Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,360
Kampuni ya Quality Finance Corparation Ltd (QFC) amefungua madai ya fidia ya Sh. bilioni 18.7 Mahakama Kuu ya Tanzania dhidi ya Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, kama hasara kwa kiuka makubaliano ya mkopo katika ya yao Septemba 12, 2005.
Kadhalika, kampuni ya QFC, imeomba mahakama itoe amri kwa kampuni ya Kagoda kulipa riba ya fedha iliyozidishwa.
Kupitia hati ya madai hayo pia, kampuni ya QFC, imeomba kulipwa fidia ya hasara na usumbufu kutokana na mahakama itakavyoamua.
Katika madai ya msingi, mlalamikaji aliingia kwenye makubaliano ya mkopo na mlalamikiwa Septemba 12, 2005, ambapo alipokea Sh. 31,710,000,000 ambao ulitakiwa kurejeshwa na riba kwa miaka mitatu.
Ilidaiwa kuwa makubaliano hayo yalitekelezwa nusu. Mlalamikaji alipokea Sh. bilioni 31.7 kama mkopo ambapo aliweza kurejesha Sh. 18,710,000,000 kama walivyokubaliana kwenye mkataba wao.
Ilidaiwa kuwa Januari, 2008 mlalamikaji alijulishwa na mamlaka husika kwamba kumegundulika ukiukwaji wa taratibu kwenye vyanzo vya fedha hizo.
Aidha, baada ya taarifa hiyo, mlalamikaji alilazimika kuzirejesha Sh. bilioni 31.7 ambapo alilipa zaidi kwa kuzidisha Sh. bilioni 18 ambazo alimlipa mlalamikiwa na kujikuta anapata hasara.
Hata hivyo, baada ya mlalamikaji kumtaka mlalamikiwa kumtejeshea zile fedha za ziada jitihada hizo hazikuzaa matunda hivyo anaiomba mahakama kumuamuru amlipe kabla ya muda wa makubaliano haujapitwa na wakati. Kupitia hati ya madai, mlalamikaji anaona ana haki ya kulipwa hasara hiyo aliyoipata kutoka kwa mlalamikiwa, kwa kuwa kitendo hicho kimemvunjia hadhi na heshima kwa jamii.
Mlalamikaji ameomba mahakama itoe amri ya kumrejeshea Sh. bilioni 18.7 na riba ya asilimia 18 kwa fedha hizo tangu siku mkataba ulipokosewa hadi siku hukumu itakapotolewa. Pia, hasara za jumla alizozipata, gharama za kuendesha kesi vyote vilipwe na mlalamikiwa pamoja na malipo mengine ambayo mahakama itaona yanafaa kufanyika.
CHANZO: NIPASHE
Kadhalika, kampuni ya QFC, imeomba mahakama itoe amri kwa kampuni ya Kagoda kulipa riba ya fedha iliyozidishwa.
Kupitia hati ya madai hayo pia, kampuni ya QFC, imeomba kulipwa fidia ya hasara na usumbufu kutokana na mahakama itakavyoamua.
Katika madai ya msingi, mlalamikaji aliingia kwenye makubaliano ya mkopo na mlalamikiwa Septemba 12, 2005, ambapo alipokea Sh. 31,710,000,000 ambao ulitakiwa kurejeshwa na riba kwa miaka mitatu.
Ilidaiwa kuwa makubaliano hayo yalitekelezwa nusu. Mlalamikaji alipokea Sh. bilioni 31.7 kama mkopo ambapo aliweza kurejesha Sh. 18,710,000,000 kama walivyokubaliana kwenye mkataba wao.
Ilidaiwa kuwa Januari, 2008 mlalamikaji alijulishwa na mamlaka husika kwamba kumegundulika ukiukwaji wa taratibu kwenye vyanzo vya fedha hizo.
Aidha, baada ya taarifa hiyo, mlalamikaji alilazimika kuzirejesha Sh. bilioni 31.7 ambapo alilipa zaidi kwa kuzidisha Sh. bilioni 18 ambazo alimlipa mlalamikiwa na kujikuta anapata hasara.
Hata hivyo, baada ya mlalamikaji kumtaka mlalamikiwa kumtejeshea zile fedha za ziada jitihada hizo hazikuzaa matunda hivyo anaiomba mahakama kumuamuru amlipe kabla ya muda wa makubaliano haujapitwa na wakati. Kupitia hati ya madai, mlalamikaji anaona ana haki ya kulipwa hasara hiyo aliyoipata kutoka kwa mlalamikiwa, kwa kuwa kitendo hicho kimemvunjia hadhi na heshima kwa jamii.
Mlalamikaji ameomba mahakama itoe amri ya kumrejeshea Sh. bilioni 18.7 na riba ya asilimia 18 kwa fedha hizo tangu siku mkataba ulipokosewa hadi siku hukumu itakapotolewa. Pia, hasara za jumla alizozipata, gharama za kuendesha kesi vyote vilipwe na mlalamikiwa pamoja na malipo mengine ambayo mahakama itaona yanafaa kufanyika.
CHANZO: NIPASHE