Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
naombeni tips jamani jinsi ya kuishi kipindi hiki cha ujauzito niliopata hapa jf ili niweze kijifungua maxence wangu salama
nashukuruni
nashukuru kwa ushauri ivo vitu vya pinki mi wala situmiikula matunda na mboga mboga, kunywa maziwa kila siku na maini atleast once a week! acha pombe sigara, mikorogo na madawa ya nywele kipindi chote cha ujauzito!
usilale lale; be active, punguza/epuka stress!
Utazaa mtoto mzuri mwenye afya ya mwili na akili! Ukitaka afya ya roho pia; sali na mkabidhi huyo mzaliwa wa kwanza kwa mungu yeyote unayemuamini!
Ni hayo tu!
Kula matunda na mboga mboga, kunywa Maziwa kila siku na maini atleast once a week! Acha pombe sigara, mikorogo na madawa ya nywele kipindi chote cha ujauzito!
Usilale lale; be active, punguza/epuka stress!
Utazaa mtoto mzuri mwenye afya ya mwili na akili! Ukitaka afya ya roho pia; sali na mkabidhi huyo mzaliwa wa kwanza kwa Mungu yeyote unayemuamini!
Ni hayo tu!
Utunzi wa mama kabla ya kuzaa Huu ni utunzi ambao hutolewa kwa mama wakati wa uja uzito ili kuhakikisha ya kwamba mama anabakia kuwa mwenye afya na anajifungua mtoto mwenye afya.Hujumuisha mambo yafuatayo:
Historia ya uvutaji sigara, unywaji wa pombe na matumizi ya madawainafaa kutathminiwa. Pia wanawake wanashauriwa kutojitibu kabla ya kuangalia kwanza usalama wao na wa mtoto aliyetumboni. Ni bora kutaja kwamba vitamini na tiba za kutumia mitishamba zinafaa kupunguzwa wakati wa uja uzito. Kwa mfano, matumizi ya zaidi ya vidonge viwili vyaVitamini A kila siku kunaweza kusababisha dosari za kuzaliwa kwa mtoto atakayezaliwa. Mlo Ushauri kuhusu mlo unafaa kutilia mkazo mlo kamili na vyakula tofauti tofauti ukisisitizia kabohaidreti changamani na protini, pamoja na kiasi cha kutosha cha foliate(miligramu 0.5), chuma (miligramu 15) ,kalshiamu(miligramu 1200) na maji (lita 2-3) kila siku. Tembelea kituo cha afya ya mama wajawazito Tembelea ktuo cha afya ya mama wajawazito kila mwezi katika kipindi cha kwanza cha wiki 28, baadaye nenda baada ya kila wiki mbili mpaka wiki ya 36. Kutoka hapa nenda kila wiki mpaka siku ya kuzaa. Kila wakati unapotembelea kituo cha afya, hali ya afya yako na ya mtoto wako inaangaliwa. Usumbufu wa kawaida wakati wa ujauzito
|
Hapo kwenye red n bolded. Acha kumhatarisha mtoto wa mwenzio. Kula vyote ulivyoambiwa ila hiyo ya maini sikushauri kabisa dada. maini is one of the most poisonous organ of any living organisms. Sumu nyingi hukusanywa kwenye ini na kupunguzwa ukali wake kabla haijaenda sehemu nyngine za mwili. Fanya tafiti na utaniambia kwamba daktari yeyote mjanja huwa hali maini iwe ya ng'ombe au mdudu mwingine yeyote.
Usitumie hiyo kitu, kuna uwezekano, japo kidogo, ukasababisha mwanao apate hizo sumu, teratogens, zikapelekea kuzaa mtoto mwenye kasoro bure dada, acha hiyo kitu mbona mboga ziko nyingi tu.
Ubaki salama na mimba yako dada.
Asante Ndyoko....
Watu wengi tu hawajui kwamba maini sio mazuri kwa mama mjamzito....nadhani ni muhimu wamama wanapoenda clinic kwa mara ya kwanza wakawa wanataarifiwa kuhusu vyakula ambavyo wanatakiwa kuavoid ili kutohatarisha afya ya mtoto.