BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Date::11/19/2008
Waziri asihi vyombo vya habari kuachana na habari za EPA, migomo ya walimu
Festo Polea na Kuruthum Ahmed
Mwananchi
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwamtumu Mahiza amevitaka vyombo vya habari nchini kuachana na habari zinazohusu sakata la wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje, (EPA) pamoja na masuala ya migomo ya walimu kwa madai kuwa masuala hayo tayari yametafutiwa ufumbuzi.
Badala yake alivitaka vyombo hivyo kuelekeza nguvu hizo katika habari nyingine ikiwa ni pamoja na kufichua na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanafunzi.
Waziri Mahiza alisema hayo jana wakati akizindua kampeni ya Jifunze bila woga iliyofadhiliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Plan-Tanzania yenye lengo la kupinga ukatili wa kijinsia mashuleni.
Mahiza alisema anachukizwa kuana masuala ya EPA na migomo ya walimu ikishikiliwa bango kila kukicha wakati tayari malalamiko hayo yamefika mwisho kwa sababu walimu wameanza kulipwa na watuhumiwa wa EPA wameshafikishwa Mahakamani.
Sasa tubadilishe CD, kila wakati EPA na migomo ya walimu, waandishi wa habari na vyombo vya dola tubadilike, mimi nikiona mnalivalia njuga kwa kufichua masuala ya unyanyasaji wa kijinsia, kuwafichua waharibifu wa wanafunzi, kisha wakakamatwa nitafurahi sana, alisema Waziri Mahiza
Mahiza alitumia nafasi hiyo kulaani walimu wote wanaoharibu watoto kijinsia kwa kutumia udhaifu wa wanafunzi wa kike na kiume kwa kuwarubuni kwa kuwapa vitu vinavyowashawishi kama Simu na magari.
Alisema masuala ya ukatili wa kijinsia yanaongezeka licha ya kukemewa mara kwa mara.
Aliwataka viongozi wa dini mbalimbali nchini kuandaa makongamano yenye lengo la kuombea laana walimu na watu wengine wanaorubuni wanafunzi bila kujali maisha yao ya baadae.
Waziri asihi vyombo vya habari kuachana na habari za EPA, migomo ya walimu
Festo Polea na Kuruthum Ahmed
Mwananchi
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwamtumu Mahiza amevitaka vyombo vya habari nchini kuachana na habari zinazohusu sakata la wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje, (EPA) pamoja na masuala ya migomo ya walimu kwa madai kuwa masuala hayo tayari yametafutiwa ufumbuzi.
Badala yake alivitaka vyombo hivyo kuelekeza nguvu hizo katika habari nyingine ikiwa ni pamoja na kufichua na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanafunzi.
Waziri Mahiza alisema hayo jana wakati akizindua kampeni ya Jifunze bila woga iliyofadhiliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Plan-Tanzania yenye lengo la kupinga ukatili wa kijinsia mashuleni.
Mahiza alisema anachukizwa kuana masuala ya EPA na migomo ya walimu ikishikiliwa bango kila kukicha wakati tayari malalamiko hayo yamefika mwisho kwa sababu walimu wameanza kulipwa na watuhumiwa wa EPA wameshafikishwa Mahakamani.
Sasa tubadilishe CD, kila wakati EPA na migomo ya walimu, waandishi wa habari na vyombo vya dola tubadilike, mimi nikiona mnalivalia njuga kwa kufichua masuala ya unyanyasaji wa kijinsia, kuwafichua waharibifu wa wanafunzi, kisha wakakamatwa nitafurahi sana, alisema Waziri Mahiza
Mahiza alitumia nafasi hiyo kulaani walimu wote wanaoharibu watoto kijinsia kwa kutumia udhaifu wa wanafunzi wa kike na kiume kwa kuwarubuni kwa kuwapa vitu vinavyowashawishi kama Simu na magari.
Alisema masuala ya ukatili wa kijinsia yanaongezeka licha ya kukemewa mara kwa mara.
Aliwataka viongozi wa dini mbalimbali nchini kuandaa makongamano yenye lengo la kuombea laana walimu na watu wengine wanaorubuni wanafunzi bila kujali maisha yao ya baadae.