Ukibaraka wa Zitto wa jana na unafiki wa Makamba wa leo!

Dijovisonjn

JF-Expert Member
Nov 14, 2011
466
125
Mmoja wa rafiki zangu aliwahi kuniambia kuwa hata siku moja wanaume na wanawake hawawezi kuwa sawa 50%-50% katika nyanja ya kisiasa! Kwamba siku zote wanaume watakuwa juu ya wanawake! Nilipouliza kwa nini aliniambia kuwa sababu kuu ni moja kwamba WANAWAKE WENYEWE KWA WENYEWE HAWAPENDANI yaani wanahofia kama wakimuunga mkono mwenzao na akafanikiwa atawasumbua kwa sababu wanahisi kama ni kuringa kutaogezeka, kama ni mwendo utabadilika na kama ni dharau kwa wanawake wenzake ndo zitaongezeka mara 100! Na hii ndo sababu wanawake wengi wanawaunga mkono wanaume ktk nyanja za siasa!

Kwa karibu hali hii naona kama vile inatunyemelea sisi vijana! Kwa sababu zisizowazi na naogopa kusita kuziita za kinafiki vijana wengi walimchukia Zitto na kumuita majina mbalimbali na tofauti (haswa haswa walimuona kama kibaraka wa CCM ndani ya CHADEMA!) ukiuliza sababu unaambiwa eti ni kwa nini alikubali kuteuliwa na raisi kwny ile tume ya kuchunguza sekta ya madini, mara utaambiwa eti kuwa alitaka kugombea uenyekiti ili amuondoe Mbowe, mara anapendwa na wabunge wa CCM n.k lakin sababu zoteee hazina hata msingi wa kumuita mtu kibaraka!

January Makamba, huyu naye ni mbunge kijana mwenye uwezo mzuri sana bungeni lakini siku hizi anaitwa eti "mnafiki" kisa eti hakusaini ili kuuunga mkono hoja ya Zitto ya kumuondoa waziri mkuu. Binafsi mwanzoni nlimshangaa Makamba na nakumbuka niliingia twitter na kumuomba asaini! Nakumbuka alijibu kuwa yeye (Makamba) akitaka mtu/kiongozi ajiudhuru atamfuata ana kwa ana na kumwambia wewe hufai na jiudhuru .....
Na kwamba yeye na Zitto wana nia moja (same objective) ila wanatofautiana njia za kufikia hiyo nia! Nilipofuatilia yaliyojiri kwny kikao cha wabunge wa CCM ni kweli Makamba alifanya kama alivyonambia kwenye twitter! Sasa unafiki upo wapi?

My Take: vijana wenzangu hebu tujitahid kujivunia na kuwaunga mkono hawa viongozi ambao ni vijana wenzetu (sio Zitto na Makamba tu bali viongozi vijana wote) na tujifunze kuwahukumu baada ya kuwasikiliza (kama tulivyomuhukumu yule mbunge wa Nzega (Dr Kigwangala) sina uhakika na usahihi wa kuandka jina) na sio kwa kusikiliza maneno ya wengine!
 
Ni nani alokuambia zito anashutumiwa kwa hayo mambo uluyoyaolozesha?
 
Huyu mleta thread anahitaji huruma za Mungu wa israel kwani anaandika uzembe humu.
 
wengi hupenda kufanya siasa za mihemko na matukio bila kupima mambo kwa upana wake. cjaona undumiakuwiliwa zito katika hoja zake hadi leo hii!
 
Hamna cha maana hapo. Labda cha maana kwa Zito (25) ni maamuzi ya kamati ya rufaa yanasema mechi ya Azam na Mtibwa itarudiwa.
 
Like am just passing:

1. Wewe una fikra mgando. Kwa sababu unataka litokee jambo watu walipokee kama unavyotaka wewe. Haiko Hivyo. We have Mathematical Analysis for science and engineering issues. This is the same fo Politics. Watu wanapofanya analysis na kama wewe kidogo si mwelewa wa mambo, kwa maana ya kuyachukulia yalivyo chukua time kujiuliza kwa nini watu wameenda mbele zaidi.

2. Zitto ni 'mnafiki' ni 'kibaraka', ni 'ambitious', ni 'selfish' labda ulikuw hujui hayo, Nimekuongezea. Hayo ndiyo yanajenga mafanikio aliyonayo Zitto kisiasa. Unafiki unamsaidia kuji-position popote, CDM ama CCM. Uki-baraka unamsaidia kutimiza malengo yake binafsi. Zitto namfahamu alipoanzisha motion ya Kumwondoa raisi wa DARUSO pale UDSM kipindi hicho akiwa mwanafunzi pale. Ni kusema Zitto hajaanza leo unafiki na ukibaraka kwa maana ya ubinafsi kutokana na malengo yake ya kuwa juu.

3. Wewe unajua Makamba alimwambia nani personally JIUZULU? Na ninani amekuambia Makamba ni bora kuliko Edward Lowassa? Wana tofauti gani (kama wengine wanavyoamnini EL ni fisadi). January kijana aliyefanya kazi IKULU karibu sana na JK unaniambia leo ni MwanaMapiduzi? Hata kwa USALAMA WA TAIFA KOKO tulio nao hangekuwapo. Ni mnafiki sijawazaga kama Makamba ana jipya. What I like about January Makamba ni a morden guys, using morden 'colonial strategies) hujifanya kuwa karibu na wewe kumbe anakumaliza. Makamba is a 'Black Muzungu' bwana. Personally I never trusted the guy even compared to Zitto.

4. Nasema hawa ni vijana, wanaviziana kiMASLAHI. Hawana jipya la kitendea Tanzania na WaTanzania. There are Potential people wako, wako ila not these guyz
 
Ndg mtoa hoja kuna kitu kimoja umesahau kwamba hii JF ni yana Chadema tu. ukionge ukweli wao kazi yao ni kung'aka. nasikitika JF sikuhizi imepotez mvuto maana imekaa ki Chadema zaidi na sio ki Taifa.

Ombi: wekeni wazi tu kuwa hoja za hapa ni kwaajili ya kusifia CDM na viongozi wao na sio kwa maslahi mapana ya taifa la Tanzania.
 
Like am just passing:

1. Wewe una fikra mgando. Kwa sababu unataka litokee jambo watu walipokee kama unavyotaka wewe. Haiko Hivyo. We have Mathematical Analysis for science and engineering issues. This is the same fo Politics. Watu wanapofanya analysis na kama wewe kidogo si mwelewa wa mambo, kwa maana ya kuyachukulia yalivyo chukua time kujiuliza kwa nini watu wameenda mbele zaidi.

2. Zitto ni 'mnafiki' ni 'kibaraka', ni 'ambitious', ni 'selfish' labda ulikuw hujui hayo, Nimekuongezea. Hayo ndiyo yanajenga mafanikio aliyonayo Zitto kisiasa. Unafiki unamsaidia kuji-position popote, CDM ama CCM. Uki-baraka unamsaidia kutimiza malengo yake binafsi. Zitto namfahamu alipoanzisha motion ya Kumwondoa raisi wa DARUSO pale UDSM kipindi hicho akiwa mwanafunzi pale. Ni kusema Zitto hajaanza leo unafiki na ukibaraka kwa maana ya ubinafsi kutokana na malengo yake ya kuwa juu.

3. Wewe unajua Makamba alimwambia nani personally JIUZULU? Na ninani amekuambia Makamba ni bora kuliko Edward Lowassa? Wana tofauti gani (kama wengine wanavyoamnini EL ni fisadi). January kijana aliyefanya kazi IKULU karibu sana na JK unaniambia leo ni MwanaMapiduzi? Hata kwa USALAMA WA TAIFA KOKO tulio nao hangekuwapo. Ni mnafiki sijawazaga kama Makamba ana jipya. What I like about January Makamba ni a morden guys, using morden 'colonial strategies) hujifanya kuwa karibu na wewe kumbe anakumaliza. Makamba is a 'Black Muzungu' bwana. Personally I never trusted the guy even compared to Zitto.

4. Nasema hawa ni vijana, wanaviziana kiMASLAHI. Hawana jipya la kitendea Tanzania na WaTanzania. There are Potential people wako, wako ila not these guyz

Zitto ni noumaaaaaaaa! Kama umesoma nae onesha mchango wako kwa Taifa unaomzid Zitto,wameshindwa watu wenye nguvu zao kumchafua Zitto itakuwa ww mlemavu wa akili!
 
Hivi mkuu mleta mada unasumbuliwa na nini hasa?mbona ndugu zako Jf hautaki kutuweka wazi tukusaidie?
 
Back
Top Bottom