"Ujinai" wa Lulu katika "mauaji" ya Kanumba (R.I.P)

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Naanza na kutoa Pole kwa watanzania wote, hasa ndugu jamaa na marafiki wa karibu wa Kanumba The Great (R.I.P) kabla sijatoa mchango wangu kuhusu hili jambo zito na nyeti ambalo limetawala maongezi katika kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka. Mengi yamesemwa na pia kuna mengi pia hayajasemwa, moja wapo likiwa "ujinai" wa Lulu katika kifo cha Kanumba.

Katika mukatadha wa sheria, tunaona kwamba Tanzania ni moja ya nchi zenye kuuweka uwajibikaji kijinai kuwa chini ya UMRI wa miaka 18 kwa kuweka miaka 10 kama umri ambapo mtu anaweza kushtakiwa kwa kosa la jinai. (Linganisha na Kenya miaka 8, Zimbabwe -7,Zambia 8,Africa Kusini 10) n.k. Ina maana kwamba mtu (mtoto) aliye chini ya umri huu hawezi kushtakiwa labda ithibitishwe kuwa alikua anajua kabisa anachokifanya. Lulu hafit kwenye kundi hili hata kama ana umri wa miaka 17 kama ambavyo Mh Halima Mdee ame tweet leo baada ya kumtembelea LuLU Oysterbay Polisi.

Tukiacha sheria na matakwa yake, kwa kuzingatia yale yanayosemwa kuhusu mkasa huu wa kifo cha Kanumba (R.I.P), inatupasa tuone kuwa kila hadithi ina pande mbili. Hadithi ya Kanumba ambaye kwa sasa hayupo kuelezea, na hadithi ya Lulu aliye mahabusu. Inasikitisha sana kwamba kifo kimetokea katika mazingira ya kutatanisha. Kifo hiki kimesikitisha watu wengi na kufanya udadisi wa kutaka kujua ukweli ulio objective iwe vigumu. Watu wamebakia kushusha lawama ZOTE kwa Lulu tu bila kutaka kujua haswa ilitokea nini hadi kifo hicho kikatokea.

Kama watanzania wengine napenda niseme kwamba , nahuzunika kama wengine kumpoteza Kanumba na pia kuona ndoto zake kama msanii zikizimwa ghafla. Aidha wapenzi wake wamekatishwa ile raha ya kuendelea kuburidika na filamu zake. Pamoja kuwa na huzuni kuu, pia najaribu kuangalia upande wa pili – Lulu! Huyu binti wa miaka 17/18 kijamii bado ni msichana mdogo japo kisheria hasamehewi kuwajibishwa kijinai. Lakini uwajibishwaji huo utakuja pale upelelezi utakapokamilika. Kufuatana na waliobahatika kumuona huyu binti, ana majeraha kuashiria kuwa alipigwa na kuumizwa na marehemu. Ingekuwa marehemu hakufa, basi nadhani kesi hii ingekuwa ya aina yake kama ingefika kunakohusika. Wote walijeruhiana. Lakini mazingira ya kujeruhi huko ni yepi?

Tumeambiwa na hata kusoma kwamba:

1. Lulu alienda kwa Kanumba usiku mkali mishale ya saa 6, kusudi watoke kwenda kucheza muziki kwa msanii Chaz baba – Mashujaa band ( Kanumba alishapiga simu kutaka andaliwe viti na sehemu maalum ya kukaa yeye na marafiki zake na pia akiomba hata wimbo maalum atakapofika)
2. Lulu alitoka nje kusikiliza simu – Kanumba akamfuata na kumrudisha ndani ili aeleze anaongea na nani.( Hapa tunaona kabisa Kanumba akianzisha shari yeye mwenyewe badala ya kuepuka shari)
3. Kanumba alimfungia Lulu ndani wakawa wanagombana. Aggressor hapa ni Kanumba na siyo Lulu.Kelele za ugomvi ziliashiria vurugu na kwa vile mlango ulifungwa na ufunguo, ilikuwa vigumu Lulu kukimbia tena au hata watu nje kuja kutoa msaada.
4. Lulu alitoka nje kwenda kumwita Seth na kumwambia Kanumba kaanguka.Lulu alikimbia akiwa na majeraha.Hii haionyeshi kuwa Lulu aliua vinginevyo angetoka kimya kimya akatokomea.

Sasa ndugu zanguni, kwanini Lulu anaonekana alifanya mauaji ya kukusudia? Ikiwa Kanumba alianguka katika purukushani na kuponda kichwa na kufa, Lulu kaua vipi? Kukamatwa na polisi na kushikiliwa ili kusaidia uchunguzi ni utaratibu wa kawaida sana. Nimewahi kushuhudia mtu kajiua, ndugu yake na mkewe waliomgundua kajining'iniza walikamatwa wakakaa ndani ili wasaidie uchunguzi Ilahali mtu kajiua mwenyewe. Ilisikitisha sana kwa maana wafiwa walitiwa misukosuko kwa kifo ambacho marehemu alijiletea kwa kujitundika. Walikaa masaa kadhaa kabla ya ndugu kwenda kuwatetea na kushinikiza waachiwe!

Kwenye hii kesi ya Lulu, bahati mbaya sana Lulu ana sifa mbaya kwenye jamii kiasi kwamba hakuna mtu anathubutu kumtetea na kumsaidia angalau aweze kujipanga kukabiliana na siku za kusubiri hatma baada ya upelelezi. Kibaya zaidi kuna statements za watu wazito ndani ya jamii, statements ambazo zenyewe tu zimeshapasisha kwamba Lulu ndio muuaji. Kibaya zaidi, unyeti wa hali inayozunguka msanii maarufu kipenzi cha wengi utaathiri hata mwenendo mzima wa upelelezi na kitakachojiri to the detriment of Lulu.

Nadhani kwa vile hii haijawa kesi ya kimahakama, na kwa vile jamii inazungumzia hiki kifo, hakuna ubaya tukawa na scenario zote.

Sijaandika haya kwa vile nataka kumsemea Lulu asiwajibike kama anahusika kijinai bali najaribu kupanua mjadala.

Nawasilisha.
WoS.
 
kuumizwa kwa lulu(majeraha) kulitokana na nini?
Kipigo kutoka kwa kanumba?
Kipigo kutoka kwa seth?
Kipigo kutoka kwa polisi wakati wa mahojiano?
Kipigo kutoka kwa majirani au mashabiki wa kanumba?
Majeraha ya kujipandikiza(self inflicted)?
Majeraha kabla ya kufika kwa kanumba(labda wazazi walimpiga)?
................
Hapa ndipo tutakapoona weledi wa forensic investigators nchini kwetu.
 
Amini usiaminni, huwezi kujadili jambo hili bila kupata maelezo ya Lulu na seth toka kwenye jalada kule polisi ukalisoma. Na hayo maelezo ndiyo yatakayopelekwa kwa mawakili wa serikali ili kulingana na maelezo hayo ya yale ya mashahidi wengine, wadetermine kama itakuwa murder or manslaughter.

However, it is most likely kuwa maslaughter kwa mtazamo wa juu juu, hata hivyo hatuwezi kusema chochote bila kusoma maelezo ya cautioned statements na yale ya mashahidi ambayo yapo kule polisi. zaidi ya hapo, kujadili jambo ambalo hujui facts zake vizuri, ni kutwanga maji kwenye kinu.
 
hapa naona kila mtu anaelezea jinsi anavyo hisi na sio hali halisi ilivyo na je tumuamini nani kati ya lulu na seth maana ndio ma suspect wa kubwa ngoja tuone weledi wa TISS yetu siku zijazo..
 
Hata kama Lulu aliua basi ni kwa bahati mbaya wakati akijitahidi kuepuka kipigo au kujihami asiuliwe/kujeruhiwa yeye yaani Self-Defense, hivyo bado ana nafasi ya hata kuwa huru akipata wakili mzuri na kuthibitisha motives was Self defense au kupata adhabu ndogo ya manslaughter (kuua bila kukusudia). Motive ya murder in first degree(kukusudia) haipo kabisa hapo.
 
kuumizwa kwa lulu(majeraha) kulitokana na nini?
Kipigo kutoka kwa kanumba?
Kipigo kutoka kwa seth?
Kipigo kutoka kwa polisi wakati wa mahojiano?
Kipigo kutoka kwa majirani au mashabiki wa kanumba?
Majeraha ya kujipandikiza(self inflicted)?
Majeraha kabla ya kufika kwa kanumba(labda wazazi walimpiga)?
................
Hapa ndipo tutakapoona weledi wa forensic investigators nchini kwetu.

Umegusa penyewe kabisa!
Ukiangalia mazingira ya tukio, sijaona kiwango cha kuridhisha kutosha kukusanya ushahidi forensically.Eneo la tukio limeingiliwa na watu wa kila aina kiasi ambacho sijui kama kweli inawezekana kupata forensic evidence.Pia Kanumba alipofikishwa Muhimbili alipelekwa motuary moja kwa moja......
 
dah, nashkuru sana Womanofsubstance,
nakubalia na ujumbe wako kwa asilimia 100% kwamba ni ngumu sana kumuita lulu muuaji kuendana na hayo mazingira na hata kama atakua kwa njia moja amehusika na kifo cha kanumba naamini si kwa makusudi bali ni katika jitihada za kujinusuru!!
siamini kwamba lulu alitoka huko kote usiku kwa nia ya kwenda kuua jamani.....
Nilimpenda sana kanumba na kazi zake ila Mungu amempenda zaidi
Nampenda sana lulu, pamoja na ukorofi alonao bado anahitaji kutendewa haki katika hili
 
Hata kama Lulu aliua basi ni kwa bahati mbaya wakati akijitahidi kuepuka kipigo au kujihami asiuliwe/kujeruhiwa yeye yaani Self-Defense, hivyo bado ana nafasi ya hata kuwa huru akipata wakili mzuri na kuthibitisha motives was Self defense au kupata adhabu ndogo ya manslaughter (kuua bila kukusudia). Motive ya murder in first degree(kukusudia) haipo kabisa hapo.

ni ushahidi gani unaokufanya useme motive ya murder haikuwepo?unajuaje kwamba lulu alifika na kifaa(mfano chuma kizito) kwa ajili ya kumpiga kanumba?
Unajuaje simu aliyopokea lulu ilimpa maelekezo nini cha kufanya ili amuadhibu marehemu?
 
Utata mtupu.Mbona kuna maelezo mengine kuwa alilegea na kuanguka mwenyewe?Inapingana na suala la kupigana
 
dah, nashkuru sana Womanofsubstance,
nakubalia na ujumbe wako kwa asilimia 100% kwamba ni ngumu sana kumuita lulu muuaji kuendana na hayo mazingira na hata kama atakua kwa njia moja amehusika na kifo cha kanumba naamini si kwa makusudi bali ni katika jitihada za kujinusuru!!
siamini kwamba lulu alitoka huko kote usiku kwa nia ya kwenda kuua jamani.....
Nilimpenda sana kanumba na kazi zake ila Mungu amempenda zaidi
Nampenda sana lulu, pamoja na ukorofi alonao bado anahitaji kutendewa haki katika hili
 
kwa nini kanumba alikuwa na daktari wake?
Je alikuwa na ugonjwa wa muda mrefu(kifafa?)
je alikuwa naye kwa sababu yeye ni superstar?
Je huyu dokta ni rafiki yake tu?ilikuaje seth akamjua?ilikuaje seth akawa na namba zake?
Je kuna ugonjwa kanumba alikuwa nao siku chache kabla ya tukio?na alikuwa akiendelea na matibabu?
Huyu dokta kamuhudumia kanumba mara ngapi?
Huyu dokta anayo medical history ya kanumba?
Impression ya dokta alipofika eneo la tukio ilikuwa ni nini?
Kwa nini dokta aliombwa kufuatwa na si kutoa maelekezo kwa seth/lulu.?
 
dah, nashkuru sana Womanofsubstance,
nakubalia na ujumbe wako kwa asilimia 100% kwamba ni ngumu sana kumuita lulu muuaji kuendana na hayo mazingira na hata kama atakua kwa njia moja amehusika na kifo cha kanumba naamini si kwa makusudi bali ni katika jitihada za kujinusuru!!
siamini kwamba lulu alitoka huko kote usiku kwa nia ya kwenda kuua jamani.....
Nilimpenda sana kanumba na kazi zake ila Mungu amempenda zaidi
Nampenda sana lulu, pamoja na ukorofi alonao bado anahitaji kutendewa haki katika hili

Mimi natabari hakutakuwa na charges za murder one dhidi ya Lulu. Na kama akishitakiwa kwa murder one na haki ikatendeka basi atakuwa acquitted. Ila sidhani hata kutakuwa na kesi ya jinai.

Grounds za wrongful death zipo na familia ya Kanumba kama wakipenda wanaweza kuchukua mkondo huo. Ila Lulu ana nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom