Leo kwenye kipindi cha maswali na majibu bungeni, James Lembeli, yule mbunge wa Kahama aliuliza swali akitaka kujua ni kwanini moja ya barabara katika mji wa Kahama imejengwa chini ya kiwango, kiasi gani mkandarasi kalipwa na hatua gani zimechukuliwa dhidi ya mkandarasi.
Katika majibu yake waziri katika ofisi ya waziri mkuu amesema mkandarasi yeyote anayefanya kazi chini ya kiwango huchukuliwa hatua kali, na kwamba kipande cha barabara kilichojengwa ni km 1.5 na tayari serikali imelipa zaidi ya tsh billion 1 na mkandarasi kaamuriwa kurekebisha sehemu korofi kwa gharama zake.
Mimi ni mkazi wa mji huu wa Kahama, kwa kweli ni aibu tupu. Barabara hii tuliambiwa inajengwa kwa kiwango cha lami, (barabara imara ina layer zaidi ya 3 za material mbali mbali) kilichofanyika ni kuweka layer moja ya moramu na kunyunyizia MCO(kimiminika cheusi kinachowekwa kabla ya lami) halafu serikali ya ccm ikapitisha malipo ya mamilioni ya shilingi kwa mkandarasi- Jasco Construction ya jiji Mwanza kwamba kipanda hicho ujenzi tayari.
Hali ilivyo kwa sasa ni aibu, barabara tayari ina mashimo na kingo (shoulders) zilishazolewa na maji hata mwaka haujaisha.
Kahama ni wilaya yenye hazina kubwa ya madini, Migodi mikubwa miwili Buzwagi na Bulyanhulu ipo katika wilaya hii lakini huduma za jamii ni duni kupita maelezo, umeme si wa uhakika hata kwenye maeneo nyeti kama hospitalini wakati katika migodi, kwa matapeli wanaojiita wawekezaji (Barrick) ni wa masaa 24, barabara za mjini na vijijini zina hali mbaya wakati helikopta moja tu huja kuchukua dhahabu yetu yenye thamani ya zaidi ya billion 43 (rejea taarifa ya TRA kuhusu wazalendo wapenda nchi yao waliojaribu kuteka helikopta katika mgodi wa Geita mwaka jana) helikopta hizi huja zaidi ya mara 3 kwa mwezi kwa kila mgodi kuchukua dhahabu, fanya hesabu kuna migodi zaidi ya 5 kanda ya ziwa pekee.
Kwa ujumla kila mahali ni ufisadi! CCM hii inatufilisi hata maliasili zetu, lakini wasubiri 2015
Katika majibu yake waziri katika ofisi ya waziri mkuu amesema mkandarasi yeyote anayefanya kazi chini ya kiwango huchukuliwa hatua kali, na kwamba kipande cha barabara kilichojengwa ni km 1.5 na tayari serikali imelipa zaidi ya tsh billion 1 na mkandarasi kaamuriwa kurekebisha sehemu korofi kwa gharama zake.
Mimi ni mkazi wa mji huu wa Kahama, kwa kweli ni aibu tupu. Barabara hii tuliambiwa inajengwa kwa kiwango cha lami, (barabara imara ina layer zaidi ya 3 za material mbali mbali) kilichofanyika ni kuweka layer moja ya moramu na kunyunyizia MCO(kimiminika cheusi kinachowekwa kabla ya lami) halafu serikali ya ccm ikapitisha malipo ya mamilioni ya shilingi kwa mkandarasi- Jasco Construction ya jiji Mwanza kwamba kipanda hicho ujenzi tayari.
Hali ilivyo kwa sasa ni aibu, barabara tayari ina mashimo na kingo (shoulders) zilishazolewa na maji hata mwaka haujaisha.
Kahama ni wilaya yenye hazina kubwa ya madini, Migodi mikubwa miwili Buzwagi na Bulyanhulu ipo katika wilaya hii lakini huduma za jamii ni duni kupita maelezo, umeme si wa uhakika hata kwenye maeneo nyeti kama hospitalini wakati katika migodi, kwa matapeli wanaojiita wawekezaji (Barrick) ni wa masaa 24, barabara za mjini na vijijini zina hali mbaya wakati helikopta moja tu huja kuchukua dhahabu yetu yenye thamani ya zaidi ya billion 43 (rejea taarifa ya TRA kuhusu wazalendo wapenda nchi yao waliojaribu kuteka helikopta katika mgodi wa Geita mwaka jana) helikopta hizi huja zaidi ya mara 3 kwa mwezi kwa kila mgodi kuchukua dhahabu, fanya hesabu kuna migodi zaidi ya 5 kanda ya ziwa pekee.
Kwa ujumla kila mahali ni ufisadi! CCM hii inatufilisi hata maliasili zetu, lakini wasubiri 2015