Ujenzi bora wa mabanda ya kufugia kuku wa kisasa na kienyeji

Kwa kuku wa kienyeji.....ufugaji mzuri ni wa nusu huria kwa maana ya usiku wanalala bandani mchana nje.
Kwa kuanzia vyumba vitatu: 1: mita 3 (kuku wanaoanzia miezi 2 na kuendelea) 2: mita 2 (kwa mitetea wanaoatamia) 3: mita 2 (kwa ajili ya vifaranga ambao watahifadhiwa kwa kutumia joto, liwe la umeme, maji ya moto kwenye dumu n.k).

Linatakiwa kuwa na madirisha mbele yenye ukubwa kama wa futi 2 kwa kila chumba na mlango unaokuwezesha kuingia bila vikwazo..............Urefu wa banda kama mita 3 tu zinatosha kwa maana kwamba unaweza kuingia na kufanya usafi bila tatizo.

Kumbuka kuku ni ndege kwa hiyo unaweza kupitisha fito pembeni ili wanaotaka kulala wamening'inia wasipate shida. Chini weka pumba za mpunga au maranda ya mbao kuabsorb kinyesi ili kupunguza bakteria.

Kwa sababu ni wa kienyeji nje ya banda unazungushia uwa wa waya ili wasitoke lakini wapate nafasi ya kufanya mazoezi, na kula. Banda la aina hii lina uwezowa kuchukua kuku 300.
 
Mnaouliza ukubwa wa banda ninavyojua kuku wakubwa wa mayai 7-9 kwa square metre moja na wa nyama 9-10 kwa square metre moja
ina maana kuku mia tano ni banda (500kuku/10)= 50m2 approx 5mx10m au kipimo chochote upate 50m2 hii kwa broiler
layers kwa sababu ya viota na pia sababu wataishi muda mrefu wanahitaji space zaidi kuweza kufanya mazoezi (hawahitaji uzito mkubwa)
kuku 500/9 = 55.5m2 approx 5mx11m
ila ngoja wengine waje watoe ushauri zaidi
space pia inategemea mzunguko wa hewa, kama huna space au umebanwa usijaze kuku ili kuepuka vifo kwa magonjwa yanayoambukizwa kwa hewa. All the best

Ndivyo nilivyoshauriwa pia......asante
 
Maundumula na akohi mpo!
Kwa kuku wa kienyeji.....ufugaji mzuri ni wa nusu huria kwa maana ya usiku wanalala bandani mchana nje.
Kwa kuanzia vyumba vitatu: 1: mita 3 (kuku wanaoanzia miezi 2 na kuendelea) 2: mita 2 (kwa mitetea wanaoatamia) 3: mita 2 (kwa ajili ya vifaranga ambao watahifadhiwa kwa kutumia joto, liwe la umeme, maji ya moto kwenye dumu n.k).

Linatakiwa kuwa na madirisha mbele yenye ukubwa kama wa futi 2 kwa kila chumba na mlango unaokuwezesha kuingia bila vikwazo..............Urefu wa banda kama mita 3 tu zinatosha kwa maana kwamba unaweza kuingia na kufanya usafi bila tatizo.

Kumbuka kuku ni ndege kwa hiyo unaweza kupitisha fito pembeni ili wanaotaka kulala wamening'inia wasipate shida. Chini weka pumba za mpunga au maranda ya mbao kuabsorb kinyesi ili kupunguza bakteria.

Kwa sababu ni wa kienyeji nje ya banda unazungushia uwa wa waya ili wasitoke lakini wapate nafasi ya kufanya mazoezi, na kula. Banda la aina hii lina uwezowa kuchukua kuku 300.

Platozoom unatisha mkuu, ngoja niku PM....thx

www.oric.co.tz, skype: alfred.kohi, 0784800989
 
Nimetumia mabazi ya mbao na hapo kwenye nyavu wanashinda mchana. HAINGII PANYA WALA KICHECHE

Mzee Safari naona umenipa changamoto nyingine maana sasa naweza ku design lAngu kwa muundoo huo huo ...ntaleta picha likikamilika....thx

www.oric.co.tz, skype: alfred.kohi, 0784800989
 
Nimependa ushauri wako Mama Joe, kweli mambo haya wayajua mpaka natamani ungekuwa jirani yangu nikufate unipe ushauri zaidi kabla sijaanza mradi huu ambao watu wengi wananitisha kuwa una risk nyingi ila nina tabia ya kutokuogopa hasara kama jambo nilifanyalo nalijua vizuri.
 
akohi, wadau tunaomba kufahamu umefikia wapi nasi tujaribu???
Pia tunapenda kufahamu changamoto ulizopitia.
 
Last edited by a moderator:
mkuu Chasha wewe huna banda? tuwekee bana!

Ninayo ila sijayapiga Picha, Mambanda kwa ujmla hayana Formula maalumu ya Kujenga, ni Ilimuradi yakidhi vigezo vya kutunzia kuku kama maswala ya usafu, panya wasingie, hewa ya kutosha, mwanga, na yasiwe kwenye sehemu za mikondo ya maji,
Ila kwenye ramani wapo wanao jenga ya Mviringo kama nyumba za Msonge, wapo wanao jenga ya Full suti Bati chini na juu, wapo wanajenga na kuezeka kwa makuti, wapo wanotumia Udongo kujengea, nahayo yote hufaa kulingana na maeneo ulipo,
 
Chasha ukipata chance tuwekee bana we can learn something kutoka kwako mkuu!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom