Ukitaka kushangaa nenda Buza Tandika

Naomba uelewe kwanza Qur-an haina uhusiano na albadir, wala katika qur-an hakuna kitu kinaitwa albadir,na wala katika mafundisho ya uislam hakuna al badir sehem yeyote inapofundishwa,
Kwanza hakuna ukweli kama al-badir ina madhara yeyote ila tunachoamini huwa kweli,kwa sababu huyo anaekusomea albadir anasoma kitabu cha majina ya watu ambao walipigana katika vita ya Badri ndio maana kinaitwa al badir.ndani yake hakuna dua yeyote zaidi ya majina ya watu,ila kwa sababu tulishaamini toka enzi tunaumia kwa imani kuliko ukweli wenyewe

Asante sana mkuu kwa darasa zuri, watu wamekariri dini halafu wanataka kupotosha.
Uislam hauendi kwa mazoea bali dalili kutoka katika Quran na Sunnah.
 
mh mi sipo uko,wezi wote wa maeneo hayo wamekubaliana kabisa na,hili suala,,,albadil ni nouma mazeee!
 
Yanatokea hayo.Njooni Zanzibar maeneo ya mchina mwanzo, kuna ngombe zaidi ya 20. hawana mwenyewe wanazurura tu mpaka manispaa imewashindwa.kila mwaka wanaongezeka. inasemekana kuna ngombe kama watatu waliibiwa miaka mingi kidogo nyuma. mwenyewe akawasomea Albadiri.walioiba wakapukutika, tokea miaka hiyo ngombe hawana mwenyewe wanazurura na kuzaliana tu mitaani.kila mtu anawaogopa.mbaya zaidi mwenye mali alishatangulia mbele ya haki.kwa wale wasiomini Quraan Tukufu waje wachukue mali za bure.au wakachukue hiyo Toyo.


Mimi siji kuchukua naamini kweli Qurraan inaua. Hahahahahha
 
hapa Morogoro, kuna mbuzi, hao mbuzi wasikie kwenye radio tu. Nimeshuhudia kwa macho yangu wakifungua mfuko jalalani, na hawataki kula nyasi zao ni makombo yaliyobaki iwe wali twende, iwe ugali twende, iwe mabaki ya mboga twende ila nyasi no, Njoo moro uwaone, wanaishi mjini tu, SASA WEWE TUKA HUKO utokako NA KICHAA CHAKO umwIBe AU MGONGE NA GARI AU TUKUTUKU, Utauona moto wake
 
aiseeeee babaangu inaonekana ujasoma vizuri huu uzi rudia mara 3 ukija kuchukuwa upitie manzese ununue jeneza lako ili ukifa usiwape shida ndugu zako

Wacha uoga wewe ,hujasikia kitu inaitwa anti dote? basi mi nina ant-dote ya hayo mavitu!
Jaribu hii piga kojo kwenye ndoo ,kata na gogo ,fanya mkorogo mwepesi,changanya na unga wa majani ya mvuje,weka stand by bangi na mmavimavi.
siku ya kuuramba huo usafiri jikogeshe mkorogo wako kinyesi na mvuje ,jisugue na mmavimavi mwil mzima,jifukize bangi (usiivute!)
Na wakati muafaka ni pale fullmoon!yaani hapo mzee hata ukipelekwa peponi watu wote nduki wata kukimbia
wanakimbilia motoni!
kuna maneno yake ya kunuizia siwezi kuyaweka hadharani msije mkaniogopa bure!
 
Ile pikipiki Toyo kule Buza yaendelea kuumiza watu, kama mwezi hivi uliopita ilichukuliwa na kuvushwa reli halafu ikarudishwa pale pale halafu ikachukuliwa tena ikarudishwa. Wiki kama mbili hivi zilizopita ikachukuliwa tukajua hii ndio basi tena sasa jana imerudishwa palepale. Cha kushangaza juzi kabla haijarudishwa tulipita hapo tukakuta gari la wagonjwa ambulance likiwa na watu ndani mmoja wetu akasema usikute aliyeichukua pikipiki amekuja kuonyesha tatizo lilipomuanzia na si ajabu pikipiki atairudisha na kweli pikipiki imerudi palepale na iko vile vile hakuna kitu kilichopungua. Ama kweli watu dunia hii wabaya. Hili pia linaweza kuwa eneo la utalii.
 
weka na picha yake kabisa tutajua kama imepaki leo au mwezi uliopita
Bujibuji hii ngoma ni nzito, kama sio al badir itakuwa kuna kinyamkela au zindiko, naogopa hata kupiga picha nyingine.
 
Last edited by a moderator:
Yanatokea hayo.Njooni Zanzibar maeneo ya mchina mwanzo, kuna ngombe zaidi ya 20. hawana mwenyewe wanazurura tu mpaka manispaa imewashindwa.kila mwaka wanaongezeka. inasemekana kuna ngombe kama watatu waliibiwa miaka mingi kidogo nyuma. mwenyewe akawasomea Albadiri.walioiba wakapukutika, tokea miaka hiyo ngombe hawana mwenyewe wanazurura na kuzaliana tu mitaani.kila mtu anawaogopa.mbaya zaidi mwenye mali alishatangulia mbele ya haki.kwa wale wasiomini Quraan Tukufu waje wachukue mali za bure.au wakachukue hiyo Toyo.

Tukisema hiyo dini ni ya shetani watu mapovu yanawatoka. Huhitaji kuwa na PhD kulitambua hilo.
 
Hata kule Malawi unapotokea mji wa Karonga kuna Mlima mmoja mkali sana kama unaenda Mzuzu hapo napo kuna Ng'ombe wengi hawana mwenyewe na kuna kibao kinatahadharisha magari kuwa makini wanapoendesha magari yao nasikia hao ng'ombe mwenyewe alitangulia mbele ya haki lakini hawaguswi ,ukijaribu tu ndio mwisho wa kupta oxygen,ngozi nyeusi kwa haya mambo ni nambari wani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom