Jimena
JF-Expert Member
- Jun 10, 2015
- 25,844
- 95,792
Sio kila siku uji wa ulezi tu jamani tuwe tunabadilisha ili kutowachosha walaji
Mahitaji:
Kiazi kitamu 1
(pia unaweza kuongeza vipimo kulingana na ukubwa wa familia yako)
Maziwa fresh kikombe 1 na nusu
Sukari 1/4 kikombe
Iriki ya unga 1/4 kijiko cha chai
Karanga kiasi zilizosagwa
JINSI YA KUTAYARISHA
Chemsha kiazi kitamu ila sasa kama utatumia presha cooker basi ni hadi zile filimbi zilie mara 2 na kama una chemsha kawaida basi chemsha hadi kiive vizuri.
Baada ya kuchemsha menya maganda kisha kisage kwenye blender
Weka kiazi kilichokwisha sagwa kwenye sufuria
Weka maziwa, karanga na sukari kisha changanya vizuri hadi vichanganyike
Weka moto wa kiasi ili uji upate kuchemka vizuri
Weka Iriki na koroga tena
Punguza moto na acha kwa dakika 10 ili uji uive vizuri
Epua uji maana uko tayari sasa
Mahitaji:
Kiazi kitamu 1
(pia unaweza kuongeza vipimo kulingana na ukubwa wa familia yako)
Maziwa fresh kikombe 1 na nusu
Sukari 1/4 kikombe
Iriki ya unga 1/4 kijiko cha chai
Karanga kiasi zilizosagwa
JINSI YA KUTAYARISHA
Chemsha kiazi kitamu ila sasa kama utatumia presha cooker basi ni hadi zile filimbi zilie mara 2 na kama una chemsha kawaida basi chemsha hadi kiive vizuri.
Baada ya kuchemsha menya maganda kisha kisage kwenye blender
Weka kiazi kilichokwisha sagwa kwenye sufuria
Weka maziwa, karanga na sukari kisha changanya vizuri hadi vichanganyike
Weka moto wa kiasi ili uji upate kuchemka vizuri
Weka Iriki na koroga tena
Punguza moto na acha kwa dakika 10 ili uji uive vizuri
Epua uji maana uko tayari sasa