Uislam na Makanisa

Status
Not open for further replies.

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,505
41,011
Katika vipindi mbalimbali nchini mwetu Tanzania, tumeshuhudia vurugu na fujo zenye mwelekeo wa kidini. Kuanzia zile za uvunjaji wa bucha za nguruwe (Tanzania Bara), uchomaji wa baa (Zanzibar), uchomaji wa makanisa (Zanzibar) na uchomaji wa nyumba za kuishi na biashara (Zanzibar). Na hivi sasa uchomaji wa makanisa na vitisho kwa watu wa bara waishio Zanzibar. Japo ndani yake kunaonekana ni chuki dhidi ya watu wa bara lakini ukweli ni kuwa kuna sehemu kubwa ambayo ni chuki dhidi ya Ukristo.

Watu wengi, ikiwemo watu wa kawaida na viongozi, hasa wale walio wakristo, wamekuwa waangalifu sana wa kuchagua maneno katika kuongelea mambo haya, na hasa isije ikaonekana kuwa kwa kuwa wao ni wakristo labda kwa kauli zao wanaubeza au kuudharau uislam.

Kwangu mimi, nadhani ni muhimu sana kwa Waislam wa Tanzania na Dunia nzima, kujiondoa katika kutazamwa kuwa dini yao inapenda kupalilia vurugu au mafundisho yake hayana mkazo wa dhati juu ya kuheshimu haki za watu wengine. Wasio waislam wana maswali mengi juu ya dhamira ya kweli ya Uislam kuyakubali makundi mengine yenye imani tofauti na Uislam kuishi kama jamii moja katika mazingira ya aina moja.

Waislam ni wengi sana Duniani, na kama kila Muislam angekuwa ni mtu wa vurugu basi Dunia isingeweza kukalika. Lakini hao wachache wenye kupenda fujo, mapigano na mauuaji wanaashiria upungufu fulani katika mafundisho ya uislam, maana hao wauaji wote na wapenda vurugu, kwa wakati fulani wamepitia kwenye mafundisho ya dini ya Kiislam, na hata wakati wanapofanya mauaji na mapigano hudai kuwa wanatimiza mafundisho ya Dini ya Kiislam. Huko kwenye mafundisho ya Uislam wanafundishwa nini mpaka wawe watu hayawani kabisa wa kufurahia mauaji au mapigano.

Viongozi wengi Duniani, wanapoongea mbele ya watu hueleza kuwa wanapigana na makundi ya kigaidi na siyo uislam lakini ukweli ni kuwa zaidi ya 90% ya makundi hayo ya kigaidi, wafuasi na viongozi wake ni waislam. Hiyo pekee yake ilitosha kuufanya uongozi wa dini ya Kiislam, kukaa na kujiuliza na kutafakari, kwa nini iwe hivyo, maana kwa vyovyote ni lazima kuna walakini wa mafundisho yanayosisitiza upendo na uvumilivu baina ya binadamu. Hata hapa kwetu, wakati kuna makanisa yamechomwa lakini sijawahi kusikia msikiti umechomwa moto; wakati nimesikia bucha za nguruwe, bar na nyumba za wakristo zikichomwa na Waislam lakini sijawahi kusikia biashara au makazi ya waislam yameshambuliwa na wakristo. Ninaamini utulivu wa nchi yetu umetokana na uvumilivu wa Wakristo, lakini kama na Wakristo wangetaka kulipiza kisasi, hakika Tanzania isingekuwepo.

Hapa kwetu tuna bahati kubwa, Rais wetu ni Muislam, Makamu wa Rais ni Muislam, Jaji Mkuu ni Muislam, Mkuu wa Jeshi la Polisi ni Muislam, Afisa Tawala Mkuu wa JWTZ ni muislam, hivi hawa wote wanajisikiaje katika nafasi zao hizo wanaposhuhudia kunakuwa na vurugu zinazohusishwa na imani yao? Kwa kuwa ni imani yao, nina imani kuwa walikuwa kwenye nafasi nzuri sana ya kudhibiti na kuwakanya viongozi wa dini yao wanaopandikiza na kushabikia vurugu, kama wangekuwa na dhamira. Kwa kiongozi yeyote mwenye hekima, ni aibu kubwa hata kwako binafsi kama kundi mojawapo ambalo wewe umo linatenda kinyume cha sheria na hekima.

Naheshimu sana utendaji wa Yusuph Makamba alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam juu ya uovu unaosima katika fikra za kidini, hakuwa na simile kwa waleta vurugu wowote wanaosimama nyuma ya kivuli cha uislam. Na kwa maneno yake aliwahi kusema, 'Yeyote anayefanya fujo akikimbilia msikitini tutamfuata na kumtoa, uislam unaujua wewe tu?'. Lakini hawa wa sasa katika maneno wanalaani udini lakini katika matendo wanapalilia.

Sikutaka kuongea kwa kufurahisha nafsi ya mtu yeyote bali yale ninayoamini. Ninaamini huu ni wakati sahihi kwa waislam wote nchini wanaopenda amani (ambao ni wengi), kusimama na kulaani uchafu unaofanywa na makundi ya kidini Zanzibar, na ndani ya taasisi za kuislam lazima uwepo uwezo na taratibu za kuwadhibiti watu hawa maana kwa matendo yao wanaudhalilisha uislam na Waislam, hata ifike mahali iaminike kuwa mafundisho ya dini ya kiislam yanalea na kupalilia fujo na mauaji. Kikwete, Sheni, Mwema, Zito, n.k. mko wapi? Mbona watu wanafanya ouvu nyuma ya imani yenu bila sisi wengine kuona kama kuna jitihada za wazi za kudhibiti hali hiyo. Ninyi mna bahati mnaufahamu uislam na mnafahamu sheria za nchi yetu na sheria za kimatifa, mna uwezo wa kujadiliana na wenzenu katika imani yenu na mna nafasi za Kitaifa katika jamii yetu lakini mbona hatuoni uwezo wenu? Au hata ninyi hamna uwezo juu hao waovu wanaosimama nyuma ya imani yenu?
 
Kikwete, Sheni, Mwema, Zito, n.k. mko wapi? Mbona watu wanafanya ouvu nyuma ya imani yenu bila sisi wengine kuona kama kuna jitihada za wazi za kudhibiti hali hiyo. Ninyi mna bahati mnaufahamu uislam na mnafahamu sheria za nchi yetu na sheria za kimatifa, mna uwezo wa kujadiliana na wenzenu katika imani yenu na mna nafasi za Kitaifa katika jamii yetu lakini mbona hatuoni uwezo wenu? Au hata ninyi hamna uwezo juu hao waovu wanaosimama nyuma ya imani yenu?
zitto alishatoa tamko lake la kulaani sana nyumba za ibada kuchomwa moto..hao wengine wamefurahi labda ndio maana hawjatoa matamko
 
Katika vipindi mbalimbali nchini mwetu Tanzania, tumeshuhudia vurugu na fujo zenye mwelekeo wa kidini. Kuanzia zile za uvunjaji wa bucha za nguruwe (Tanzania Bara), uchomaji wa baa (Zanzibar), uchomaji wa makanisa (Zanzibar) na uchomaji wa nyumba za kuishi na biashara (Zanzibar). Na hivi sasa uchomaji wa makanisa na vitisho kwa watu wa bara waishio Zanzibar. Japo ndani yake kunaonekana ni chuki dhidi ya watu wa bara lakini ukweli ni kuwa kuna sehemu kubwa ambayo ni chuki dhidi ya Ukristo.

Watu wengi, ikiwemo watu wa kawaida na viongozi, hasa wale walio wakristo, wamekuwa waangalifu sana wa kuchagua maneno katika kuongelea mambo haya, na hasa isije ikaonekana kuwa kwa kuwa wao ni wakristo labda kwa kauli zao wanaubeza au kuudharau uislam.

Kwangu mimi, nadhani ni muhimu sana kwa Waislam wa Tanzania na Dunia nzima, kujiondoa katika kutazamwa kuwa dini yao inapenda kupalilia vurugu au mafundisho yake hayana mkazo wa dhati juu ya kuheshimu haki za watu wengine. Wasio waislam wana maswali mengi juu ya dhamira ya kweli ya Uislam kuyakubali makundi mengine yenye imani tofauti na Uislam kuishi kama jamii moja katika mazingira ya aina moja.

Waislam ni wengi sana Duniani, na kama kila Muislam angekuwa ni mtu wa vurugu basi Dunia isingeweza kukalika. Lakini hao wachache wenye kupenda fujo, mapigano na mauuaji wanaashiria upungufu fulani katika mafundisho ya uislam, maana hao wauaji wote na wapenda vurugu, kwa wakati fulani wamepitia kwenye mafundisho ya dini ya Kiislam, na hata wakati wanapofanya mauaji na mapigano hudai kuwa wanatimiza mafundisho ya Dini ya Kiislam. Huko kwenye mafundisho ya Uislam wanafundishwa nini mpaka wawe watu hayawani kabisa wa kufurahia mauaji au mapigano.

Viongozi wengi Duniani, wanapoongea mbele ya watu hueleza kuwa wanapigana na makundi ya kigaidi na siyo uislam lakini ukweli ni kuwa zaidi ya 90% ya makundi hayo ya kigaidi, wafuasi na viongozi wake ni waislam. Hiyo pekee yake ilitosha kuufanya uongozi wa dini ya Kiislam, kukaa na kujiuliza na kutafakari, kwa nini iwe hivyo, maana kwa vyovyote ni lazima kuna walakini wa mafundisho yanayosisitiza upendo na uvumilivu baina ya binadamu. Hata hapa kwetu, wakati kuna makanisa yamechomwa lakini sijawahi kusikia msikiti umechomwa moto; wakati nimesikia bucha za nguruwe, bar na nyumba za wakristo zikichomwa na Waislam lakini sijawahi kusikia biashara au makazi ya waislam yameshambuliwa na wakristo. Ninaamini utulivu wa nchi yetu umetokana na uvumilivu wa Wakristo, lakini kama na Wakristo wangetaka kulipiza kisasi, hakika Tanzania isingekuwepo.

Hapa kwetu tuna bahati kubwa, Rais wetu ni Muislam, Makamu wa Rais ni Muislam, Jaji Mkuu ni Muislam, Mkuu wa Jeshi la Polisi ni Muislam, Afisa Tawala Mkuu wa JWTZ ni muislam, hivi hawa wote wanajisikiaje katika nafasi zao hizo wanaposhuhudia kunakuwa na vurugu zinazohusishwa na imani yao? Kwa kuwa ni imani yao, nina imani kuwa walikuwa kwenye nafasi nzuri sana ya kudhibiti na kuwakanya viongozi wa dini yao wanaopandikiza na kushabikia vurugu, kama wangekuwa na dhamira. Kwa kiongozi yeyote mwenye hekima, ni aibu kubwa hata kwako binafsi kama kundi mojawapo ambalo wewe umo linatenda kinyume cha sheria na hekima.

Naheshimu sana utendaji wa Yusuph Makamba alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam juu ya uovu unaosima katika fikra za kidini, hakuwa na simile kwa waleta vurugu wowote wanaosimama nyuma ya kivuli cha uislam. Na kwa maneno yake aliwahi kusema, 'Yeyote anayefanya fujo akikimbilia msikitini tutamfuata na kumtoa, uislam unaujua wewe tu?'. Lakini hawa wa sasa katika maneno wanalaani udini lakini katika matendo wanapalilia.

