Ujenzi na Siasa UNIVERSITY OF DODOMA

Si kweli mkuu, kuna ukweli mwingi wa kifo cha udsm in re building UDOM,
mfano mzuri ni ukwapuaji wa wataalamu toka ud to UDOM, hili wanalifanikisha kwa kukiwezesha chuo cha UDOM financially, kiasi kwamba, wakimchukua lecturer ud, mshahara kidogo, akifika udom anakuwa sr. lecturer, na marupu rupu kibao, nani hapendi pesa? mwishowe walimu wazuri wanachukuliwa toka UD kwenda UDOM

Hiyo ya mlimacity sawa, lakini madhara makubwa yapo katika ukosefu wa pesa ili hali UDOM zinamwagwa kama njugu, chakushangaza vyote ni vyuo vya uma!


Naunga mkono ujenzi wa chuo kikuu dodoma ...lakini isiwe sababu ya kuuwa vyuo vyetu tulivokuwa navyo.....mwisho wa siku tukishindwa kufikia malengo dodoma tutajikuta na hivi vingine vimekufa......bajeti za vyuo vikuu vyote zipitiswe bila kupendelea vyote ni vyetu...la sivyo itajenga makundi ...na kukifanya chuo kikuu cha dodoma kijengwe kama moto wa mabua...kikakosa misingi imara ya kukifanya kiendelee baada ya wale waazilishi kuwa hawapo.....

matatizo ya wanafunzi vyuo kama sokoine ,mlimani etc yasiifanye wanasiasa wakaamua kuviacha....kwani tayari vyuo hivi vinaheshimiaka.....na tungependa pia UDOM nayo ifuate nyayo kwa kuwa chuo kikuu kikubwa kusini mwa sahara kwa ukubwa na ubora...

upanukaji wa chuo lazima uendane na muda na upimwe kwa ubora....ukiangalia chuo kikuu cha makerere kina miaka karibu 75 na kina wanafunzi 50,000......sisi tunataka kufikisha wanafunzi 40,000 ndani ya miaka 5....nafikiri kisomi hii sio sawa....ukuaji lazima uende na uzoefu ,,...na muhimu ni ubora si namba...,tutajikuta bila kuwa na misingi imara tunaanguka ,...tuwe makini na hii ni changamoto kwa wasomi pale...how do we sustain the growth in such in short life span......the test of time is always a good experimint!!!

nadhani kabla ya kufikisha wanafunzi 40,000 udom ....tungeanza na angalau 10,000 tuangalie matatizo na mafanikio ...wakisha dahilishwa [graduate] thats 4 years ..tunafanya ongezeko la asilimia 50.....na kuendelea ...ingekuwa busara kutumia miaka 15 kufikisha wanafunzi 40,000.......na wakati huo huo tukifikisha wanafunzi 50,000 mlimani.., sokoine 20,000 ,mzumbe 10,000, etc ...na kuwezesha vyuo vikuu binafsi kimazingira kutoa jumla wanafunzi 100,000 ndani ya miaka 10 ijayo.....tukiweza kupeleka asilimia 75% ya wanafunzi wenye sifa vyuo vikuu itakuwa hatua kubwa kufikia maendeleo ya kielimu......sambamaba na kutumia open university kusaidia wale walio makazini kupata sifa bila kuadhiri tija!!
 
mbona sekta zingine wazawa wameweza?

tatizo ni kuwa ma archietcts wetu walikuwa wapo kwenye comfort zones na sasa baada ya hii sekta kufunguka kwa wengine wanaishiwa hawawezi kucompete kwenye hii competitive market sasa wapewe tuu kwa sababu ya uzawa?

Hivi ushaona majengo mengi yaliyokuwa designed na local architectss? acha tuuu. hao akina MD Consultancy na wengineo they have yet to buld anything utakachosema kuwa ni worth it

Mfano tazama jengo jipya la ARECO pale samora, ni zuri kwa kulitazama lakini unajiuliza how energy friendly will it be? ukwli ni kuwa hakuna kitu kama lile la pale Bibi Titi MOhammed

kwa kuanza wangeanza kumerge na makampuni ya nje ili wapate ujuzi na connections zaidi kuliko kukngangania kufanya boashara kizamani.

