EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,091
Katika siku za hivi karibuni dhana ya ukabila/udini na umimi imekuwa inachukua nafasi kubwa sana hasa baada ya msuguano wa kisiasa kuonekana unakuwa mkubwa hapa nchini. Nakumbuka katika hotuba kadhaa za baba wa taifa alikuwa akijaribu kukemea hili kwa nguvu sana hasa suala hili la udini na ukabila.
Ukabila
Katika hili ntatoa mifano michache ambayo inazungumzwa sana kwa kipindi hiki ili kuonyesha dhana ya ukabila inavyochukua nafasi katika siku za hivi karibuni. Nakumbuka katika uchaguzi wa mwaka 1995 kulizuka dhana ya ukabila ambayo ilienezwa ikikihusisha zaidi chama cha NCCR Mageuzi wakati huo kikiwa chini ya Mh. Lyatonga kuwa ni chama cha "wachaga" baadae dhana hiyo ikafutika hasa baada ya uchaguzi ule kumalizika lakini sasa imeibuka tena na kipindi hiki ikihusisha zaidi chama cha Chadema ambapo awali ilikuwa ikiita chama cha "wachaga" lakini sasa imepanuka zaidi na kukiita chama cha "Kaskazini" kinachonitia hofu kidogo hapa ni namna dhana hii inavyokuwa kwa kasi na wakati mwingine napata woga kidogo kuwa "watanzania tumeshafika hapo"
Hivi tunapochagua kiongozi ni nini tunakuwa tunaangalia kutoka kwake? Je ni kabila lake, wapi anatoka au ni uwezo wake wa kufanya kazi? Inanisikitisha kidogo kwasababu ni dhana ambayo sasa inawaingia mpaka wasomi wakubwa ambao mi nilitegemea wangekuwa nguzo ya umoja na mshikamano wetu kama nchi.
Udini
Hivi majuzi baada ya tume ya katiba kutangazwa na kuapishwa niliendelea kusikia minong'ono kuwa "mbona waislam ni wengi kuliko wakristo" Dah hii nayo ikanifanya nitetemeke maana niliona sasa huku tunakokwenda siko na tena kigezo walichokuwa wanakitumia wenye hoja hiyo ni majina nikawa najiuliza hivi kwa mfano jina la "Jaji Augustino Ramadhani" unamuita mkristo au Muislam?
Mi mtazamo wangu ni kwamba nafikiri bado tuna uwezo wa kurekebisha hili hasa kwa wanasiasa maana ukiangalia kwa kiwango kikubwa dhana hii inachangiwa na wanasiasa ambao wako tayari kufanya lolote ili kuwa bora wenzao huku wakiteketeza umoja na mshikamano tulionao watanzania. Mwisho nasema kwamba;
"Yule anayewasema wenzie ni wakabila na wadini, yeye ndiye mkabila na mdini maana kama asingekuwa mkabila na mdini asingeona ukabila na udini bali uwezo wa kufanya kazi wa watu"
Ukabila
Katika hili ntatoa mifano michache ambayo inazungumzwa sana kwa kipindi hiki ili kuonyesha dhana ya ukabila inavyochukua nafasi katika siku za hivi karibuni. Nakumbuka katika uchaguzi wa mwaka 1995 kulizuka dhana ya ukabila ambayo ilienezwa ikikihusisha zaidi chama cha NCCR Mageuzi wakati huo kikiwa chini ya Mh. Lyatonga kuwa ni chama cha "wachaga" baadae dhana hiyo ikafutika hasa baada ya uchaguzi ule kumalizika lakini sasa imeibuka tena na kipindi hiki ikihusisha zaidi chama cha Chadema ambapo awali ilikuwa ikiita chama cha "wachaga" lakini sasa imepanuka zaidi na kukiita chama cha "Kaskazini" kinachonitia hofu kidogo hapa ni namna dhana hii inavyokuwa kwa kasi na wakati mwingine napata woga kidogo kuwa "watanzania tumeshafika hapo"
Hivi tunapochagua kiongozi ni nini tunakuwa tunaangalia kutoka kwake? Je ni kabila lake, wapi anatoka au ni uwezo wake wa kufanya kazi? Inanisikitisha kidogo kwasababu ni dhana ambayo sasa inawaingia mpaka wasomi wakubwa ambao mi nilitegemea wangekuwa nguzo ya umoja na mshikamano wetu kama nchi.
Udini
Hivi majuzi baada ya tume ya katiba kutangazwa na kuapishwa niliendelea kusikia minong'ono kuwa "mbona waislam ni wengi kuliko wakristo" Dah hii nayo ikanifanya nitetemeke maana niliona sasa huku tunakokwenda siko na tena kigezo walichokuwa wanakitumia wenye hoja hiyo ni majina nikawa najiuliza hivi kwa mfano jina la "Jaji Augustino Ramadhani" unamuita mkristo au Muislam?
Mi mtazamo wangu ni kwamba nafikiri bado tuna uwezo wa kurekebisha hili hasa kwa wanasiasa maana ukiangalia kwa kiwango kikubwa dhana hii inachangiwa na wanasiasa ambao wako tayari kufanya lolote ili kuwa bora wenzao huku wakiteketeza umoja na mshikamano tulionao watanzania. Mwisho nasema kwamba;
"Yule anayewasema wenzie ni wakabila na wadini, yeye ndiye mkabila na mdini maana kama asingekuwa mkabila na mdini asingeona ukabila na udini bali uwezo wa kufanya kazi wa watu"