Sikutaka kuongea kwa kufurahisha nafsi ya mtu yeyote bali yale ninayoamini. Ninaamini huu ni wakati sahihi kwa waislam wote nchini wanaopenda amani (ambao ni wengi), kusimama na kulaani uchafu unaofanywa na makundi ya kidini Zanzibar, na ndani ya taasisi za kuislam lazima uwepo uwezo na taratibu za kuwadhibiti watu hawa maana kwa matendo yao wanaudhalilisha uislam na Waislam, hata ifike mahali iaminike kuwa mafundisho ya dini ya kiislam yanalea na kupalilia fujo na mauaji. Kikwete, Sheni, Mwema, Zito, n.k. mko wapi? Mbona watu wanafanya ouvu nyuma ya imani yenu bila sisi wengine kuona kama kuna jitihada za wazi za kudhibiti hali hiyo. Ninyi mna bahati mnaufahamu uislam na mnafahamu sheria za nchi yetu na sheria za kimatifa, mna uwezo wa kujadiliana na wenzenu katika imani yenu na mna nafasi za Kitaifa katika jamii yetu lakini mbona hatuoni uwezo wenu? Au hata ninyi hamna uwezo juu hao waovu wanaosimama nyuma ya imani yenu?
Mkuu wangu tafadhali sana unapolitumia jina la UISLAAM ktk maandishi yako ni lazima kwanza ufahamu nini maana ya UISLAAM badala ya kuchukua ya nchi za magharibi ktk kuutafisri uislaam na waumini wake. Usitake kutafisiri Uislaam kama unavyouchukulia Ukristu kwa sababu haviko sawa kabisa. Uislaam ni dini wakati ukristu ni imani ya ufuasi wa Yesu.

Nitakwambia kwa nini, na utanisamehe sana kwa kutumia maneno haya ambayo pengine yatakukwaza lakini ndio ukweli wenyewe - UISLAAM ni dini ambayo mtu yeyote anayejiita Muislaam lazima awe MUUMINI wa dini hii kwa kufuata mafundisho ya imani yenyewe, nje ya hapo hakuna waislaam jina ila wale wenye kufikiria kukiristu ya kwamba ukiwa mfuasi wa Yesu basi wewe umeokoka..

Kwa hiyo vitendo vya watu wote hawa wanaojiita waislaam ili hali wanafanya mambo machafu yanayokinzana na uislaam wenyewe basi bila shaka huwaondoa ktk uislaam kwa sababu Uislaam sii wa ubini, kuzaliwa wala kumfuata Mtume Muhammad bali Islaam ni dini ya mwenyezi Mungu.. hata yeye Mtume Muhammad (SAW) alikuwa muislaam na alitakiwa kufuata na kutenda mema kama unavyotakiwa wewe na mimi hapa. Hivyo hakuna musilaam kwa jina na unapotumia majina ya kina Makamba, sijui mkuu wa mkoa, usalama na kadhalika hii ni tafisri ya kikristu kwa ubatizo ukimwabudu Yesu basi wewe mkristu tosha na umeokoka.

Yaliyotokea Zanzibar ni maswala ya Kisiasa na yataendelea kuwa ya kisiasa hadi pale ufumbuzi wa swala la Muungano litakapo patiwa majibu. Binafsi yangu nitasema kwamba hawa wote wanaotaka kuuvunja Muungano ni walalahoi, watu ambao kwa bahati mbaya hawana elimu ya kutosha kuelewa kwamba kuna mahusiano makubwa kati ya hisia zao na serikali kushindwa kuondoa UMASKINI nchini hivyo wanafikiria kwamba tatizo ni bara badala ya viongozi wao na chama tawala. Kwa nini wasijiulize hivi mbona viongozi wetu wote ni wanachama wa CUF na CCM vyama ambavyo vimeungana kuiongoza nchi yetu. Kama hawa pia hawautaki muungano kwa nini wasiondoke ktk vyama hivi na kudai Zanzibar huru? wala hutawasikia Wazanzibar walioshiba waliosoma ama ambao wako madaakani isipokuwa wanaopiga kelele wote ni walalahoi wasiokuwa na mbele wala nyuma kama sisi bara tunaolia na Kikwete badala ya CCM.

Na kibaya zaidi, tazama utagundua kwamba hawa wanaochochea mgogoro wa Muungano hawana tumaini la maisha ni wale ambao kwamba wamesahaulika na utawala huu kiasi kwamba sasa imefikia kutafuta MCHAWI na hakuna aliyeko mbele yao isipokuwa tofauti zao na bara. Hi ndio athari ya watu wasiopenda kuuchosha ubongo wao kama sisi bara kuna watu wanaaamini kabisa kwamba JK ameshindwa kuongoza kwa sababu ni Musilaam na pengine angekuwa mkristu mambo yangekuwa tofauti wakitolewa mfano mzuri Nyerere na Mkapa na kuwabeza Mwinyi na Kikwete.