Mkuu GT MD Consultancy ni kati ya Ma-architect wazawa waliofanya kazi nzuri peke yao na nyingine kwa kushirikiana na wageni. eg PPF tower, Stanbic bank kinondoni, Machinga Complex etc. yeye ni mchoraji si mjenzi kama ARECO tofautisha.

Hao ARECO kazi zao zote au 95% wanafanya JV na wachina, na ndicho muhimu.

Wazawa wanaweza sana wakiwezeshwa, mradi mkubwa iliyojengwa na wazawa ni kama PPF Tower parking structure, ila wako wachache na hawana mitaji na vifaa.
 
Mkuu GT MD Consultancy ni kati ya Ma-architect wazawa waliofanya kazi nzuri peke yao na nyingine kwa kushirikiana na wageni. eg PPF tower, Stanbic bank kinondoni, Machinga Complex etc. yeye ni mchoraji si mjenzi kama ARECO tofautisha.

Hao ARECO kazi zao zote au 95% wanafanya JV na wachina, na ndicho muhimu.

Wazawa wanaweza sana wakiwezeshwa, mradi mkubwa iliyojengwa na wazawa ni kama PPF Tower parking structure, ila wako wachache na hawana mitaji na vifaa.
Mi naamini yapo makampuni mengi ya wazawa yenye nia na ari ya kufanya vizuri katika construction industry. Mazingira ya sasa yanawapata ugumu hasa kwenye suala la capital. Kwa unyeti wa sector hii kwa maendeleo ya Tanzania, itakuwa jambo la busara kuangalia namna ya kuwawezesha kufanya kazi zenye viwango vya juu badala ya kuwapa wazawa wageni 100%.Tunahitaji kuwa na macontractor wa ndani wenye uwezo huo.
 
hebu nifafanulie kwa undani na kwa data zaidi namna gani Mlimani inaachwa kufa..sijakuelewa

Kuna ukweli kisasi fulani - niliwahi kutembelea pale CoET/UDSM wakati mvua inavyesha. Yaani kuanzia kwenye corridor hadi laboratory/workshop niliyoenda paa lilikuwa linavuja - jamaa niliyemtembelea alikuwa amekinga kindoo maji yasitawanyike. Kuangalia juu ceiling imedondoka (sehemu) imebaki vipande vipande na kusababisha harufu ya vyooni iingie hadi sehemu ya kazi! Ila jamaa wamo tu wamezoea hiyo harufu/kama vile haipo vile. Inatia huruma. Yale majengo yaliyojengwa miaka 35 iliyopita na kweli yanahitaji yahudumiwe. Si ajabu hayajawahi kufanyiwa mainteinance yoyote kubwa kwa miaka hiyo yote.
 
halafu wale ma armchair critics ambao hawajawahi kukanyaga ardhi ya Tanzania wanapiga kelele ohh CCM haina inachokifanya! hakuna anayekataaa kuna matatizo kwenye system lakini ukiwa on the ground mazuri yanayofanyika lazima ukubali kuwa wako mbele kukamilisha ilani ya uchaguzi ya 2005

GT tulikuona unakoelekea lakini hukuwa muwazi tukaona tukuache na kweli umeyasema yaliyo moyoni. So kwa kujengwa kwa UDOM tusikemee wizi wa mabilioni dhidi ya mali za maskini wa kitanzania, EPA, Tangold/Meremeta kwa uchache tu? After all kwani hiyo serikali imejenga kwa michango ya wanachama wa ccm? Si ni kodi za walalahoi (wafanyakazi maana wafanyabishara/mafisadi wako exempted kwenye kodi kibao) ndizo zilizojenga?

