Columbus
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 2,002
- 648
Buza kuna pikipiki Toyo ya matairi matatu imepaki pembeni ya barabara yapata mwaka sasa baada ya kuuliza kulikoni nikaambiwa hiyo Toyo imeshauwa watu sita. Wezi waliiba na waliohusika na hiyo Toyo walianza kufa mmoja baada ya mwingine walipofika sita ndugu zao waamua kuileta hapo barabarani wakaitelekeza.
Wakati barabara inajengwa aliletwa shehe aruhusu iwekwe pembeni baada ya kujenga ikarudishwa palepale mpaka hivi leo, tuliendelea kushangaa.
Tuliendelea kumuuliza jamaa mmoja akadai mwenye hiyo Toyo yake hawezi kwenda kuichukua kwa sababu ilishasomewa kitabu yaani Al badir na kama akienda kuichukua na yeye anakufa, hii imekaaje?
Nikifanikiwa kupita tena huko nitawawekea picha hapa.
Wakati barabara inajengwa aliletwa shehe aruhusu iwekwe pembeni baada ya kujenga ikarudishwa palepale mpaka hivi leo, tuliendelea kushangaa.
Tuliendelea kumuuliza jamaa mmoja akadai mwenye hiyo Toyo yake hawezi kwenda kuichukua kwa sababu ilishasomewa kitabu yaani Al badir na kama akienda kuichukua na yeye anakufa, hii imekaaje?
Nikifanikiwa kupita tena huko nitawawekea picha hapa.