Ukimya wa Kamati ya Usalama na Ulinzi ya Bunge...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...

Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.


Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....
 
Kamati hii ina interest kwenye uonevu unaofanywa na vyombo vya Ulinzi na Usalama,hivyo kukosa legitimacy ya kuhoji
Jambo moja tu linalowaunganisha watawala na ccm ni maslahi,yaani kila mmoja kwa nafasi yake ana maslahi kwenye hili,kwa kuwa polisi wanaua ili kuwalinda wao,pamoja na kamati hii
 
Kamati hii ina interest kwenye uonevu unaofanywa na vyombo vya Ulinzi na Usalama,hivyo kukosa legitimacy ya kuhoji
Jambo moja tu linalowaunganisha watawala na ccm ni maslahi,yaani kila mmoja kwa nafasi yake ana maslahi kwenye hili,kwa kuwa polisi wanaua ili kuwalinda wao,pamoja na kamati hii

Ni kweli kabisa, laiti hii kamati ingefanya kazi sawa sawa na jina lake! usalama ingekuwa mboni ya kazi zake, na ulinzi ungekuwa msingi.

Watu wamelindwaje kwa kuuawa,
pana usalama gani kama wapaswao kuhakikisha huo usalama ndio wanautowesha na kudai sheria ifuatwe. wao hawakufuata sheria, bali wenzao ndio wafuate. Tuwaondoe jeshini.

Hakika ccm ni adui kuliko njaa.
 
Mpaka wa Malawi na Tanzania uligusa maslahi ndo maana
kamati ilisema, haya mengine ni kama kelele za mlango...
 
Dhaifu nani hapo? Huyo Lowassa unayemsema ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na usalama. Mbona unajichanganya mwenyewe? Tatizo ni kwamba Kamati hiyo inaongozwa na watu wanaoota uchaguzi Mkuu 2015 na kwamba wao watakuwa na nafasi gani au watakuwa wapi kisiasa hivyo kero kubwa kama hizi ambazo zinahusu uhai wa binadamu ambao wanatamani kuwaongoza japo sijui kama wanasifa hizo, wanaona hazina maana na hawana muda wa kuzisemea au kuzikemea. Wanatamani makubwa majukumu makubwa zaidi ilhali kwa hayo madogo wanaonekana kupwaya. Mimi nadhani Wabunge pia wawe makini kuchagua Wajumbe wa Kamati husika pamoja na viongozi wa Kamati hizo kwa maana ya Mwenyekiti na Makamu wake. Wakiwa wanachaguana kwa malengo ya kuimarishana kisiasa zaidi kuliko kutumikia umma, hakika nchi yetu itazidi kuwa nyuma kwa mambo mengi.
 
Kimsingi kamati hii ni tawi la ccm na usitegemee itakemea mauaji yanayoendelea nchini kwa maana yanabaraka zote za serikali na chama tawala kwa maslahi yao. Nikijaribu kuichunguza pamoja na kamati nyingine na vyombo vya dola ninachokigundua ni kwamba wanashindwa hata kukemea mambo ambayo yako wazi mno mpaka watu wanajiuliza kuna umuhimu wa kuwa na kamati kama hizi? Matokeo yake bila kujijua hutumia nguvu kubwa kubadili ukweli uwe uongo ili kutimiza matakwa yao ya kisiasa. Ulitegemea kamati hii iseme nini wakati walishajiandaa kwa mfano kusema kuwa chadema ni chama cha kigaidi, kinatumia mabomu na polisi tayari waliisha sema hivyo wakaja kuumbuka na picha ambazo zilipigwa eneo la tukio. Ndani na chini ya serikali ya chama cha ccm hamna kamati wala chochote kile kitakachokemea kuuwawa kwa raia ambako kunalenga kudhoofisha vyama vingine vya siasa?
 
Hapo ndio ukweli wa nafsi za hawa wataka urais unapoujua! Wanachagua matukio ya kujitokeza kwa manufaa yao.Hawafai hata kidogo kutuongoza!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Inawezekana hili haliwahusu. Kabla ya hili la Malawi, kuna wakati walikuwa wanaongelea lile la Morocco kwa hiyo inawezekana wanashughulika na masuala ya namna hiyo!
 
Mkuu hii kamati ni changa la macho tu. imewekwa ki-geresha tu kutimiza pengine hitajio la kisheria hasa hizi za kimataifa. lakini ukweli wa mambo ni kwamba hii kamati ni bora isingekuwepo maana inatia hasira tu. HAWA ccm MAJAMBAZI/WAUAJI/MAFISADI YAMEJIANDAA KUTUMALIZA WATANZANIA, WATANZANIA TUAMKE KABLA HAYA MAHALIFU HAYAJATUZIDI NGUVU INGAWA NAAMINI HAWAWEZI KUUSHINDA UMMA UNAODAI HAKI ZAKE.
 
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...

Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.


Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....[/QUOTE]

Naamini Mwenyekiti wa Kamati hii na wajumbe wake haya maonevu kwa wananchi wasiokuwa na hatia kwao siyo issue; kama lengo ni KIKOMBE KIKUBWA (mfano-URAIS katika uchaguzi ujao) suala la kunipatia kusikika KIMATAIFA japo katika UKANDA wa jirani na nchini kwangu na kuweza kuwaonesha WANANCHI WA NCHINI KWANGU NAWEZA KUSIMAMA KAMA AMIRI JESHI MKUU KATIKA KIPINDI KIHITAJICHO MAAMUZI MAGUMU (mfano VITA) inakuwa na POINT ZAIDI kwa mpango wa kutafuta KOMBE KUBWA.

KWa ufupi, yatokeayo ndani ya nchi kwa mwananchi wa kawaida siyo ISSUE kwao hususani kama haijaathiri MIPANGO YAO....
 
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...

Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.


Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....

I once thought that Lowasa is the best president we will never have....but not anymore...
 
Huu usalama wa ndani hauna mileage kwa aspirants kama akina Lowassa, Sitta, Membe, Makinda na wengine ndani ya CCM.

Wao ni kuangalia mambo yao binafsi na ya chama chao tu, no more no less.

Pole ndugu yangu MM kwa kuwapa heshima na dhamana kubwa kiasi hicho wasiostahili.
 
Mzee MMK, hiyo ni analysis kubwa sana. Hii kamati ipo kimya sana,

Ila nadhani wanatekeleza majukumu yao ingawa sisi tunaona kama hawafanyi. Pengine hivi ilivyo ndio malengo ya kamati husika. Nadhani kuna haja ya kujua majukumu yao kwanza!
 
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...

Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.


Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....

Imedhihirika kuwa hao ni wauza sura tu!
Sana sana macho yao yameelekezwa 2015 na kama uchumi ulivyobinafsishwa na siasa inaendeshwa kwa mafao binafsi, si ya nchi.
 
Hujui Majukumu ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge? Looh!, unatisha kama njaaa.
 
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...

Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.


Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....

Aaa!! Ama kweli Nyani halioni Kundule ,si ilikuwa ni wewe mwanakijiji na wafuasi wako wakati ule CUF wakihilikishwa na kuzushiwa kila aina ya uovu na jeshi la polisi na serekali kama linavyowafanyia Chadema hivi sasa ijapokuwa hawajafikia hatuwa waliyokuwa wakiwafanyia CuF wengi wenu hapa mliwapamba kwa kila aina ya sifa jeshi la polisi na kuwatusi wana Cuf na wazanzibar , leo ndio mmehisi ya machungu imekupandeni ?kwa tarifa yako huo ndio mwanzo Mass murder 2015 tutakuja kumbusha.

 
Back
Top Bottom