Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Mmoja wa rafiki zangu aliwahi kuniambia kuwa hata siku moja wanaume na wanawake hawawezi kuwa sawa 50%-50% katika nyanja ya kisiasa! Kwamba siku zote wanaume watakuwa juu ya wanawake! Nilipouliza kwa nini aliniambia kuwa sababu kuu ni moja kwamba WANAWAKE WENYEWE KWA WENYEWE HAWAPENDANI yaani wanahofia kama wakimuunga mkono mwenzao na akafanikiwa atawasumbua kwa sababu wanahisi kama ni kuringa kutaogezeka, kama ni mwendo utabadilika na kama ni dharau kwa wanawake wenzake ndo zitaongezeka mara 100! Na hii ndo sababu wanawake wengi wanawaunga mkono wanaume ktk nyanja za siasa!
Kwa karibu hali hii naona kama vile inatunyemelea sisi vijana! Kwa sababu zisizowazi na naogopa kusita kuziita za kinafiki vijana wengi walimchukia Zitto na kumuita majina mbalimbali na tofauti (haswa haswa walimuona kama kibaraka wa CCM ndani ya CHADEMA!) ukiuliza sababu unaambiwa eti ni kwa nini alikubali kuteuliwa na raisi kwny ile tume ya kuchunguza sekta ya madini, mara utaambiwa eti kuwa alitaka kugombea uenyekiti ili amuondoe Mbowe, mara anapendwa na wabunge wa CCM n.k lakin sababu zoteee hazina hata msingi wa kumuita mtu kibaraka!
January Makamba, huyu naye ni mbunge kijana mwenye uwezo mzuri sana bungeni lakini siku hizi anaitwa eti "mnafiki" kisa eti hakusaini ili kuuunga mkono hoja ya Zitto ya kumuondoa waziri mkuu. Binafsi mwanzoni nlimshangaa Makamba na nakumbuka niliingia twitter na kumuomba asaini! Nakumbuka alijibu kuwa yeye (Makamba) akitaka mtu/kiongozi ajiudhuru atamfuata ana kwa ana na kumwambia wewe hufai na jiudhuru .....
Na kwamba yeye na Zitto wana nia moja (same objective) ila wanatofautiana njia za kufikia hiyo nia! Nilipofuatilia yaliyojiri kwny kikao cha wabunge wa CCM ni kweli Makamba alifanya kama alivyonambia kwenye twitter! Sasa unafiki upo wapi?
My Take: vijana wenzangu hebu tujitahid kujivunia na kuwaunga mkono hawa viongozi ambao ni vijana wenzetu (sio Zitto na Makamba tu bali viongozi vijana wote) na tujifunze kuwahukumu baada ya kuwasikiliza (kama tulivyomuhukumu yule mbunge wa Nzega (Dr Kigwangala) sina uhakika na usahihi wa kuandka jina) na sio kwa kusikiliza maneno ya wengine!
Kwa karibu hali hii naona kama vile inatunyemelea sisi vijana! Kwa sababu zisizowazi na naogopa kusita kuziita za kinafiki vijana wengi walimchukia Zitto na kumuita majina mbalimbali na tofauti (haswa haswa walimuona kama kibaraka wa CCM ndani ya CHADEMA!) ukiuliza sababu unaambiwa eti ni kwa nini alikubali kuteuliwa na raisi kwny ile tume ya kuchunguza sekta ya madini, mara utaambiwa eti kuwa alitaka kugombea uenyekiti ili amuondoe Mbowe, mara anapendwa na wabunge wa CCM n.k lakin sababu zoteee hazina hata msingi wa kumuita mtu kibaraka!
January Makamba, huyu naye ni mbunge kijana mwenye uwezo mzuri sana bungeni lakini siku hizi anaitwa eti "mnafiki" kisa eti hakusaini ili kuuunga mkono hoja ya Zitto ya kumuondoa waziri mkuu. Binafsi mwanzoni nlimshangaa Makamba na nakumbuka niliingia twitter na kumuomba asaini! Nakumbuka alijibu kuwa yeye (Makamba) akitaka mtu/kiongozi ajiudhuru atamfuata ana kwa ana na kumwambia wewe hufai na jiudhuru .....
Na kwamba yeye na Zitto wana nia moja (same objective) ila wanatofautiana njia za kufikia hiyo nia! Nilipofuatilia yaliyojiri kwny kikao cha wabunge wa CCM ni kweli Makamba alifanya kama alivyonambia kwenye twitter! Sasa unafiki upo wapi?
My Take: vijana wenzangu hebu tujitahid kujivunia na kuwaunga mkono hawa viongozi ambao ni vijana wenzetu (sio Zitto na Makamba tu bali viongozi vijana wote) na tujifunze kuwahukumu baada ya kuwasikiliza (kama tulivyomuhukumu yule mbunge wa Nzega (Dr Kigwangala) sina uhakika na usahihi wa kuandka jina) na sio kwa kusikiliza maneno ya wengine!