Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,920
- 31,153
Heshima kwenu wakuu,
Mwanajamvi anayekwenda kwa jina ritz alituhabarisha juu ya mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa kitongoji cha Kaloleni.
Mradi wa ujenzi Kaloleni umekaa kifisadi zipo sababu kuu sita ambazo zimeuchafua mradi mzima.
[1] Mradi haukufuata utaratibu wa tenda kama sheria na kanuni za manispaa zinavyotaka.
[2] Mradi utamnufaisha zaidi mwekezaji badala ya manispaa [mwenye mali].Mwekezaji ana uhuru wa kukopa fedha kwaajili ya kuendelza mradi kwa kutumia ardhi ya manispaa sasa jiulize ni kwanini Manispaa haitumii fursa ya kukopa wenyewe na hatimae wajenge wenyewe na mwisho wamiliki wenyewe kwakuwa wana collateral.
[3] Mradi utamnufasisha/umeshamnufaisha meya wa jiji.Tayari kuna fununu Meya kashanyakua share toka kampuni ya mwekezaji.
[4] Madiwani wamepewa ofa ya kutembelea Dubai,hii ni rushwa sijui kwanini TAKUKURU mpaka sasa wako kimya.
[5] Kati ya Nyumba 100 tayari nyumba 2 zilishauzwa.
[a] Nyumba namba 11 iliuzwa kwa Mama Moshi kwakuwa alikuwa na uhusiano na marehemu Makongoro[Nyumba ndogo].Kwa wasiomfahamu Marehemu Makongoro huyu alikuwa mpiga debe maarufu tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza rasmi mwaka 1992.Marehemu Makongoro alikuwa akimiliki Land Rover pick up amabayo ilikuwa mahususi kwaajili ya uwindaji lakini kipindi cha kampeni kinapowadia alikuwa akiitumia kwa shughuli za uchaguzi hasa matangazo ya mikutano.Marehemu Makongoro ni miongoni mwa wanaCCM waliomstaki Makongoro Nyerere wa NCCR Mageuzi na hatimaye kuvuliwa ubunge wa Arusha mjini.
Nyumba namba 17 iliuzwa kwa Mama Mzunguu [Mama mchanganyiko Msambaa na Mjerumani] huyu alikuwa na ukaribu na Mheshimiwa Dr A L Mrema wakati huo akiwa Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Mambo ya Ndani.Watoto wa Mzee wa Kiraracha wakati huo wakisoma St Contantino Nje ya mji wa Arusha wakilifunga shule walikuwa wakichukuliwa na Mama Mzunguu.Mama Mzunguu pia alikuwa na uhusiano wa karibu na kigogo mwingine wa CCM Mheshimiwa Zamu Zamu [Mkwe]so up uwezekano alisaidiwa kuuziwa nyumba either na Dr A L Mrema au Mheshimiwa Zamu Zamu.Mheshimiwa Zamu Zamu alikuwa wakala pekee wa usambazaji wa sukari zipo taarifa kwamba alikuwa akidaiwa mabilioni na CRDB akasingizia kifo mpaka leo kuna taarifa kwamba anaishi Zanzibar kama ulikuwa unashangaa mchezo wa Balali wako walio tangulia zamani kuucheza.Mheshimiwa Zamu Zamu aliwahi kutoa fedha nyingi kwa CCM mkoa wa Arusha kwaajili ya kampeni pia aliongeza urefu wa ukuta wa uwanja wa Sheikh Amri Abeid hili kuzuia vijana wasiweze kuruka ukuta kwa urahisi.Enzi za utawala wa Dr Salimin Amour Mheshimiwa Zam Zam alikuwa juu sana alikuwa hashikiki.
[6] Wakaazi wengine 98 wa nyumba za Kaloleni waliomba nao wauziwe nyumba kama wenzao walivyouziwa lakini kwakuwa hawakuwa na kigogo wa kuwakingia kifua hawakuuziwa badala yake wanatakiwa kuondoka hili kupisha ujenzi wa nyumba mpya amabo haukufuata taratibu.
Mheshimiwa Mbunge wa Arusha yuko sahihi kupinga mradi tumuunge mkono.
