Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni

hermes

Member
Jul 15, 2010
17
0
Ilikuwa jana usiku katika taarifa ya habari nilipo shuhudia watu wakishangilia kukubaliwa na kupitishwa kwa sheria ya kuruhusu ndoa ya jinsia moja huko Argentina.Nilishangaa nilipo sikia kuwa si Argentina pekee Duniani iliyo pitisha sheria hiyo tu!kumbe kunanchi nyingine saba zilizo pitisha pia.Nikabaki nashangaa tu! na kujiuliza maswali mengi kichwani hivi kwani humu dunianai kuna idadi kubwa ya Wanawake kuliko Wanaume au kuna idadi kubwa ya Wanaume kuliko Wanawake mpaka inafikia hatua watu wa jinsia moja wanaowana, na inakuwaje na wanafanyaje tendo la ndoa.inasikitisha sana kuona jambo hilo.Na sijui itakuwaje siku ya mwisho pindi watakapoulizwa kuhusu jambo hilo kwa maana Mungu kakataza kitu hicho.Nazipa sifa kubwa nchi za kiarabu kwa misimamo yao mikali kuhusu jambo hilo.:crying:
 
hivi jamani kwa hakuna wachangiaje kwa maana sioni mchangiaji.Au mnalikubali jambo hilo!!
 
Hayo yote yanaletwa na kukosa hofu ya MUNGU. Pole pole Tanzania kuna mashoga tayari, watakapokuwa wengine nao wataanza kuidai hiyo sheria.
 
Dunia ya leo imekuwa kama Sodoma na Gomora. watu wengi sasa ni wagonjwa wa akili na roho. Usione watu wanatembea na kuongea wamevaa vizuri ukadhani wote ni wazima. Wengi wagonjwa! Mbaya zaidi hawajui kama wagonjwa, wanadhani ni fasheni, ni maendeleo, ni kwenda na wakati, nk. Na wanataka dunia yote iwafuate huko upotevuni.
Pili, kuna hili la kutafuta raha/anasa ya pekee. Watu wanajaribu kufanya mapinduzi katika uwanja wa ngono ili wapate kile ambacho hakijawazwa na wengi. Hawaoni kama heterosexual relations zina cha pekee. Wanataka upekee, na huo upekee ndo umewafikisha kwenye hayo maushoga, na maulezibiani. Wakishazoea ndo hapo wanataka kuhalalisha kisheria. Na wanaelekea kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani serikali na wagonjwa wengine katika jamii wanawatetea. Tumwombe Mungu atusaidie na balaa hili.
 
Hivi wewe unadhani Bwana Yesu alipokuwa akitabiri hali ya siku za mwisho, zitakuwa kama ilivyokuwa siku za sodama alikua anatania? Na sii afadhali kwa wana siasa kupigia chupuo jambo hilo kuliko ilivyo sasa hivi. Kuna mashetwani yaliyojivalisha kanzu madhabahuni wakijinadi kama watumishi wa mungu, na kuridhia jambo hilo. Na visa vya kufunga ndoa za jinsia moja katika yale madanguro yanayojiita kanisa vimekwisha ripotiwa. (haya ni mashetani yale yaliyosemwa yanamwamini Mungu na kutetemeka mbele zake lakini hayana tabia. Ni makanaji ya nguvu za Mungu)
 
Back
Top Bottom