva wa bodaboda.. baadhi ya madereva ni waliokuwa Vibaka mitaani (na hili nimelishuhudia mwenyewe).. Wengine walikuwa ni wa vijiweni tu.. Wengine walikuwa ni wafanyakazi wa ndani.. Tajiri kanunua pikipiki kaamua kumkabidhi kijana wake wa ng'ombe.. Hii yote inamaanisha hawa wameingia barabarani bila ya kuwa na uelewa wa sheria za barabarani na hata uendeshaji wa pikipiki wenyewe ni wa mashaka.. Serikali izinduke kabla hili bomu halijalipuka kabisa..
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mbona mabais yanachinja kila siku na hayajazuiwa,swala sio kuruhusu ama kutoruhusu boda boda,suala ni mkazo kwenye sheria ndogondogo na kuwapiga msasa wa mara kwa mara bodaboda
 
Inatisha,lakini waendesha bodaboda wengi wana matitizo juzi nimeona bodaboda ikichomekea scania.
 
Back
Top Bottom