Ndugu wana jamvi, hii tabia imekuwa ikinikera hata sijui cha kufanya "is kind off" niko kwenye "dilemma". Nina rafiki yangu mpenzi ambaye hivi siku za karibuni nimegundua kuwa wife wake anacheat na sehemu anayofanyia huo mchezo naifahamu. Rohoni najiuliza kumwambia mme wake ndoa yao inaweza vunjika, na itakuwa mm ndiye niliyesababisha kuvunjika kwa kutoa siri hiyo. Lakini naumia sana rohoni maana, utakuta rafiki yangu anakwama kufanya shughuli zake zingine akidhani wife wake yuko kazini na gari kumbe amebana sehemu na jamaa yake. Wakati mwingine ananiomba niende kumpeleka sehemu anayotaka kwenda. of course kwa kuwa ni rafiki yangu naenda huku rohoni naumia nikiwaza kama hivi ingekuwa mm rafiki yangu ananiambia wife wako anacheat sehemu furani ninge react namna gani. Kinachosikitisha huyo mama kila wakati ananilalamikia jinsi mume wake anavyocheat. Najiuliza hivi huwa haoni aibu kulalamika na yeye ndiyo mchezo wake? Naomba ushauri wenu nimwambie????
Je best yako nae katulia (au anecheat vilevile)? Kama nae anecheat kama alivyokulalamikia mke basi piga kimya mazee.