Ujenzi wa Gas-Pipeline kutoka Mtwara-Dar unaanza kuingia nyongo..

Katika siku za karibuni husani mwaka 2000-2010 wanaharakati wamekuwa wakipiga kelele jinsi mataifa ya nje yanavyoshirikiana na baazi ya viongozi wasio waaminifu kuhamisha rasilimali za nchi kutoka tz kupeleka mataifa ya magharibi.
Mifano imejitokeza kwenye secta ya madini ambapo wawekezaji wamediriki kuchukua mchanga na kupeleka ulaya ukachekechwe kisa teknolojia ya kufanya hiyo shughuli haipo hapa kwetu.

Siku za hivi karibuni Mh. JK ameweka bayana juu ya mpango wa serikali kuweka pipeline ya gas kutoka Mtwara kuipeleka Dar ili kuzalisha umeme.Habari zilizopo ni kwamba baazi ya wakazi wa Mtwara wameanza kuhasishana kuupinga mradi huo kwa kilelezo cha kuwa kwa nini umeme usizalishwe Mtwara kisha ukasafirishwa? Kuna ugumu gani kwa hilo?.

Mara nyingi serikali kupitia viongozi wasio na uzalendo wamekuwa wakikwepesha miradi kwenye maeneo fulani na kuipeleka kwenye maeneo wanayotoka bila kujali uwiyano ktk mgawanyo wa rasilimali .Hili la mtwara kuukwepesha mradi wa ujenzi wa power plant unakwepeshwa makusudi
Hivi hiyo gas ni kwa ajili ya umeme tu hakuna matumizi mengine?.Dar kuna viwanda vingi vinaweza kuuziwa hiyo gas ili iwe mbadala wa mafuta ambayo ni ghali sana. Vilevile gas inahitajiwa dar kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya majumbani. Cha msingi tu Mtwara wasiachwe mbali sana, hiyo kampuni itakayoshughulikia gas basi ijihusishe kwenye mambo ya kijamii ya wana mtwara.likiwamo ujenzi wa mashule,hospitali,barabara nk
 
Nadhaan Huu Mradi Kama Hakuna Ufisadi Katikati Yake nadhan ni Bora gas isafirishwe kwa Bomba kwani Matumizi ya Gas yapo ya aina nyingi!! Kwanza Kuzalisha Umeme; Pili Kutumika Raw Viwandani; Tatu Matumizi ya Nyumbani!! Kama huko Mtwara watakuwa wanahitaji raw gas nao wataachiwa Matoleo Yao!! Suala la umeme Mtwara Tayari wanao wa Kutosha Unaozalishwa na Artumus!! Nadhani cha Muhimu wanachotakiwa kukifanya ni Kuwashauri wabunge wao wasimame Kidete waweze Kuiondoa Tanesco Kwenye Supply ya Huo Umeme kwani nadhani Ukiritimba na Gharama zitapungua sana!! Hawa Jamaa wanazalisha Megawati 18; Ila matumizi kwa sasa ni Megawati 10; Megawati 8 hazina Watumiaji!! Live Data!!
Huwa Wachina ni watu ambao wako so Corrupt!! Ingekuwa ni fresh Deal kutoka nchi ambayo ina reputation Nzuri katika suala la Kuzuia Rushwa nisingekuwa na Wasi!! Ila kwa wachina!!! Sijui!! Yangu Macho!! Mimi ningependekeza Hao Wachina watukopeshe Hizo Hela na sisi tutafute Reputable Contractor kwa free Tendering procedure Aweza kufanya Kazi hiyo ya Ujenzi!! Kwani by any How we are supposed to pay for the loan!! Nawasilisha

Mbona hii mitambo ya megawatt 18 imeshauzwa kwa serikali na siku yoyote TANESCO wanaanza rasmi kuiendesha. Kwa sasa wafanyakazi wa hiyo Artumus Power LTD ambayo baadae iliitwa Wentworth Power LTD wanasubiri tu notes na mshiko wao waanze mbele. Taratibu zote za kuuziana zimeshakamilika na listi ya watu ambao TANESCO ingependa waendelee kufanya nao kazi iko hadharani tangu leo mchana. Ni mipango tu kwamba Mtwara itarudi gizani siku sio nyingi japo gas imejaa tele. Na kiukweli running cost za hii kitu ni kubwa na hasa kwa usanii wa watu wetu.
 
ni kweli unachokisema Njowepo. mtoa mada anapaswa kufanya utafiti kidogo, kusafirisha umeme ni ghali sana na unapotea mwingi ni afadhali kusafirisha gas kwenye pipe. pia akumbuke kuna mitambo ya umeme kule mtwara na hili la kwamba gas ina matumizi mengi sana huku dar na mikoa mingine kama viwanda, majumbani nk

Kwa nini mnang'ang'ania kuwa umeme uliopo Mtwara unatosha? Tunataka viwanda pia viwepo tena sio tu vidogo. Hatukatai gas kusafirishwa lakini basi na huku tuone faida za kuwapo kwa gas hiyo. Kama mitambo mikubwa itakuwa Dar nani atajali kama Mtwara itaingia gizani, nani atakumbuka kuiweka kusini kwenye grid ya taifa. Kuna mema mangapi yanaliwa na kusazwa Dar na miji mingine mikubwa lakini kusini na hata miji mingine midogo hayapo. Hii spirit of sharing mbona inabagua? Huu umeme unaonekana unatosha ni kwa sasa kwa sababu ya ukiritimba wa TANESCO na serikali kwa jumla. Mtwara na Lindi ina wateja kibao ambao wanatamani kupata umeme lakini TANESCO inasua sua kuwapa huduma hii. Mimi mwenyewe nimeomba umeme tangia July 2007 mpaka leo sijapata na gharama zinapanda kila siku. At peak hours 12MW zinatumika, hizo MW 6 zinatosha kwa kiwanda gani?
 
Kwa nini mnang'ang'ania kuwa umeme uliopo Mtwara unatosha? Tunataka viwanda pia viwepo tena sio tu vidogo. Hatukatai gas kusafirishwa lakini basi na huku tuone faida za kuwapo kwa gas hiyo. Kama mitambo mikubwa itakuwa Dar nani atajali kama Mtwara itaingia gizani, nani atakumbuka kuiweka kusini kwenye grid ya taifa. Kuna mema mangapi yanaliwa na kusazwa Dar na miji mingine mikubwa lakini kusini na hata miji mingine midogo hayapo. Hii spirit of sharing mbona inabagua? Huu umeme unaonekana unatosha ni kwa sasa kwa sababu ya ukiritimba wa TANESCO na serikali kwa jumla. Mtwara na Lindi ina wateja kibao ambao wanatamani kupata umeme lakini TANESCO inasua sua kuwapa huduma hii. Mimi mwenyewe nimeomba umeme tangia July 2007 mpaka leo sijapata na gharama zinapanda kila siku. At peak hours 12MW zinatumika, hizo MW 6 zinatosha kwa kiwanda gani?
Laiti watawala wetu wangekuwa makini haya mambo yasengeenda mramba kama moto unavyoanza kuwaka kwa kasi kipindi hichi. Walishadokezwa kuwa mradi ule wa pipeline ya gas una mashaka walipaswa kuyafanyia kazi maoni na maono ya watu. Wataumbuka vibaya sana wakipuuza hizi kuni chache zinazoongezwa mototo uendelee kushika kasi zaidi na zaidi
 
Back
Top Bottom