Ukimwi Wapungua Tanzania

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040




3664166.jpg

Idadi ya watu wanaoambukizwa virusi vya ukimwi nchini Tanzania imeshuka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha mwaka 2008-2009 kwa kulinganisha na mwaka 2007-2008. Wednesday, December 02, 2009 4:49 AM
Idadi ya watu wanaoambukizwa virusi vya ukimwi nchini Tanzania imeshuka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha mwaka 2008-2009 kulinganisha na kipindi cha mwaka 2007-2008. Kigoma ndio mkoa wenye wagonjwa wachache sana wa ukimwi kuliko mikoa mingine. Imeelezwa kuwa idadi ya watu wanaoambukizwa virusi vya ukimwi nchini Tanzania imeshuka kwa kiwango kikubwa katika kipindi cha mwaka 2008-2009 kwa kulinganisha na mwaka 2007-2008.

Hayo yamebainishwa katika hotuba mbalimbali katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani ambayo nchini Tanzania yalifanyika kitaifa katika mkoa wa Tanga.

Katika taarifa za kitaifa, kiwango cha ukimwi kinatajwa kushuka kutoka asilimia 7.2 mwaka 2008 hadi kufikia asilimia 5.5 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa za kitaifa mkoa wa kigoma ndio unaotajwa kuwa na maambukizi madogo kuliko mikoa mingine nchini Tanzania na kwamba ni asilimia 2.2 ya maambukizi ukilinganishana mikoa ya Iringa, Dar es salaam na Mbeya inayotajwa kuwa na kiwango cha juu cha kati ya asilimia 7 na 12.

Aidha takwimu za mkoa wa Kigoma zinaonesha kuwa wilaya ya Kasulu ambayo ina idadi ya watu wapatao laki saba pamoja na wakimbizi wa DRC na Burundi, ndiyo yenye maambukizi ya chini.

Kwa mujibu wa hotuba ya mkuu wa wilaya ya Kasulu Bi. Zainab Kwikwega aliyoitoa jana katika kijiji cha Kanazi katika maadhimisho ya kiwilaya amebainisha kuwa katika kipindi cha mwaka 2008, jumla ya wananchi 30,352 wakiwemo wanaume 11,111 na wanawake 19,241 walijitokeza kwa hiari kupimwa Afya zao ambapo Kati ya yao wananchi 413, wakiwemo wanaume 162 na wanawake 251 waligundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi sawa na asilimia 1.3 ya wote waliopimwa.

Akichambua juu ya sababu za kuwepo kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi, mkuu wa wilaya ya Kasulu Zainab Kwikwega amebainisha kuwa, tabia ya vijana kufanya ngono zisizo salama kabla na baada ya kuoa au kuoelewa ni moja ya vyanzo vikubwa vya kuendelea kuwepo kwa UKIMWI hapa nchini.

Amebainisha kuwa, juhudi zaidi za kutoa elimu zinaendelea kufanyika ili hatimaye kiwango cha maambukizi kiweze kushuka zaidi au kutokomea kabisa na kwamba kila Mtanzania anawajibika kujilinda ili asiambukizwe na aliyeambukizwa asiwaambukize wengine.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=3664166&&Cat=1
 
Wasichosema katika article hii ni kwamba hizi asilimia ni za wale wachache wanaoamua kupimwa au wajawazito wanaopimwa kwa lazima au vyote.

In any case watu wengi hawapimwi kwa kuhofia kukutwa positive, whatever the percentage given, to get an approximation of the true picture one must add at least half of it, kwa hiyo kama official figures za ukimwi Dar ni 12%, the real figure is between 16% and 20%.

That **could** be as high as one person in five.
 
Hizi ni takwimu za kisiasa tu! Nadhani kasi ya ukimwi bado inaendelea kukua kwani kila siku watu wanapata maambukizi, haswa sehemu za starehe.
Asilimia hizi zilizoandikwa hapa nadhani ni zawale wagonjwa mahutihuti waliolazwa hosptakini au wanawake wajawazito wanaliopimwa wakati wanahudhuria kliniki!
 
Hizo ni takwimu za kukadilia tu ili nao waonekane wanafanya kazi, siasa tupu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom