UKIMWI umeniacha 2008

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
MSICHANA Blandina alisikika akiwalaumu majirani zake kijijini huku akilia machozi, akisema, "Jamani mngeniambia mapema nisingekuwa hivi sasa. Lakini mkaniacha tu jamani mimi nawalaumu nyie kwa kuwa sasa nitakufa niwaache watoto wangu."

"Hivi Benson siku hizi yuko wapi; ni mzima? anazidi kuulizia kwa hofu. Blandina alijuta namna alivyomsaliti mume wake Benson.

Alimsaliti kwa kuwa Benson na Dickson, walikuwa marafiki walioishi katika nyumba moja yenye vyumba tofauti. Dickson akiwa hana mke, alikuja pale kijijini kwa Benson kwa lengo la kujihusisha na shughuli za uchimbaji mdogo wa madini.
Ilikuwa bahati kwake kila alipojaribu uchimbaji, alipata pesa nyingi. Hali hiyoilimfanya aonekane wa kipato cha juu kuliko hata wenyeji na muhimu zaidi, kuliko rafiki yake Benson.

Benson alipopata nafasi ya masomo jijini Nairobi kwa kipindi cha miezi mitatu, uaminifu ulishindikana baina ya Dickson na Blandina; wakaiona hiyo ni nafasi tosha ya kumsaliti vilivyo Benson.

Lakini, wachache waliojaribu kumzuia Blandina kwa njia ya utani kuwa anachokifanya si chema kwake, kwa mume wake, kwa jamii na hata kwa Mungu yeye mwenyewe alisema kwa kujiamini.

"Huyu (Benson) si tumekaa naye tu kwani tumeoana kabisa." Ndipo mshangao ulizidi kuwavamia watu hata wasiamini kuwa kweli ni Blandina ndiye anayesema hayo. Kila mwenye mapenzi mema, anayejua thamani ya ndoa na uhai, alifumba kimya na kuinamisha kichwa kwa mshangao. Alivamiwa na butwaa la aina yake. Wengine wakasema

UPANDACHO, NDICHO UVUNACHO
Wanaojua, walijua kuwa Blandina na mwenzake walikuwa tayari wamekufa kidhamira na sasa wanasubiri kifo cha UKIMWI.

Walisema hivyo maana walijua kwa tabia hiyo, UKIMWI hautakuwa tayari kumsamehe Blandina, hawakuongopa.
Labda mtu anaweza kujiuliza kuwa dhamiri ni nini? Dhamiri ni sauti ya Mungu iliyo katika roho ya kila mwanadamu inayomsaidia kujua jema na baya. Mtu anapokufa kidhamiri, matendo yake hayatofautiani na ya mnyama na wakati mwingine kuliko mnyama kamili.

Hata katika mazingira ya sasa, uovu wa aina yoyote unaofanyika duniani, ni matokeo ya kufa kidhamira.

Uovu mwingine ni chanzo cha kuenea kwa ugonjwa hatari wa UKIMWI. Hakuna asiyejua kuwa UKIMWI sasa limekuwa ni tatizo ambalo limeikumba jamii na kuwa sugu kutokana na ugumu wa mioyo ya watu unaosababishwa na watu kufa kidhamira.

Sote tunaitambua njia kuu ya kuenea kwa UKIMWI kuwa ni kushiriki vitendo vya uzinzi na uasherati, lakini kutokana na ugumu wa mioyo na dhamira zetu, tunapoonywa ili tusishiriki vitendo hivyo, hatusikii.

Katika mahubiri ya Jumapili ya Pili ya Pasaka Mwaka uliopita, Frateri Evarist S. Tarimo, alisema parokiani Changombe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam kuwa, "Kinachotufanya tuwe wagumu wa mioyo ni kwa sababu ile sauti ya Mungu inayotufanya tumwogope Mungu haipo tena katika mioyo yetu."

Mtu aliyekufa kidhamiri utamsikia akijitahidi kupotosha maana na kutoa kirefu cha neno AIDS kuwa ni "Acha Iniue Dogodogo Siachi" au hata akijigamba kuwa, UKIMWI ni ugonjwa kama mafua tu... "Majibu hayo yanaonesha jinsi watu walivyokufa kidhamiri. Wazo la kumuogopa Mungu tena halipo," alisema.