Naomba kuwasilisha.
Mwanajamvi anayekwenda kwa jina ritz alituhabarisha juu ya mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa kitongoji cha Kaloleni.
Mradi wa ujenzi Kaloleni umekaa kifisadi zipo sababu kuu sita ambazo zimeuchafua mradi mzima.
[1] Mradi haukufuata utaratibu wa tenda kama sheria na kanuni za manispaa zinavyotaka.
[2] Mradi utamnufaisha zaidi mwekezaji badala ya manispaa [mwenye mali].Mwekezaji ana uhuru wa kukopa fedha kwaajili ya kuendelza mradi kwa kutumia ardhi ya manispaa sasa jiulize ni kwanini Manispaa haitumii fursa ya kukopa wenyewe na hatimae wajenge wenyewe na mwisho wamiliki wenyewe kwakuwa wana collateral.
[3] Mradi utamnufasisha/umeshamnufaisha meya wa jiji.Tayari kuna fununu Meya kashanyakua share toka kampuni ya mwekezaji.
[4] Madiwani wamepewa ofa ya kutembelea Dubai,hii ni rushwa sijui kwanini TAKUKURU mpaka sasa wako kimya.
[5] Kati ya Nyumba 100 tayari nyumba 2 zilishauzwa.
[a] Nyumba namba 11 iliuzwa kwa Mama Moshi kwakuwa alikuwa na uhusiano na marehemu Makongoro[Nyumba ndogo].Kwa wasiomfahamu Marehemu Makongoro huyu alikuwa mpiga debe maarufu tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza rasmi mwaka 1992.Marehemu Makongoro alikuwa akimiliki Land Rover pick up amabayo ilikuwa mahususi kwaajili ya uwindaji lakini kipindi cha kampeni kinapowadia alikuwa akiitumia kwa shughuli za uchaguzi hasa matangazo ya mikutano.Marehemu Makongoro ni miongoni mwa wanaCCM waliomstaki Makongoro Nyerere wa NCCR Mageuzi na hatimaye kuvuliwa ubunge wa Arusha mjini.
Nyumba namba 17 iliuzwa kwa Mama Mzunguu [Mama mchanganyiko Msambaa na Mjerumani] huyu alikuwa na ukaribu na Mheshimiwa Dr A L Mrema wakati huo akiwa Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Mambo ya Ndani.Watoto wa Mzee wa Kiraracha wakati huo wakisoma St Contantino Nje ya mji wa Arusha wakilifunga shule walikuwa wakichukuliwa na Mama Mzunguu.Mama Mzunguu pia alikuwa na uhusiano wa karibu na kigogo mwingine wa CCM Mheshimiwa Zamu Zamu [Mkwe]so up uwezekano alisaidiwa kuuziwa nyumba either na Dr A L Mrema au Mheshimiwa Zamu Zamu.Mheshimiwa Zamu Zamu alikuwa wakala pekee wa usambazaji wa sukari zipo taarifa kwamba alikuwa akidaiwa mabilioni na CRDB akasingizia kifo mpaka leo kuna taarifa kwamba anaishi Zanzibar kama ulikuwa unashangaa mchezo wa Balali wako walio tangulia zamani kuucheza.Mheshimiwa Zamu Zamu aliwahi kutoa fedha nyingi kwa CCM mkoa wa Arusha kwaajili ya kampeni pia aliongeza urefu wa ukuta wa uwanja wa Sheikh Amri Abeid hili kuzuia vijana wasiweze kuruka ukuta kwa urahisi.Enzi za utawala wa Dr Salimin Amour Mheshimiwa Zam Zam alikuwa juu sana alikuwa hashikiki.
[6] Wakaazi wengine 98 wa nyumba za Kaloleni waliomba nao wauziwe nyumba kama wenzao walivyouziwa lakini kwakuwa hawakuwa na kigogo wa kuwakingia kifua hawakuuziwa badala yake wanatakiwa kuondoka hili kupisha ujenzi wa nyumba mpya amabo haukufuata taratibu.
Mheshimiwa Mbunge wa Arusha yuko sahihi kupinga mradi tumuunge mkono.
Naomba kuwasilisha.