Hivyo basi tujiangalie sana sisi wenyewe tunapoandika habari kama hizi ambazo zinaweza kabisa kuchochea UDINI badala ya kutupatia ufumbuzi. Muislaam safi hawezio kwenda kuchoma moto kanisa ikiwa kanisa hilo nyumba ya ibada na kalikuta. Hiyo Zanzibar kuna makanisa yalikuwepo toka na kabla hata Sultan hajaweka mguu pale hivyo tuwe makini sana tunapojadili hasa maswala haya ya dini kwa sababu ndio ngao pekee ilobakia ktk ushikamano wetu. Na katika sifa za Uislaam kanisa la Jerusalem ni moja ya mahala patakatifu duniani iweje hawa watu wajidhalilishe kinyume cha hata hadithi za mtume..

Na tukiuvunja muungano kwa sababu ya dini basi sidhani kama tunaweza pata suluhisho hata huku bara maana chokochoko hizi zitaingia hadi vitandani mwetu. Imeshasemwa kwamba wahuni waliochoma makanisa watatafutwa na kufunguliwa mashtaka hivyo tuwe na subira ktk uchunguzi unapofanywa maana ni swala jingine kabisa serikali inapoingia msikitini na kuua watu au kuchoma moto makanisa na pale watu wachache wahuni wanapochukua mamlaka haya mikononi mwao.
 
Ungeandika tu "uislam na ukristo" AMA " misikiti na makanisa" ingekaa vizuri zaidi.
 
wenzio dini yao imejengeka katika uongo na imani za kibubusa, sisi dini yetu aya ya kwanza tu ni EDUCATION (IQRA-A) Quran 96: 1-5, ndo maana sheikh au imamu lazima ahojiwe. Wao kaja babu wa loliondo wakamuamini,kibwetere kawatia moto hawakuhoji. eti wachungaji nao wanatoa mapepo.

hebu tafuta mchungaji anaetoa mapepo bila kuwa na pete mkononi ya kiganga unitajie jina lake, kama si uchawi kutoka nigeria tu ili kukusanya sadaka. dini ya kiislamu hakuna sheikh anaye miliki magari, majumba, maghorofa mabenki, kwa sababu ni dini ya haki.
 
Mkuu wangu tafadhali sana unapolitumia jina la UISLAAM ktk maandishi yako ni lazima kwanza ufahamu nini maana ya UISLAAM badala ya kuchukua ya nchi za magharibi ktk kuutafisri uislaam na waumini wake. Usitake kutafisiri Uislmaam kama unavyouchukulia Ukristu kwa sababu haviko sawa kabisa.

Nitakwambia kwa nini, na utanisamehe sana kwa kutumia maneno haya ambayo pengine yatakukwaza lakini ndio ukweli wenyewe - UISLAAM ni dini ambayo mtu yeyote anayejiita Muislaam lazima awe MUUMINI wa dini hii kwa kufuata mafundsho ya imani yenyewe, nje ya hapo hakuna muislaam jina ila wale wenye kufikiria kukiristu kwamba ukiwa mfuasi wa Yesu basi wewe umeokoka na kwamba Yesu kisha yachukua madhambi yako.

Kwa hiyo vitendo vya watu wote hawa wanaojiita waislaam ili hali wanafanya mambo machafu yanayokinzana na uislaam wenyewe basi bila shaka huwaondoa ktk uislaam kwa sababu Uislaam sii wa ubini, kuzaliwa wala kumfuata Mtume Muhammad bali Islaam ni dini ya mwenyezi Mungu.. hata yeye Mtume Muhammad (SAW) alikuwa muislaam na alitakiwa kufuata na kutenda mema kama unavyotakiwa wewe na mimi hapa. Hivyo hakuna musilaam kwa jina na unapotumia majina ya kina Makamba, sijui mkuu wa mkoa, usalama na kadhalika hii ni tafisri ya kikristu kwa ubatizo basi wewe umemkubali Yesu na kuoikoka.