Ni wajibu wa serikali kuboresha elimu na mengineyo so tunayohaki ya kukaa kimya pale wanapotekeleza wajibu kwani wanalipwa kwa hilo lakini ni haki yetu kupiga kelele kwa sauti kuu pale tunapoona dhamana ya kutuongoza tuliyowapa wanaitumia kwa maslai binafsi.
 
Hapana Shaka kuwa nakumbuka kuwa wakati wa uchanguzi mwaka 2005 Bwana Freeman Mbowe alisema kuwa, kama akipata urais atafanya mji wa Dodoma kuwa kitivo cha Elimu cha Tanzania kwa sababu hauna rasilimali za kutosha kama vile Madini na vitu vigine, hivyo wakati mwingine lazima kupongeza wakina Mbowe na Jk aliamua kufanya uamuzi huo na sio Ilani ya CCM
 
Serikali imejitahidi kuwasaidia wale ambao tayari walikuwa nyumbani kuchunga ng'ombe kwani passmark zao hazikuwezesha kujiunga na UDSM,SUA,MUHIMBIRI NK.
Tatizo ni jinsi watakavyofanikiwa kupata ajira ukilinganisha hivi sasa ajira nyingi bado zimeshikiliwa na wakongwe.Lakini cha kusikitisha zaidi ni jinsi wanafunzi wa UDOM walivyo marimbukeni wa ngono,yaani ni aibu sana pale Dodoma.Hivi sasa machangudoa wengi wanajiita wasomi wa Udom kwani ndio waliopo ktk soko baada ya kuwazidi kete watoto wa CBE.Muda wa jioni utaona magari ya wakubwa yakipishana hapo Chimwaga kufuatilia vidosho wa Udom,nenda katika sehemu za starehe kama mabaa pale chako ni chako,royal village,actic open bar,saturday bar,kilimani,mwanga bar n.k mademu wengi utakaowakuta hapo ni wasomi wa Udom.Hivi sasa Claster 1 wamefunga chuo hadi mwezi oktoba utaona wanafunzi wengi wa kike wa Udom wanasambaa mitaani kutafuta waheshimiwa ili kuweza kupitisha siku,wengi wanasema miezi minne ya kukaa nyumbani ni mingi mno.
Wana JF naomba tuwasaidie hawa vijana la sivyo hakutakuwa na taifa lijalo.Mungu ibariki elimu ya TZ.
 
......NADHANI KIKWETE AMEKUWA MNO OCCUPIED NA DODOMA KIASI KUWA WANAACHA MLIMANI INAKUFA...kumbukeni mlimani kipo au kilikuwa kati ya vyuo vikuu 100 bora duniani...naambiwa sasa kinashuka kwa kasi ya ajabu....

miradi yote ya elimu ya juu lazima iende sambamba na kuimarisha ile tuliyokuwa nayo.....wote ni watoto wetu...hatuwezi kuwatenga wengine tu kwa kuwa ni watukutu....mtoto wako akikunyea hukati mkono..sasa watu wanahisi kuwa wanasiasa wana chuki na mlimani hasa kutokana na misimamo yao kisiasa...rais kikwete hajapata kufanya ziara rasmi mlimani zaidi ya kuhudhuria graduation ya rzwani na salama kama mzazi!!..hapo dodoma kila akiwa pale lazima apite UDOM...Wote wanao baba!!

Mzee check facts zako. Mlimani kuwa kwenye 100 katika fani gani? Ujamaa na kujitegemea.
 
