Ukimya wa upinzani katika Matukio yanayotokea nchini, kulikoni?

Nimekuwa nikifuatilia harakati za Chadema kwa muda mrefu sasa, linapokuwa linatokea jambo gumu linalohusu Taifa Chama hiki maarufu kimekuwa nyuma sasa kutoa msimamo wao. Mfano tukio la Mbagala na Zanzibar, haya kila mtu anayajua jinsi yalivyotokea lakini Chama makini bado wao hawajasikia hayo matukio labda wapo mbali na vyombo vya habari kama walivyosema. Mimi nafikiri kama kunakuwepo na mkutano sehemu ni bora wanachama tukawajulisha kabla hawapanda jukwaani ili jambo la kwanza kiongozi apandapo jukwaani aonyeshe basi kuguswa hata kama haguswi. Wananchi wanaotarajiwa kuongozwa ndo hao hao wanaopatwa na majanga kama hayo tuwaliwaze hata kwa kauli ambazo tunajua ni danganya kubwa, kwa haya viongozi wa Chadema siwatofautishi na Rais Kikwete.



Kinga ni bora kuliko tiba

Mbona cdm hawatoi tamko kuhusu ndoa ya katibu wao mkuu
 
Nimekuwa nikifuatilia harakati za Chadema kwa muda mrefu sasa, linapokuwa linatokea jambo gumu linalohusu Taifa Chama hiki maarufu kimekuwa nyuma sasa kutoa msimamo wao. Mfano tukio la Mbagala na Zanzibar, haya kila mtu anayajua jinsi yalivyotokea lakini Chama makini bado wao hawajasikia hayo matukio labda wapo mbali na vyombo vya habari kama walivyosema. Mimi nafikiri kama kunakuwepo na mkutano sehemu ni bora wanachama tukawajulisha kabla hawapanda jukwaani ili jambo la kwanza kiongozi apandapo jukwaani aonyeshe basi kuguswa hata kama haguswi. Wananchi wanaotarajiwa kuongozwa ndo hao hao wanaopatwa na majanga kama hayo tuwaliwaze hata kwa kauli ambazo tunajua ni danganya kubwa, kwa haya viongozi wa Chadema siwatofautishi na Rais Kikwete.



Kinga ni bora kuliko tiba
HIVI CCM wameshatoa tamko ati! this is another one ended open mind
 
Hii imenikumbusha kisa kimoja cha rafiki aliyekuwa bar akinywa na rafiki yake polisi, akaanzisha ugomvi na wanajeshi akitegemea polisi amsaidie. Mmelikoroga mlinywe wenyewe sio mnatafuta msaada kwa CDM.
 
Watoe tamko wakati wanashabikia Chezea christian democratic movement walishasema nchi haitatawalika tumeona juhudi zao.Dini ndani ya siasa hao ndo chadema bwana
 
Mkuu tata mura kipi cha muhimu kwako...

CDM kutoa tamko AU serikali iliyopo madarakani kudhibiti huu upotofu??
 
Mnapenda matamko sana?
Yameshatolewa mengi tu, hayajawatosha bado?

Mpaka CHADEMA waongee ndo mjisikie raha sio?
 
Tata mura tatiga muraaa:

Chadema na mbagala wapi na wapi????????
Yaliotokea mbagala na zanzibar ni mambo ya kiimani za kidini na wala sio maswala ya kdunia (mambo ya kiserikali); hapo kaka utakuwa umepotea kabisa;






nimekuwa nikifuatilia harakati za chadema kwa muda mrefu sasa, linapokuwa linatokea jambo gumu linalohusu taifa chama hiki maarufu kimekuwa nyuma sasa kutoa msimamo wao. Mfano tukio la mbagala na zanzibar, haya kila mtu anayajua jinsi yalivyotokea lakini chama makini bado wao hawajasikia hayo matukio labda wapo mbali na vyombo vya habari kama walivyosema. Mimi nafikiri kama kunakuwepo na mkutano sehemu ni bora wanachama tukawajulisha kabla hawapanda jukwaani ili jambo la kwanza kiongozi apandapo jukwaani aonyeshe basi kuguswa hata kama haguswi. Wananchi wanaotarajiwa kuongozwa ndo hao hao wanaopatwa na majanga kama hayo tuwaliwaze hata kwa kauli ambazo tunajua ni danganya kubwa, kwa haya viongozi wa chadema siwatofautishi na rais kikwete.



Kinga ni bora kuliko tiba
 
Kuna tamko gani zaidi tunalolihitaji tena zaidi ya kuambiwa DHAIFU? Iliyobaki ni sisi kuchukua hatua stahiki.
 
Mwenyekiti wa CDM, Freeman Mbowe alishawahi kuionya serikali ya CCM na Rais juu ya propaganda za udini na ukanda wanazofanya dhidi ya Chadema, wenye akili tulimuelewa, Wabunge wa CCM wakafanya ni siasa.

Sasa unataka CDM waseme nini wakati walishatahadharisha mapema?
 
Kitendo cha kuitaka CDM itoe tamko ni sawa na kitendo cha wabunge wa CCM kuanza kujadili kwa upana maoni ya bajeti ya kambi ya upinzani kuliko bajeti yenyewe iliyowasilishwa na serikali! CDM hata ikiongeza tamko hapo, kama serikali haitakuwa willing kutekeleza basi itakuwa hakuna maana, kwani serikali ndiyo yenye dola!
 
Hivi kwanini sisi hatutaki kuzipa ushirikiano akili zetu?

-Wapi CHADEMA waliweka mkataba na wananchi kuhusu mustakabali wao wa Taifa, kuhusu amani na utulivu?

-Okay, Let's say wametoa tamko, halafu?

-Wakati wakiwa wanatoa "tamko", Serikali inafanya nini? ---Kama wananchi Tunafanya nini?

-Hili suala chanzo chake ni mambo ya kidini, so litasuluhishwa kwa njia za kidini! CHADEMA,au chama chochote cha siasa kuongea (kwa watanzania sisi wenye kuwa na ugumu wa kuzishughulisha akili zetu tutasema, Chama fulani kipo nyuma ya jambo hili)..Acha nao(Hao CHADEMA)wajisafiahe kwa njia hiyo, maana kila vurugu wao ndio wamesababisha!

Kwani siyo serikali hii hii, ilikuwa iko tayari kuingia vitani kwa gharama yeyote kwa ajili ya mpaka?..Ikisema "NGUVU ipo"!!?..Kwanini nguvu hiyo hiyo isitumike kuwadhibiti hao waandamanaji(bila ulinzi), ina maana haiwajui?

Rais yuko wapi?Makamu wake? W/mkuu? Waziri wa Mambo ya ndani? Waziri wa Ulinzi? Wasaidizi(Manaibu) wao? Mkuu wa Jeshi la Polisi?..wao wamefanya nini?
Hawajui?

Si kila jambo huitaji mazoea, tufanye wajibu wetu kila mtu kwa nafasi yake.
 
Huyo mjinga mleta mada aje na tamko la ccm na nape toka rumumba kwanza ndio aiseme cdm. Anataka cdm waseme halafu waseme cdm inawachukia waislaam. Wakisema nongwa, wakikaa kimya nongwa. Mmelianzisha wenyewe limalizen wenyewe.
 
Hayo si mambo magumu kama akili yako inavyokutuma, huu ni UDINI. CDM iko mbali na upuuzi huo!
 
Viongozi wenye busara huzungumzia au kutoa tamko mahali na wakati unaofaa hivyo naona kwa viongozi wa vyama vya upinzani hasa CDM na CUF kukaa kimya ni sahihi zaidi kutokana na mazingira ya tukio, wakati na uelewa wa watu katika masuala mbalimbali. Wangekuwa wameshatoa tamko sasa hivi kukngekuwa na matusi, kejeli na maneno kutoka kwa watu mbalimbali kwani tumeona hili kwenye tukio la Morogoro, Iringa na kwingineko. Hata hivyo matamko katika hali hii yanapaswa kutolewa na viongozi wa dini na serikali na si vyama vya siasa, vile vile matamko tu hayasaidii isipokuwa matendo hasa mema.
 
Nimekuwa nikifuatilia harakati za Chadema kwa muda mrefu sasa, linapokuwa linatokea jambo gumu linalohusu Taifa Chama hiki maarufu kimekuwa nyuma sasa kutoa msimamo wao. Mfano tukio la Mbagala na Zanzibar, haya kila mtu anayajua jinsi yalivyotokea lakini Chama makini bado wao hawajasikia hayo matukio labda wapo mbali na vyombo vya habari kama walivyosema. Mimi nafikiri kama kunakuwepo na mkutano sehemu ni bora wanachama tukawajulisha kabla hawapanda jukwaani ili jambo la kwanza kiongozi apandapo jukwaani aonyeshe basi kuguswa hata kama haguswi. Wananchi wanaotarajiwa kuongozwa ndo hao hao wanaopatwa na majanga kama hayo tuwaliwaze hata kwa kauli ambazo tunajua ni danganya kubwa, kwa haya viongozi wa Chadema siwatofautishi na Rais Kikwete.



Kinga ni bora kuliko tiba

Matukio ni ya KISIASA AU KIJAMII.we huoni kama huu ni mtego.MAGAMBA WAMESEMA NN MBONA HUWAULIZI.
 
Kimsingi nimependa wachangiaji ambao wao wanajenga hoja ama kupinga au kushauri au kuunga mkono kama ndugu ENZIHURU,NORBITI na MCHUNGAJI nyie mnafaa kuzungumza siasa safi sana pia sipendi tabia ya kuropoka ropoka kama ndugu MWANAMTOKAPABAYA neno umetumwa pia sipendi matusi na kashifa kama ndugu KANIGINI kwani tabia ya mtu mwenye matusi na kashifa ni sifa ya mtoto wa zinaa.

funguka mkuu......
 
Hili ni tatizo la udini, Tatizo ambalo muasiasi wake ni Kikwete na CCM yake.

Ni sera za CCM na kikwete katika kujipatia kura wakiwatapeli watanzania kwa misingi ya Udini, Ukabila na Ukanda.

Chadema Inathamini watanzania wote kwa utanzania wao na imani ya mtu sio sera ya Chadema ni jumkumu lake mtu binafsi.

Ni busara ya kawaida kabisa kwamba Chadema haiwezi kuhubili na haiwezi kuingilia sera za kikwete na ccm.

CCm na Kikwete washugulikie wenyewe moto waliouanzisha yaani, sera ya udini na matokeo yake kwa sababu

matunda yake wanayafahamu si wapo madarakani na wanakula inchi?
 
Back
Top Bottom