Ukipewa kuongoza nchi...

Annina

JF-Expert Member
Nov 15, 2009
437
57
Kwa kawaida kila kiongozi huwa ana malengo ya kufikia katika kipindi cha uongozi wake, malengo hayo ndio huzaa mipango, mikakati, majukumu na utendaji a kila siku. Mara nyingi viongozi wetu huwa na malengo yanayofanana...kuboresha hali za maisha ya wananchi. Tofauti inakuja katika mipango, mikakati na utekelezaji wake katika kufikia lengo.

Nikipewa idhini ya kuongoza nchi yetu, nitakuwa na agenda mbili tu kama msingi wa kufikia lengo la kuboresha maisha ya wananchi.

1. Chakula cha kutosha kwa kila kinywa
2. Uhuru wa kutoa maoni kwa kila mwananchi


Nakaribisha maoni


Annina
 
Natofautiana Nawe kidogo Annina,
Labda hili nalotofautiana nawe ndilo laweka Upinzani.....

Mimi naamini hili katika Uongozi
1. Naamini Katika Uongozi uletao Maendeleo Hakuna Demokrasia ya 100% katika Uongozi......Ukitoa Uhuru asilimia 100% wa kila mwananchi
naamini Uongozi utakuwa Mzigo and mgumu Badala yake....Mimi kama kiongozi Mwenye Malengo na Dira iliyonipelekea kutaka nafasi
kuwaletea Maendeleo Wanajamii wangu, Pamoja na Work force nitakayo iandaa, Nitahakikisha kushirikiana na maoni yenye akili ya
wawakilishi wa wananchi yanakuwa priority, na Maswala yote ya msingi yanafanyiwa kazi.

2. Mfumo nitakaotumia kukusanya Maoni hautakuwa wa mabishano na usio na utaratibu, Naona sasa watu hawabishani kujenga bali
kuzodoana, kukejeliana na kuharibu, Kupakana matope n.k

3. Nina hisia kuwa Ili TZ iendelee inahitaji Kkiongozi mwenye chembe chembe za Udikteta fulani, ambae Anaweka nnchi mbele....Uki messUp
hauna Maisha, and uwadabishaji maradufu. Kiongozi asiehitaji Udhibitisho (physically) wa ubadilifu bali mazingira yanapo weka mashaka tu
na hauna maelezo yakinifu....( you pay for your doings)

VIPAUMBELE VYANGU:
1. Infrastructure ( Mfano Dar nabomoa na kubuni altenative roads, Barabara za kiwango na za muda mrefu.

2. Kujengea uwezo Vijana na watoto Kuwa na spirit ya Uthubutu......(Yes I can spirit), kujitambua wanaweza and kufanya kazi kwa bidii

3. Kilimo........Ku-modernise Kilimo cha Umwagiliaji.............

NAENDELEA KUTAFAKARI................
 
Back
Top Bottom