Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Nchi ya Tanzania imepitia mifumo kadhaa ya kiuchumi. Mfumo wa kwanza wa african socialism ulioasisiwa na Mwl Nyerere ulishindwa miaka ya mwanzoni mwa 80 kwa kuzalisha umasikini, kutokuwajibika, wezi na wahujumu wa mali ya umma. Pamoja na kwamba mfumo huu na sheria ziliweka wazi viongozi kutukumiliki mali au kutokuwa na biashara bado waliendelea kuwa navyo kwa njia za panya.
Miaka ya 80 Nyerere akishuhudia umasikini, njaa, ukosefu wa bidhaa madukani, kushindwa kwa vijiji vya ujamaa na ukosefu mkubwa wa taaalamu na upoteaji mkubwa wa utu wa binadamu mwaka 1985 akaachia madaraka kwa hiari jambo na kitendo cha kishujaa kwa viongozi wa kiafrika na Tanzania ya leo.
Kwa sasa tuna mfumo wa ubepari mseto usiofuta sheria za kibepari wala usio na sheria za kudhibiti au kuumulika umezalisha wezi na viongozi wafanyabiashara kwa kutumia kodi na mali za umma bila kujali wala huruma. mfumo huu mseto ndio umewafanya viongozi wa kisiasa na serikali kujilimbikizia mali bila biashara na bila ya sheria yeyote kuhoji. Mfumo huu umemsahau mwananchi wa kawaida na mali za nchi zimekuwa zikiuzwa bila faida kwa nchi na kwa muuzaji. mfumo huu umekaribisha walafi, walaghai, wahuni, wahujumu na wasaliti kwa sababu tu hatujautengenezea sheria za kuudhibiti.
Mifumo yote miwili inaonekana inatushinda kwa sababu kama nchi hatukujiandaa kwa mfumo wa kwanza wala hatujajiandaa kwa mfumu wa pili. Katiba tuliyonayo haina nafasi kwa mifumo yote miwili. Nyerere alibeba mfumo kichwani kwake , na sasa mfumo huu wa ubepari mseto hauna sheria za jinsi ya kuuendeshal. sheria za kiuchumi haziko wazi wala za uwekezaji haziko wazi.
Ili Ubepari huu mseto uweze kufanyakazi ndani ya nchi ya Tanzania ni lazima kuangalia sheria zetu mama. katiba ijayo ni lazima ijadili kwa undani mfumo wa uchumi na jinsi ya kujenga Tanzania yenye neema. Ni kazi ya wananchi, wachumi, wanasheria, wanataaluma wote kujadili kwa kina swala la uchumi kwenye katiba yetu mpya.
Chief Mkwawa wa kalenga.
Miaka ya 80 Nyerere akishuhudia umasikini, njaa, ukosefu wa bidhaa madukani, kushindwa kwa vijiji vya ujamaa na ukosefu mkubwa wa taaalamu na upoteaji mkubwa wa utu wa binadamu mwaka 1985 akaachia madaraka kwa hiari jambo na kitendo cha kishujaa kwa viongozi wa kiafrika na Tanzania ya leo.
Kwa sasa tuna mfumo wa ubepari mseto usiofuta sheria za kibepari wala usio na sheria za kudhibiti au kuumulika umezalisha wezi na viongozi wafanyabiashara kwa kutumia kodi na mali za umma bila kujali wala huruma. mfumo huu mseto ndio umewafanya viongozi wa kisiasa na serikali kujilimbikizia mali bila biashara na bila ya sheria yeyote kuhoji. Mfumo huu umemsahau mwananchi wa kawaida na mali za nchi zimekuwa zikiuzwa bila faida kwa nchi na kwa muuzaji. mfumo huu umekaribisha walafi, walaghai, wahuni, wahujumu na wasaliti kwa sababu tu hatujautengenezea sheria za kuudhibiti.
Mifumo yote miwili inaonekana inatushinda kwa sababu kama nchi hatukujiandaa kwa mfumo wa kwanza wala hatujajiandaa kwa mfumu wa pili. Katiba tuliyonayo haina nafasi kwa mifumo yote miwili. Nyerere alibeba mfumo kichwani kwake , na sasa mfumo huu wa ubepari mseto hauna sheria za jinsi ya kuuendeshal. sheria za kiuchumi haziko wazi wala za uwekezaji haziko wazi.
Ili Ubepari huu mseto uweze kufanyakazi ndani ya nchi ya Tanzania ni lazima kuangalia sheria zetu mama. katiba ijayo ni lazima ijadili kwa undani mfumo wa uchumi na jinsi ya kujenga Tanzania yenye neema. Ni kazi ya wananchi, wachumi, wanasheria, wanataaluma wote kujadili kwa kina swala la uchumi kwenye katiba yetu mpya.
Chief Mkwawa wa kalenga.