GreenCity
JF-Expert Member
- May 28, 2012
- 5,620
- 4,265
Nikiwa nafuatilia kipindi maalumu hapa IMTV, Nimeguswa sana na hisia za waombolezaji! Kwanza nimeona chama cha waandishi wa habari mko wa Iringa na Mbeya wakiwa wamevalia fulana zinazosomeka "DAUD MWANGOSI, AMEKUFA AKITETEA TAIFA" Sio siri nimeumia sana!
Wakti huohuo, mchungaji aliyeuombea mwili wa marehemu Iringa, amesema "kamwe damu ya Mwangosi haitaenda bure" pia amewataka waandishi wenza waendelee kutoa habari bila woga ili nchi ipate mabadiliko!
Katika muda wote huo, namuona mjane wa Mwangosi akiwa amekumbatia jeneza na kulipapasa kwa uchungu, da, eh mungu okoa Taifa hili!
Pia naona na kuwasikia akina mama wakilia kwa saut zilizokwama kutokana na ku whip kwa muda mrefu!
Sio siri, nimehisi mboni zangu zinaloa machozi.. .. .!
Wakti huohuo, mchungaji aliyeuombea mwili wa marehemu Iringa, amesema "kamwe damu ya Mwangosi haitaenda bure" pia amewataka waandishi wenza waendelee kutoa habari bila woga ili nchi ipate mabadiliko!
Katika muda wote huo, namuona mjane wa Mwangosi akiwa amekumbatia jeneza na kulipapasa kwa uchungu, da, eh mungu okoa Taifa hili!
Pia naona na kuwasikia akina mama wakilia kwa saut zilizokwama kutokana na ku whip kwa muda mrefu!
Sio siri, nimehisi mboni zangu zinaloa machozi.. .. .!