Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Nawaandikia ninyi vijana, alinena mwandishi maarufu, kwa kuwa mna nguvu na mmemshinda yule mwovu. Ufurahieni ujana wenu, akasisitiza mwandishi mwingine mahiri, kabla hazijaja siku zilizo mbaya, yaani siku za uzee, mtakaposema hamna furaha katika hizo. Maandiko haya yanaonesha ni jinsi gani vijana walivyo na nafasi kubwa katika maisha na jamii kwa ujumla. Pengine ndio maana Mheshimiwa Mkuu Muungwana ametamka kuwa katika Baraza lake lijalo la Mawaziri, kama atajaliwa tena na Jalia kutinga Ikulu, basi litakuwa na sura za vijana zaidi.
Sasa swali la msingi la kujiuliza ni: Je, vijana hao watakaopewa mamlaka hayo wana nguvu? Na, je, wamemshinda yule mwovu, yaani, ufisadi? Ili kulijibu hili swali ni vyema kulinganisha vijana waliopo sasa madarakani na wazee ili kuonana dalili za kupata viongozi vijana wenye nguvu na ujasiri wa kupambana na ufisadi nafsini mwao na nchini kwao. Mada pacha ya 'Uchumi wa Kifisadi: Injini inayoendesha Nchi' inatoa mwanga wa jinsi ambavyo ufisadi haujali ujana, utoto wala uzee hapa nchini Tanzania. Sasa, je, vijana wataleta tofauti gani hapo 2011?
Sasa swali la msingi la kujiuliza ni: Je, vijana hao watakaopewa mamlaka hayo wana nguvu? Na, je, wamemshinda yule mwovu, yaani, ufisadi? Ili kulijibu hili swali ni vyema kulinganisha vijana waliopo sasa madarakani na wazee ili kuonana dalili za kupata viongozi vijana wenye nguvu na ujasiri wa kupambana na ufisadi nafsini mwao na nchini kwao. Mada pacha ya 'Uchumi wa Kifisadi: Injini inayoendesha Nchi' inatoa mwanga wa jinsi ambavyo ufisadi haujali ujana, utoto wala uzee hapa nchini Tanzania. Sasa, je, vijana wataleta tofauti gani hapo 2011?