kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
UPUNGUFU wa mishahara na maslahi madogo kwa walimu, vimeelezwa kuwa ndio chanzo cha walimu hao kujihusisha na kilimo katika maeneo yao ya kazi na kuitelekeza taaluma yao.
Hayo yalisemwa juzi na Katibu wa Chama cha Walimu (CWT), Mkoa wa Shinyaga, Martini Samara, wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho katika ngazi ya Wilaya ya Bukombe.
Samara alisema maslahi madogo wanayopata walimu yamechangia kushuka kwa elimu kila mwaka hali ambayo inahatarisha nchi kukosa wasomi.
Alisema kwa sasa baadhi ya walimu wamekuwa wakijihusisha na kilimo katika maeneo yao ya kazi, badala ya kufundisha na kusababisha wanafunzi wengi kufeli katika mitihani yao ya mwisho.
Kama unamlipa mwalimu mshahara mdogo, unafikiri anaweza kufundisha darasani? Hata ukimsimamia, ukiwa na Ofisa Elimu na Mkurugenzi, anaweza kufundisha masomo ambayo yamekwishapita, alisema Katibu huyo.
Alisema mwalimu akigoma, askari hawezi kufanya kazi ya kufundisha darasani tofauti na madaktari ambao wanaweza kugoma, na wakachukuliwa wengine kwenda kufanya kazi hiyo.
Alidai kuwa walimu wamekuwa wakidharaulika hadi kinapofikia kipindi cha uchaguzi ndipo Serikali inapowakumbuka na kuwalipa malimbikizo ya madai yao ya nyuma.
Hayo yalisemwa juzi na Katibu wa Chama cha Walimu (CWT), Mkoa wa Shinyaga, Martini Samara, wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho katika ngazi ya Wilaya ya Bukombe.
Samara alisema maslahi madogo wanayopata walimu yamechangia kushuka kwa elimu kila mwaka hali ambayo inahatarisha nchi kukosa wasomi.
Alisema kwa sasa baadhi ya walimu wamekuwa wakijihusisha na kilimo katika maeneo yao ya kazi, badala ya kufundisha na kusababisha wanafunzi wengi kufeli katika mitihani yao ya mwisho.
Kama unamlipa mwalimu mshahara mdogo, unafikiri anaweza kufundisha darasani? Hata ukimsimamia, ukiwa na Ofisa Elimu na Mkurugenzi, anaweza kufundisha masomo ambayo yamekwishapita, alisema Katibu huyo.
Alisema mwalimu akigoma, askari hawezi kufanya kazi ya kufundisha darasani tofauti na madaktari ambao wanaweza kugoma, na wakachukuliwa wengine kwenda kufanya kazi hiyo.
Alidai kuwa walimu wamekuwa wakidharaulika hadi kinapofikia kipindi cha uchaguzi ndipo Serikali inapowakumbuka na kuwalipa malimbikizo ya madai yao ya nyuma.