platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,366
- 11,154
Kwa kuku wa kienyeji.....ufugaji mzuri ni wa nusu huria kwa maana ya usiku wanalala bandani mchana nje.
Kwa kuanzia vyumba vitatu: 1: mita 3 (kuku wanaoanzia miezi 2 na kuendelea) 2: mita 2 (kwa mitetea wanaoatamia) 3: mita 2 (kwa ajili ya vifaranga ambao watahifadhiwa kwa kutumia joto, liwe la umeme, maji ya moto kwenye dumu n.k).
Linatakiwa kuwa na madirisha mbele yenye ukubwa kama wa futi 2 kwa kila chumba na mlango unaokuwezesha kuingia bila vikwazo..............Urefu wa banda kama mita 3 tu zinatosha kwa maana kwamba unaweza kuingia na kufanya usafi bila tatizo.
Kumbuka kuku ni ndege kwa hiyo unaweza kupitisha fito pembeni ili wanaotaka kulala wamening'inia wasipate shida. Chini weka pumba za mpunga au maranda ya mbao kuabsorb kinyesi ili kupunguza bakteria.
Kwa sababu ni wa kienyeji nje ya banda unazungushia uwa wa waya ili wasitoke lakini wapate nafasi ya kufanya mazoezi, na kula. Banda la aina hii lina uwezowa kuchukua kuku 300.
Kwa kuanzia vyumba vitatu: 1: mita 3 (kuku wanaoanzia miezi 2 na kuendelea) 2: mita 2 (kwa mitetea wanaoatamia) 3: mita 2 (kwa ajili ya vifaranga ambao watahifadhiwa kwa kutumia joto, liwe la umeme, maji ya moto kwenye dumu n.k).
Linatakiwa kuwa na madirisha mbele yenye ukubwa kama wa futi 2 kwa kila chumba na mlango unaokuwezesha kuingia bila vikwazo..............Urefu wa banda kama mita 3 tu zinatosha kwa maana kwamba unaweza kuingia na kufanya usafi bila tatizo.
Kumbuka kuku ni ndege kwa hiyo unaweza kupitisha fito pembeni ili wanaotaka kulala wamening'inia wasipate shida. Chini weka pumba za mpunga au maranda ya mbao kuabsorb kinyesi ili kupunguza bakteria.
Kwa sababu ni wa kienyeji nje ya banda unazungushia uwa wa waya ili wasitoke lakini wapate nafasi ya kufanya mazoezi, na kula. Banda la aina hii lina uwezowa kuchukua kuku 300.