Mzee Kibiongo
JF-Expert Member
- Jun 18, 2008
- 241
- 4
Kuna huyu mkuu wa benki ya Posta amestaafu tangu 26/11/2009 lakini hadi leo hii bado tunamuona anaingia ofisini kama kawaida na anadunda mzigo kama zamani. Nimejuzwa kuwa hana barua ya kumwongezea mkataba wala barua ya ajira, lakini eti anasubiri barua toka serekalini kwa maana aliahidiwa na bodi yao kuwa atapewa barua ya mkataba mwingine. Huyu alistaafu rasmi mwaka 1997 baadaye akapewa mkataba wa miaka mitatu na ameendelea hivyo hivyo na mikataba hadi hiyo 26/11/2009 mkataba wake wa nne ulipomalizika. Sasa fikiria ana umri gani.
Mshahara wa desemba kakunja bila mkataba, benki ina wakuu wa vitengo vya fedha, sheria, ukaguzi wa ndani, rasilimali-watu nk. lakini wako kimya. Je, tuelewe kuwa wanatafuna naye jasho la wafanyakazi wanyonge au anatumia nguvu za giza. Vyombo husika, wizara ya fedha, benki kuu, bodi ya wakurugenzi wote kimyaa !!!!!!!!!!!! Jamaa kaoa mke toka Mlingotini sijui ndiyo maana wote hao hawaoni ndani wamezibwa macho na akili na ujasiri. Maamuzi yake hayana difference na yule mkuu wa ile nyumba kubwa ya kule Zimbambwe, yaani ni ubabe juu ya ubabe ukifanya fyoko kazi huna. Lo!! poleni sana wana benki ya posta maana hamna pa kulilia, mzazi wenu bodi naye kapigwa kipapai haoni ndani ila kadata tu kama panya aliye banwa na mlango.
Wanajamvi nimewatonya haya machache ili tusaidiane kuyafanyia utafiti wa kina kuona uhalali wa kikongwe kuendelea kukaa ofisini na kutafuna mihela ya wavuja jasho bila barua yoyote na kufanya maamuzi ambayo mimi nayaite kuwa ni BATILI. Tumwambie waziwazi kuwa ONDOKA OFISINI BWANA. Umestaafu, BASI INATOSHA.
Jamani tusichoke kupiga kelele hadi kieleweke.
Nasubiri michango yenu.
Mshahara wa desemba kakunja bila mkataba, benki ina wakuu wa vitengo vya fedha, sheria, ukaguzi wa ndani, rasilimali-watu nk. lakini wako kimya. Je, tuelewe kuwa wanatafuna naye jasho la wafanyakazi wanyonge au anatumia nguvu za giza. Vyombo husika, wizara ya fedha, benki kuu, bodi ya wakurugenzi wote kimyaa !!!!!!!!!!!! Jamaa kaoa mke toka Mlingotini sijui ndiyo maana wote hao hawaoni ndani wamezibwa macho na akili na ujasiri. Maamuzi yake hayana difference na yule mkuu wa ile nyumba kubwa ya kule Zimbambwe, yaani ni ubabe juu ya ubabe ukifanya fyoko kazi huna. Lo!! poleni sana wana benki ya posta maana hamna pa kulilia, mzazi wenu bodi naye kapigwa kipapai haoni ndani ila kadata tu kama panya aliye banwa na mlango.
Wanajamvi nimewatonya haya machache ili tusaidiane kuyafanyia utafiti wa kina kuona uhalali wa kikongwe kuendelea kukaa ofisini na kutafuna mihela ya wavuja jasho bila barua yoyote na kufanya maamuzi ambayo mimi nayaite kuwa ni BATILI. Tumwambie waziwazi kuwa ONDOKA OFISINI BWANA. Umestaafu, BASI INATOSHA.
Jamani tusichoke kupiga kelele hadi kieleweke.
Nasubiri michango yenu.