Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Hata mara moja kamati hii haijawahi kusimama kuhesabiwa wananchi wa Tanzania wanapoonewa, kudhalilishwa na hata kuuawa na vyombo vya ulinzi. Vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu na zile za kiraia unaofanywa na baadhi ya maafisa wa vyombo vya ulinzi inaonekana haufanyi Kamati hii kuamka na kujaribu kufuatilia. Vitendo vya polisi kukandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo kila wakipata nafasi na hata tuhuma zilizotolewa na viongozi wa chama hicho kuwa vyombo vya usalama vinawafuatilia viongozi wa chama hicho ili kuwatendea inaonekana taarifa zake hazifiki kwenye kamati hii ya kudumu ya Bunge...
Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.
Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....
Wananchi wetu wanauawa, wanaonewa na haki zao zinaminywa na kusiginwa na wenye nguvu za dola lakini chombo cha Bunge chenye uwezo wa kusimamia na kuhoji haya na hata kupewa majibu kimeamua kuwa kimya. Njama ya Ukimya.
Isipokuwa mgogoro wa Malawi.....