ayubuchacha12
Member
- May 8, 2012
- 19
- 7
Makaratasi huwa ni mengi ya kusahihisha somo la uraia/civics kwenye mitihani ya kitaifa ya sekondari, General study (GS) kwa sekondary ya juu (High School) na development studies kwa ngazi ya vyuo. Kwa hiyo waalimu wanaosahihisha URAIA wanapata hela nyingi kushinda waalimu wa PHYSICS, CHEMISTRY, BIOLOGY na MATHEMATICS. Ukweli unaendelea kuwa huo huo kwa maprofesor wa masomo magumu magumu ukilinganisha na maprofesor wa masomo ya usanii (arts), kweli sio kila mwenye mbio ashindaye... watu wanaofanya kazi ngumu na kwa masaa mengi sio wanaolipwa vizuri hasa hapa Africa. NO FAIRNESS... Kama mtu anajua kwa nchi za wenzetu walioendelea tofauti ya mshahara na marupurupu nchi kama Uholanzi kwa mtu wa kima cha chini na kima cha juu ni mara nne tu,,, mfano profesor anamzidi mhudumu wa ofisi mara nne tu...eg profesor kama analipwa milioni 4, mhudumu analipwa milioni moja....lakini kwa hapa kwetu profesor analipwa milioni 3,,,,mhudumu analipwa laki moja....what a difference!!!!
Jamani keki ya Taifa haigawanywi kwa usawa,,,,hata sijui hao watu wanaopanga mishahara kama wamesoma au wanabuni tu kiwango cha mishahara????????
Tafadhari ofisi ya utumishi wa umma na wizara ya kazi na ajira mwende ziara ulaya na nchi zilizoendelea mkajifunze jinsi gani ya KUGAWA KEKI YA TAIFA KWA USAWA,.
Jamani keki ya Taifa haigawanywi kwa usawa,,,,hata sijui hao watu wanaopanga mishahara kama wamesoma au wanabuni tu kiwango cha mishahara????????
Tafadhari ofisi ya utumishi wa umma na wizara ya kazi na ajira mwende ziara ulaya na nchi zilizoendelea mkajifunze jinsi gani ya KUGAWA KEKI YA TAIFA KWA USAWA,.