Ujumbe alioutuma Mh. Selasini muda mfupi kabla hajapata ajali Bomang'ombe

Huyu jamaa ni mbabaishaji. Hizi hela anazotaja ni fedha za mfuko wa maendeleo ya jimbo, sio zake wala hajafight kuzipata. Hata ungeweka mtoto mdogo ukampa hizo hela angegawa.
Tunamuombea Selasini apone then atuambie jimbo letu linapata sh ngapi za mfuko wa maendeleo ya jinbo, na yeye, kwa miaka hii miwili amezitumiaje...
Tunataka atuambie amefanya nini kuwasadia maelfu ya vijana wanaomaliza form four, na six...
Tunataka atuambie amefanya nini kusimamia ujenzi wa barabara za halmashauri ambazo sehemu nyingi hazipitiki...
Tunataka atuambie tatizo la maji kwa maeneo mengi ya Tarakea, na ugawaji maji unaopendelea matajri amelighulikia vipi...
Tunataka atuambie amefanya nini kukabiliana na tatizo kubwa la ukosefu wa walimu katika shule za sekondari Rombo...
Tunataka atuambie ni kwa nini performance za shule za Rombo kwenye mitihani ya form four inazidi kuwa mbovu, ana idea gani yeye kama mbunge na amefanya nini...
Tunataka atuambie emeshughulikia vipi suala la ugawaji wa mashamba maeneo ya forest kunakofanywa kibaguzi na kiupendeleo...
Tunataka atuambie ameshughulikia vipi suala la ukosefu wa madawa na magari ya wagonjwa katika vituo vya afya, useri na Tarakea...
Tunataka atuambie anafanya nini kusaidia tatizo la mamia ya watu walioomba umeme kwa miezi mingi sasa, wamelipa lakini hawajafungiwa, na waliofungiwa walifanikiwa baada ya kutoa rushwa nyingi sana...
Tunataka atuambie yeye kama mbunge amefanya nini kuwasaidia maelfu ya vijana wa Rombo kufaidika na mlima Kilimanjaro tofauti na sasa ambapo wanaofaidika kwa kiasi kikubwa ni wa wilaya nyingine...

Selasini kiukweli amekuwa mzigo kwa Wanarombo, na kama nilivyokwisha sema humu JF tangu mwaka jana, asipojirekebisha, asipokuwa karibu na wapiga kura wake akawasikiliza na kuwasaidia kupambana na adui umaskini, then ajue 2015 hana chake. Kama haamini akawaulize kina Mramba na Salakana...


amekuwa mzigo kwako, na sio kwa wana Rombo....
 
CHADEMA inawakati mgumu sana kujivua na dhana ya udini...ukabila naweza nikawatetea ila udini bado wanasafari ndefu....Mimi nipo nanyi lakini jitahidini...iweje mbunge anadiriki kutoa orodha ndeefu yenye misaada mingi ktk taasisi za dini ya kikristo pekee...Kumbukeni munahitajika kuwa makini muache udini ili mukubalike kwa waislamu...hii itawasaidia ktk harakati za kuingia ikulu 2015..
Mringo hivi unaweza kunikumbusha ni lini Lowasa alikuwa anaendesha harambee za kujenga misikiti? au labda mimi sielewi kwamba misaada inatolewa bila kuombwa!!....i mis some point here.

Hivi kwa mfano Mbunge wa Pemba unaweza kusikia amechangia kanisa badala ya mabati ya msikiti? kuna vitu vingine wala huitaji PHD kujuwa kwamba kuna maeneo nchi hii hakuna Uislamu na kuna maeneo nchi hii hakuna Ukristo vilevile na kuna maeneo nchi hii jamii kubwa inayopatikana hapo ni wapagani. open you're eyes.
 
Kazi bado ni kubwa hii nchi.. May he get well soon' ila ifike pahala hii nchi kaz ya mbunge isiwe kuchangia computer na printer... we have a long way to go kwa kweli'
 
Bora hata yeye, maskini anaweka vitu muhimu bya kutoa feed back. sio kama kina fulani wanaweka picha za wanawake na "experiences' zao in night clubs, as if yanatuhusu! tunamuombea kwa Mungu amponye haraka.
 


18. Kwaya ya KKT Mkuu 600,000
19. Huruma Convent 2Million (Ukarabati wa mabwawa ya kufugia Samaki)
20. Tumaini Center 2Million (Msaada kwa Watoto Yatima)
25. Parokia ya Mkuu 1Million (Mchango wa Ujenzi nyumba za mapadre)
33. Parokia ya Mahida 1Million (Ujenzi wa nyumba ya mapadri)

Mwenye macho haambiwi TAZAMA.

Hiyo ndio michango ya Mh. Selasini Mbunge wa CHADEMA.

