Hikma
JF-Expert Member
- Apr 27, 2012
- 497
- 413
Asante sana Mh. Mbunge kwa taarifa hii ila ningependa kutoa maombi mawili na kuulizwa swali moja.Kwa sasa umeme umefikia eneo la Camel Oil. Nimewataka Tanesco kuingiza kwenye Mipango yao mradi wa kufikisha umeme Mwasonga.
Kwa kupitia mradi umeme vijijini (REA) maeneo ya Kimbiji na Kisarawe II yatapata umeme. Kazi hii kwa sasa inaendelea.
Kwanza ni kuhusu kuiangalia upya barabara ya Kibada - Mwasonga. Ukarabati uliofanyika baada ya kuisha kwa msimu wa mvua haukuwa kiwango ambapo kilichofanyika ni kupitisha greda tu.
Hii imepelekea maeneo korofi kuchimbika mapema sana sababu hakuna kifusi kilichoongezwa na hasa ukitilia maanani kuwa barabara hiyo siku hizi inatumika na magari mazito ya sementi.
La pili ni kuomba kwamba utilie mkazo mradi huu wa umeme ili waty wa mwasonga tuweze kupiga hatua za maendeleo kwa haraka.
Na mwisho ni swali langu kutaka kujua ni lini mradi wa chuo cha kilimo cha wakorea Mwasonga utaanza ili wadau tujipange kuchangamkia fursa.
Asante