Si kweli mkuu, kuna ukweli mwingi wa kifo cha udsm in re building UDOM,
mfano mzuri ni ukwapuaji wa wataalamu toka ud to UDOM, hili wanalifanikisha kwa kukiwezesha chuo cha UDOM financially, kiasi kwamba, wakimchukua lecturer ud, mshahara kidogo, akifika udom anakuwa sr. lecturer, na marupu rupu kibao, nani hapendi pesa? mwishowe walimu wazuri wanachukuliwa toka UD kwenda UDOM

Hiyo ya mlimacity sawa, lakini madhara makubwa yapo katika ukosefu wa pesa ili hali UDOM zinamwagwa kama njugu, chakushangaza vyote ni vyuo vya uma!


mkuu haya ni ya kweli? mie kama siamini, sio UDSM wanajiua wenyewe kwa ukiritimba wao, vijana wanakimbilia UDOM wakaanzishe nafasi zao baada ya kubanwa sana na wa wazee maprof walitangulia wanajilimbikizia miradi, na wale junior wanabaki wakihangaika, nasikia pale pana jamaa pesa za miradi zinakaa katika personal akaunti,


nadhani hili la mshahara si sahihi! mbona nasikia scale itumikayo ni moja labda kama pana allowance kidogo iliyoongezeka UDOM na MUCE, lakini bado wa UDSM wana faidika na kuwa mjini, facility, etc
 
Mzee check facts zako. Mlimani kuwa kwenye 100 katika fani gani? Ujamaa na kujitegemea.

Hapa tuko pamoja mkuu. UDSM sio chuo bora kiasi hicho. Kwanza katika Afrika hakuna chuo chochote kilichomo kwenye 100 best. Labda vile vinavyofanya utafiti wa kuruka na ungo!

Acheni kutuzuga. UDSM is just a university. Baadhi ya wahadhiri wake ni vihiyo na vibonde kama waliopo vyuo vingine vya elimu ya juu.

Juu ya UDOM, nadhani CCM inataka kutumia kama mtaji wake kisiasa kama anavyoainisha Game Theory. Unfortunately, kile chuo kinaweza kuishia kuwa cha kibabaishaji, mfanowe hakuna. Sababu yake ni siasa za kichovu kuingilia pale.

Kwa hali ilivyo sasa UDOM sio chaguo la kwanza la wanafunzi wanaojiamini ni brightest. Vilaza wengi wamekimbilia pale. Well, pengine sio vilaza, ila hawakufaulu vizuri mitihani ya kumaliza huko walikotoka.
 
......NADHANI KIKWETE AMEKUWA MNO OCCUPIED NA DODOMA KIASI KUWA WANAACHA MLIMANI INAKUFA...kumbukeni mlimani kipo au kilikuwa kati ya vyuo vikuu 100 bora duniani...naambiwa sasa kinashuka kwa kasi ya ajabu....

miradi yote ya elimu ya juu lazima iende sambamba na kuimarisha ile tuliyokuwa nayo.....wote ni watoto wetu...hatuwezi kuwatenga wengine tu kwa kuwa ni watukutu....mtoto wako akikunyea hukati mkono..sasa watu wanahisi kuwa wanasiasa wana chuki na mlimani hasa kutokana na misimamo yao kisiasa...rais kikwete hajapata kufanya ziara rasmi mlimani zaidi ya kuhudhuria graduation ya rzwani na salama kama mzazi!!..hapo dodoma kila akiwa pale lazima apite UDOM...Wote wanao baba!!

Acha mlimani ife ....wamezidi na ukiritimba. Nakumbuka zamani miaka ya 80 hadi 90 eti mtu aliye hitimu FTC haruhusiwi kujunga degree hapo....! Halafu uzembe umewajaa viongozi wa mlimani, wanajali siasa kuliko taaluma!!
 
Tarehe 23-25 june 2009 kuna interview zimefanyika hapa New Delhi, India kwa ajiri ya walimu wa UDOM sasa watanzania wenzangu muwaangalie sana hawa wahindi wanakuja. Baadhi yao nawafahamu ni scientists/engineers wazuri lakini wana tabia ya kuficha baadhi ya mambo wanapofundisha. Sasa kama UDOM hakuna utaratibu wa kuwa utilize fully, tutaambulia patupu. Walioko TZ tusaidiane......
 