Tunamshukuru mungu anapokea maombi yetu.
 
Selestin tunakuombea kwa Mungu upone haraka ili uendelee kupambana na changamoto zilizoko mbele yako. Rudi jiboni kwako sikiliza wananchi wako wanalilia nini angalia kwa kuweka vipaumbele na mkakati wa utekelezaji wake uwe wazi. Suala si kugawa tu fedha, peleka hoja zao mbele kwa kuzitetea sambamba na kuendelea kutoa michango midogomidogo kama ulivyoainisha.

Watu wako wanahitaji kukusikia ukijumuika nao na kuwasikiliza hoja zao na baadaye wanataka kusikia sauti yako ukiwatetea katika vyombo husika hususan bunge, waone unavyojenga hoja na kuzipambanua.

Kubishana tu kwa kurusha michango yako midogomidogo sidhani kama ndicho wanacholalamikia, peleka hoja za wanarombo mbele.
 
Ubunge ni kugawa hela?

Kwa Wabunge wa upinzani inabidi iwe hivyo, vinginevyo magamba wanayaadhibu majimbo ambayo hawakuchagua wapinzani kwa kuyatenga katika bajeti za maendeleo...Kuna Gamba moja liliwahi kutamka hadharani siku za nyuma kwamba kama mnataka maendeleo basie chagueni magamba

 
Jamani watanzania hebu tuwe waelewa na wenye mioyo ya subira, hivi mtu anamwaka mmoja na nusu tu tangu apewe ubunge kati ya miaka mitano mnamlaumu hivi? Kweli lawama hivi anastahili ama ni tamaa tu ya watu ya madaraka? Mbona mnachagua mtu badala ya kumpa ushirikiano na ushauri na maoni nyie mnategea atakosea wapi ili mpate kwa kusemea. Hivi kweli hata nyie mngepewa hiyo nafasi mngefanya kama mnavyowaza na kuona kama ni rahisi kiivyo?

Tubadilike watanzania, tuache majungu, fitina, na chuki za kijinga kwa uroho wa madaraka, tuwape ushirikiano viongizi tuliowachagua kutuongoza, tuwasaidie kwa michango ya mali na mawazo ktk kujiletea maendeleo yetu wenyewe.

Mbunge siyo Mungu kusema aweze kufanya kila kitu peke yake, hayo tunayolalamika pembeni kwa nini tusimpe kama ushauri namkumpa support? Sisi tumekuwa mafundi wa kulaumu na kukosoa bila kutoa michango yoyote. Hivi huo mfuko wa jimbo ni sh.ngapi mpaka mnataka mbunge afanye kila kitu ndani ya mwaka mmoja? Kwa serikali gani? Hii hii ya ccm? Please slow down people tuache unafiki na chuki.

Kumbuka mbunge anategemea bajeti ta serikali ili kufanikisha maendeleo jimboni, wenyewe mnajua hali ya uchumi na usimamizi wa fedha ilivyo kwa serikali yetu, unapeleka vipaombele 100 katika mwaka wa bajeti lakini unapata pesa ya vipaombele 3 unategemea nini? Nashauri tuwe tunafikiria na kijiuliza mara mbili kabla hatujatupa lawama.
 
Tumwombee kwa Mungu apone. Nyinyi mnaotaka Ubunge jipangeni lakini kwa mtaji huo mimi ninaimani Wanarombo wameona watapima wenyewe.
 
Cry my beloved country, kama hizo ndiyo kazi za mbunge na ndiyo namna mafanikio yanavyopimwa mtatawaliwa na CCM milele.
 
Mungu amponye aendelee kuwatumikia wananchi wake.
Katika hili ninaamini tupo pamoja na wenzetu, na kati yao hakuna hata moja analimezea mate jimbo lake.
 
Rombo siyo Pemba mazee kule hakuna misikiti acha mboyoyo.

Mbona hakuna msaada kwenye msikiti, nyumba ya Imam nk? huyu ni mdini kama Chadema wenzie tu Mwenyezimungu amhukumu anachostahiki
 
Vyombo vya habari ni mhimu sana duniani....

nasikitika kuona wabunge bado wanatumia fedha zao kwa maendeleo ya wananchi. Ndo maana wanadai posho kubwa. Lazima tuwe tunawashirikisha wananchi kwa harambee nk. Kuna mfuko wa jimbo fedha zinagawanywa vipi? Anyway nimefurahishwa na miradi ya umeme mashuleni na mingine inayowajenga wananchi kwa leo,kesho na keshokutwa.
 
jana nilikuwepo stand ya boma nikaona watu wa bodaboda wakikimbilia eneo la tukio, inasemekana alikuwa anakwepa mtu wa baiskeli then akaingia korongoni
 
Back
Top Bottom