Ujenzi Mkubwa unaoendelea Kigamboni(Dege Eco Village), ni mradi wa nani?

mmaroroi

JF-Expert Member
May 8, 2008
2,960
544
Wana jamvi,

Kuna mradi mkubwa wa ujenzi wa magorofa unaendelea Kigamboni. Ni Kigamboni ndandani mbele Zoo na naambiwa unaitwa "Dege Eco Village".

IMG_9549.jpg


Wengi wa wafanyakazi ni wazungu wenye asili ya Kituruki. Kazi inafanyika usiku na mchana.

Wenye ukweli kuhusu mradi huo mtujuze.

Karibuni wanajamvi.

=====
BAADHI YA MAJIBU:
MBUNGE:
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni

====
MDAU:
Jamani huyo ni Iqbal mdogo wake na Bahgdad aliyefungwa kwa rushwa.

Iqbal ni kijana mdogo tu na ndiye aliwahi kupewa eneo la Mnazi Mmoja. Alikuwa rafiki mkubwa mno na meya wa Dar wakati huo, Kitwana Kondo.

Hayo mambo ya kampuni ya Azimio ni mchongo tu, mradi wa mji wa kisasa wa Kigamboni ni wa George Bush mtoto. Na amekuwa akija hapa nchini kimya kimya hadi anamaliza siku sita kufuatilia mradi wake.

Mradi huu unaouzungumzia, wa NSSF na Azimio ni magumashi kama yale ya Manji na NSSF. TUSUBIRI.

Jiulizeni huko Kigamboni huyo mwarabu Iqbal na mwenzake Manji wamenunua maeneo makubwa mno ya ardhi na ndiyo ati wanaingia ubia na miradi ya mashirika ya umma.

Wanachukua ardhi ya umma wanaiuzia serikali, nchi hii!

Kwa taarifa yenu, ukanda wote wa Pwani (karibu kilometa 300) toka Kigamboni hadi Mtwara umeshanunuliwa WOTE na vigogo serikalini ili kuvizia wawekezaji na kuwinda ule mradi mfu wa Mtwara Dev. Corridor.
 
nilikua
najua ni mradi wa bush jr. maana niliwahi kusikia tetesi kuwa amenunua
eneo kubwa sana kigamboni anataka kufanya uwekezaji.
 
Sasa hivi usijisumbue kuuliza jengo hili ni la nani unapoteza wakati wako bure, maana haataa serikali siku hizi haina majengo inapanga kwa wenye majengo yaani wizara karibu zote hapo Dar , sasa wewe unamwuliza mwenye majengo hayo ukapange?
 
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni
Wabunge wote wangekuwa na majibu ya moja kwa moja namna hii lau nchi ingeendelea, lakini kuwapata wabunge na kuwauliza maswali ya papo kwa hapo mpaka kipindi cha kampeni, hawapo majimboni na wakiwepo kuwaona tu tabu!

Tunashukuru sana Mh.

Vipi nyumba hizo ni za kupangisha au zitauzwa, na mikataba kati ya Azimio na NSSF ikoje, au ni siri?
 
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni
Asante kwa majibu mazuri.

Ila mimi kama mmoja wa wapiga kura wako naomba usisahau kusisitiza selikari ya Tanganyika kwenye Katiba Mpya.
 
Na Mkuranga nayo ina Wachina kibao wanatengeneza yebo yebo, tunakula nao kuku wa kienyeji mitaa ya Dundani/Mwanambaya. Mitaa ya Kisemvule kwenda mbele ni Hwang Hoo.

Wanatugongea mademu zetu hapa Mwalusembe hadi basi
 
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni
Ni mradi mzuri kwa Dr. Dau kustaafu nao hapo atakula kiulaini.

Dr. Dau kawekeza sana Kigamboni ndiyo maana hata daraja ni muhimu sana kwake kuliko
 
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni

Hivi kwenye Katiba ni ruhusa mtu kumiliki eneo lote hilo la ardhi kiasi cha kujenga nyumba 7,000?
 
Back
Top Bottom