Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,321
Katika hali ya kushangaza mahakama imetoa hukumu kuwa mzee wa vya vijisenti alipe faini ya laki saba baada ya kukutwa na hatia ikiwemo kugonga,kuua na kuendesha gari bila Bima. Wakati flani nilisoma uzi hapa jf ukasema mzee Vijisenti huwa anapitia hukumu yake na kuiedit ili ikasomwe alivokuwa anataka. Maneno haya yanaweza kuaminika maana baada ya kudaiwa laki7,kwa sababu mama alijulishwa kabla mama aliandaa iyo 'posho', mama vijisenti alikabidhi vihela na kupanda 'luxury car' na kuondoka! Bajaji iliyogongwa,bila kujali nguo na viatu vya waliokufa si chini mil.2 ila faini ni lak7 ambayo pia ni mali ya Jamhuri! Mwenye ela atazidi kufanya atakavo katika jamii yetu. Mi nasema sikuridhika! WanaJF nisaidie maana Mahakama imenikoroga! Kutokana na kesi hii mahakama za chini nchini Tanzania zinaweza kutumia njia ya "stare decisis" na kesi zifuatazo kama hizi zipate hukumu inayofanana na hapo matajiri watatutoa roho barabarani wakijua tamati ya hukumu. Ee mola niepushe dhidi ya mabwanyenye na mafisadi wa kitanzania!