Sijui ni kwanini hiyo UDOM inaanzishwa kama vile imetokea ajali ya Earth quake kwahiyo tunaokoa majeruhi,too fast,too ambitious! Kwanini tusiende taratibu,wakati tunaendelea kujenga na kukipanua tusomeshe walimu wengi zaidi(Ulaya/US etc) badala ya kubahatisha tu mara walimu toka India mara walimu fake toka kenya mara walimu part time...Chuo kikuu gani cha serikali kinaendeshwa katika mtindo wa kiprivate namna hiyo? Mwelekeo huo sio mzuri. Just mtizamo lakini.
 
Wakati mwingine huwa natamani kulia mimi wenyewe kwa ajili ya Taifa langu kama Mtanzania na vile nauchungu sana katika Taifa langu. Sisi watanzania lazima tujenge Taifa letu wenyewe na sio kutegemea kama hivi ilivyo na pia kufanya yale ambao yanafanyika huko!! Lazima tuwe makini sana kwa ajili ya Chuo Hiki na Walimu Pia
 
Hapa tuko pamoja mkuu. UDSM sio chuo bora kiasi hicho. Kwanza katika Afrika hakuna chuo chochote kilichomo kwenye 100 best. Labda vile vinavyofanya utafiti wa kuruka na ungo!

Acheni kutuzuga. UDSM is just a university. Baadhi ya wahadhiri wake ni vihiyo na vibonde kama waliopo vyuo vingine vya elimu ya juu.

Juu ya UDOM, nadhani CCM inataka kutumia kama mtaji wake kisiasa kama anavyoainisha Game Theory. Unfortunately, kile chuo kinaweza kuishia kuwa cha kibabaishaji, mfanowe hakuna. Sababu yake ni siasa za kichovu kuingilia pale.

Kwa hali ilivyo sasa UDOM sio chaguo la kwanza la wanafunzi wanaojiamini ni brightest. Vilaza wengi wamekimbilia pale. Well, pengine sio vilaza, ila hawakufaulu vizuri mitihani ya kumaliza huko walikotoka.

UDSM ingekuwa kwenye 100 dunia, wala wasingetegemea mshiko wa serikali tena. Kwa maisha yalivyo cheap Tanzania, wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali wangekuja kusoma. Na makampuni ya kimataifa yangemwaga mapesa kwa sababu ya research.

Kuwepo kwa chuo kimoja kikubwa kunaleta ukiritimba tu. Ni lazima UDSM apate wapinzani hili chuo hicho kijiendeshe kwa kutumia vipaji sio kwa kutumia sifa za kuwa nchi haina vyuo vingine.
 
UDSM ingekuwa kwenye 100 dunia, wala wasingetegemea mshiko wa serikali tena. Kwa maisha yalivyo cheap Tanzania, wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali wangekuja kusoma. Na makampuni ya kimataifa yangemwaga mapesa kwa sababu ya research.

Kuwepo kwa chuo kimoja kikubwa kunaleta ukiritimba tu. Ni lazima UDSM apate wapinzani hili chuo hicho kijiendeshe kwa kutumia vipaji sio kwa kutumia sifa za kuwa nchi haina vyuo vingine.
Umesema Ukweli, Wakati nchi nyingine zinajitahidi hata kutoa majina ya wafanya biashara kwenye Lecturers hall hapa kwetu ni tofauti kabisa
 
Kuna watu wengine bwana very cynical. Eti kuna jamaa anasema University of Dodoma imejengwa ili kuwatamanisha mawaziri na watumishi wengine wa juu wa serikali kuhamia haraka huko maana visichana vya UDSM na IFM na CBE ndio kikwazo kikubwa kwao.

Kuna ukweli wowote katika hili ?
 
Kuna watu wengine bwana very cynical. Eti kuna jamaa anasema University of Dodoma imejengwa ili kuwatamanisha mawaziri na watumishi wengine wa juu wa serikali kuhamia haraka huko maana visichana vya UDSM na IFM na CBE ndio kikwazo kikubwa kwao.

Kuna ukweli wowote katika hili ?

Hayo ni mazungumzo baada ya habari mkuu!
 
Back
Top Bottom