mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,767
- 7,115
tukio la kusikitisha limetokea Bunju beach Masaiti, baada ya majambazi kuja na stail mpya, staili waliohitumia ni kuchukua Defender kama ya Police na kuchukua kijana mmoja kujifanya amewekwa chini ya ulinzi nakuelekea kama kwambwa anaweza kuwaonyesha watuhumiwa wengine walipo, baada ya kufika eneo la tukio wakatoka wakiongozana na kijana aliyeshikiliwa kuelekea eneo la tukio, walipofika wakagonga, housgeli akawafungulia, wakamwambia awaonyeshe chumba cha boss wake, wakabomoa mlango na kukomba vitu vyote vya chumbani wakijifanya ni vya ushahidi, wakapanda defender na kutokomea, vijana waliowaona walikimbia hovyo wakizani polisi wanatafuta wavuta bangi.
House g. alipopiga simu na kuweleza bosi, na kubonyeza kitufe cha Ultimate Security walikuta walipishana nao wakidhani ni mapolisi wanasaidiana kutafuta watuhumiwa. Ilikuwa kama sinema. Aliyeibiwa kweli anaonekana anazo sana kwa kuwa eti ni mkurugenzi kampuni ya madini.
Fundisho.
Watu wengi wanapopata vipesa hujifanya kuweka mikwara ya ulinzi, wengi wao hawana ushirikiano na majirani, eneo hili jamaa wengi wanajifanya vibopa, wanasusia ulinzi shirikishi, umoja, uelewano mzuri na majirani. Huyu aliyeibiwa, hatoagi michango ya ulinzi wala ya umoja wa wanabunju, alipopatwa na tatizo ndipo anaaaha kuomba kujiunga. Acheni maringo jenga jamii.
House g. alipopiga simu na kuweleza bosi, na kubonyeza kitufe cha Ultimate Security walikuta walipishana nao wakidhani ni mapolisi wanasaidiana kutafuta watuhumiwa. Ilikuwa kama sinema. Aliyeibiwa kweli anaonekana anazo sana kwa kuwa eti ni mkurugenzi kampuni ya madini.
Fundisho.
Watu wengi wanapopata vipesa hujifanya kuweka mikwara ya ulinzi, wengi wao hawana ushirikiano na majirani, eneo hili jamaa wengi wanajifanya vibopa, wanasusia ulinzi shirikishi, umoja, uelewano mzuri na majirani. Huyu aliyeibiwa, hatoagi michango ya ulinzi wala ya umoja wa wanabunju, alipopatwa na tatizo ndipo anaaaha kuomba kujiunga. Acheni maringo jenga jamii.