Mawazo hayo yamepitwa na wakati na ni upotoshaji na uuaji unaofanywa na "maiti wa dhamiri" kwa makusudi. Ni wakati muafaka kuyakana.

Madaktari, viongozi wa serikali na asasi za kibinafsi, hawajatambua kuwa hawatafanikiwa katika vita dhidi ya UKIMWI kwa kuwa silaha" wanazotumia ni mbovu na zinapingana na mapenzi ya Mungu.

"Njia ya kutumia kondomu au kuwa na mpenzi mmoja hazisaidii kabisa kutokomeza UKIMWI bali zinaongeza UKIMWI na kuchochea ufuska katika jamii.

Hata viongozi wanasahau kitu cha msingi ambacho kitasaidia kabisa kuutokomeza UKIMWI; yaani MUNGU." alisema.
Ni dhahiri kuwa kwa kuwa watu hao na wengine wamemweka Mungu pembeni, jamii haitafanikiwa katika vita hiyo. Hali hiyo inatazamwa kuwa ni sawa na kutatua tazizo kuanzia kwenye majani badala ya kuanzia kwenye mizizi yaani, shinani.
Kila mmoja lazima ajue kuwa UKIMWI utaisha endapo tu, jamii itamuogopa Mungu na kuacha uzinzi.

Frateri Tarimo katika mahubiri hayo alisema kuwa, kutokana na wazazi kuishi maisha ya ovyo ovyo, watoto nao wanawaiga wazazi wao katika kuishi maisha ya ovyovyo. Watoto wamekosa mwelekeo katika maisha na kuamua kufuata hata mitindo ovyo ovyo ya maisha toka kwa wazazi wao.

Hapa ni dhahiri kila mmoja anapaswa kujua kuwa kama baba ana tabia ya kuwa na nyumba ndogo, ni vigumu kumfundisha mtoto wake kuacha uasherati.

Kadhalika, kama mama ana tabia ya kuwa na "buzi la kuchuna", ni vigumu kumfundisha mtoto namna ya kuepukana na uasherati.

Kama kweli tunataka kushinda vita dhidi ya UKIMWI, ni lazima kila mmoja kwa nafasi yak aanze kujijengea dhamiri. Wazazi tukiwa na dhamii nzuri, tutaweza kuwajengea watoto wetu dhamiri nzuri maana hata Waswahili wanasema, "Mtoto anapobebwa hutazama kisogo cha mamaye." Na hata Yesu anasema kuwa, "Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya na wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri. Mt. 7: 15-20.

Kama wazazi hatutaanza kubadili tabia, tutaangamia pamoja na watoto wetu. UKIMWI utatumaliza wote. Hali yetu sasa ni mbaya mno.

Watoto na hata wanafunzi wengi katika miji mbalimbali tayari wana UKIMWI. Hawa wanasubiri kifo tu; waende; wafe.
Watoto hawa wamepata UKIMWI kwa kuwa wazazi, walezi wao na jamii nzima, hawakutimiza wajibu wao ipasavyo.

Walishindwa kuwajengea dhamiri ili wamwogope Mungu na kuitunza miili yao ambayo ni Hekalu la Roho Mtakatifu.

Inasikitisha kwani baadhi ya watoto na wanafunzi wameathirika kwa kuwa baadhi ya wazazi na walezi walifanya nao mapenzi na hali hii mara nyingi imekuwa ikidhihirika wazi.

Wazazi hao bila aibu wamediriki kuwadanganyia watoto hawa chips, kuwapa fedha na kuwapa lifti katika magari yao, aibu na dhambi iliyoje.

Ni dhahiri hali hii inabainisha namna jamii ilivyokufa kidhamiri. Baba mzima au mama mzima na heshima zako, unapata wapi ujasiri wa kufanya mapenzi na mtoto wako hata umwambukize UKIMWI?

"Ama kweli sasa tunaishi kama wanyama. Akina baba na akina mama kama hawa, hawamwogopi Mungu kabisa. Hii ni kwa sababu dhamira zao zimekufa.

Kwanza hawana habari na kuvunja Amri ya Sita ya Mungu inayokataza kuzini, hawaoni aibu kufanya mapenzi na watoto, hawaogopi kuwaua watoto hawa na hata wenyewe kujiua na pia, hawaogopi kuziacha familia zao zikiteseka mara baada ya kufa kwa UKIMWI na zaidi, hawaogopi kuwaua wake au waume zao.," alisema.

Kila mtu anapaswa kujua kuwa akizini akapata UKIMWI, atakuwa na hatia nyingi mbele za Mungu: Atakuwa na adhabu ya kuzini, atakuwa na hatia ya kujiua mwenyewe kama aliyejiua wa kisu, kujinyonga kwa kamba au kujiua kwa sumu.
Kama mtu huyu ameoa, atakuwa na hatia ya kumuua mke wake na kama akifanya mapenzi nje ya ndoa atakuwa na hatia ya kuwaua watu wengine.

Zaidi na zaidi, mtu huyu kama ameolewa au ameoa, atakuwa na hatia ya kuiacha familai yake katika kipindi cha mateso.
Pamoja na njia nyingine zinazohimizwa na wataalamu wa afya, njia sahihi za kuepukana na UKIMWI ni kuepuka kabisa uzinzi na uasherati. Jibu la kuutokomeza kabisa UKIMWI liko kwa Mungu. Wote hatuna budi kufungua mioyo yetu na kumsikiliza Mungu anatuambia nini.

Njia nyingine ni kusali, kusoma Maandiko Matakatifu (Biblia) na kuwaomba watakatifu waliotunza usafi wa moyo wakati wa maisha yao hapa duniani.

Njia nyingine ya kupambana na UKIMWI ni kwa wanandoa kukumbuka maagano waliyoyafanya siku ya ndoa. Kwamba kila mmoja atakuwa mwaminifu daima kwa mwenzie.

Kila mnapolala na kuamka, sala ya kila mmoja iwe "Nitakuwa mwaminifu kwako daima." Kila mara baba aogope kumuua mama na mama aogope kumuua baba. Baba na mama wakiogopa kuuana, watakuwa wamesadia sana kupambana na UKIMWI. Kadhalika wazazi hao wote waogope kufa kwa UKIMWI na kuacha watoto, familia na jamii zao zikiteseka.

Ni wajibu wa kila mmoja kujua kuwa vita dhidi ya UKIMWI haitengani na namna sahihi ya kuishi na kuwahudumia wale ambao tayari walishaathirika.

Jamii haipaswi kuwaona walioathirika na UKIMWI kuwa wao ni wadhambi kuliko watu wengine la hasha! Hiyo si kweli.
Lazima kila mmoja ajue kuwa inawezekana anapomcheka, kumbeza na kumdharau mgonjwa wa UKIMWI, huenda hata yeye alishaambukizwa kwa njia yoyote isipokuwa tu, hajui kwa sababu hajapimwa.

Inakera kwani wengi wetu katika jamii wana tabia ya kuwaona kuwa ni wadhambi; watu ambao wamekwishaambukizwa UKIMWI. Hii si kweli na ni dhana mbaya kwa kuwa zipo dhambi nyingi na sio kuzini pekee.

Kuiba, kupokea rushwa, masengenyo, chuki dhidi ya wenzio, kusema uongo, kuua, na mengine mengi, yote hayo ni dhambi Kumbe sote tu wadhambi.

Tunachopaswa kufanya ni kuwapenda na kuwahudumia vizuri wagonjwa wa UKIMWI sio kuwakimbia, kuwachukia, kuwasimanga, kuwadhulumu wala kuwacheka

Ni wakati sasa kuanza mwaka huu kila mmoja akijisemea kuwa: "Kama sikuambukizwa UKIMWI mwaka uliopita, basi sitaambukizwa."

Ni wakati sasa kujiuliza kwanini kitendo cha zinaa ambacho ni cha dakika chache kinipe mateso na kunipeleka katika moto wa milele?
 
"Kinachotufanya tuwe wagumu wa mioyo ni kwa sababu ile sauti ya Mungu inayotufanya tumwogope Mungu haipo tena katika mioyo yetu."

...Nice article plus several useful Wuotes, nimeipenda zaidi hiyo na ile ya mtoto abebwapo humuangalia mama kisogoni...:)
thx Shy
 
Jamaa amekufa lakini ataishi milele! Ukifa Leo wewe utatuachia nini??
 
Kuna mdau hapa JF nadhani 2016 alitoa taarifa ya kifo chake baada ya kunywa sumu gest huko mbeya town,kisa wife wake analiwa
Yeah niliuona ule uzi japo sababu ya kifo nilishindwa kuing'amua.
Kama hiyo ndo sababu inasikitisha sana!
 
Back
Top Bottom