Yaliyotokea Zanzibar ni maswala ya Kisiasa na yataendelea kuwa ya kisiasa hadi pale ufumbuzi wa swala la Muungano litakapo patiwa majibu. Binafsi yangu nitasema kwamba hawa wote wanaotaka kuuvunja Muungano ni walalahoi, watu ambao kwa bahati mbaya hawana elimu ya kutosha kuelewa kwamba kuna mahusiano makubwa kati ya vurugu hizi na serikali kushindwa kuondoa UMASKINI nchini hivyo wanafikiria kwamba tatizo ni bara badala ya uongozi wa chama tawala.

Na kibaya zaidi, tazama utagundua kwamba hawa wanaochochea mgogoro wa Muungano hawana tumaini la maisha ni wale ambao kwamba wamesahaulika na utawala huu kiasi kwamba sasa imefikia kutafuta MCHAWI na hakuna aliyeko mbele yao isipokuwa tofauti zao na bara. Hi ndio athari ya watu wasiopenda kuuchosha ubongo wao kama sisi bara kuna watu wanaaamini kabisa kwamba JK ameshindwa kuongoza kwa sababu ni Musilaam na pengine angekuwa mkristu mambo yangekuwa tofauti wakitolewa mfano mzuri Nyerere na Mkapa na kuwabeza Mwinyi na Kikwete.

Hivyo basi tujiangalie sana sisi wenyewe tunapoandika habari kama hizi ambazo zinaweza kabisa kuchochea UDINI badala ya kutupatia ufumbuzi. Muislaam safi hawezio kwenda kuchoma moto kanisa ikiwa kanisa hilo kalikuta. Tanzania kuna makanisa yalikuweo toka na kabla hata Sultan hajaweka mguu pale hivyo tuwe makini sana tunapojadili hasa maswala haya ya dini kwa sababu ndio ngao pekee ilobakia ktk ushikamano wetu.

Na tukiuvunja muungano kwa sababu ya dini basi sidhani kama tunaweza pata suluhisho hata huku bara maana chokochoko hizi zitaingia hadi vitandani mwetu. Imeshasemwa kwamba wahuni waliochoma makanisa watatafutwa na kufunguliwa mashtaka hivyo tuwe na subira ktk uchunguzi unapofanywa maana ni swala jingine kabisa serikali inapoingia msikitini na kuua watu au kuchoma moto makanisa na pale watu wachache wahuni wanapochukua mamlaka haya mikononi mwao.

Nimefurahia mchango wako.

Lakini swali langu kubwa, ni kwa nini viongozi wa Dini ya Kiislam, kila kunapotokea matukio ambayo watu wanatumia mwavuli wa Uislam, hawajitokezi kwa nguvu zote au kuwapinga watu hao, au kupinga vikundi hivyo. Ninaposema hivyo, siliangalii suala la Zanzibar pekee yake, hata huku bara kuna wakati baadhi ya watu kila mara wamekuwa wakifanya jitihada za kutaka kuonesha kuwa shida zetu zinasababishwa na Ukristo. Na katika hilo wamejaribu sana kuonesha kuwa waislam wanatengwa katika masula mbalimbali na Wakristo wanapendelewa. Wakati mwingine yamesemwa haya hata kwa mambo ambayo ni dhahiri kabisa kuwa siyo ya kweli. Hapa bara kuna watu walifikia mpaka hatua ya kusema kuwa hata kwenye mitihani Waislam wanadondoshwa kwenye mitihani, huko Zanzibar sasa wanasema wanafunzi wa Zanzibar Wanadondoshwa kwa makusudi na NECTA ambayo kwao wanasema ni ya bara, na taswira inayojengwa kwa Wazanzibar wa kawaida ni kuwa huku Bara watu wote ni Wakristo wenye nia ya kuwagandamiza Waislam. Wakati kila siku watu wanashuhudia waislam na wakristo walio matajiri na waislam, wakristo na wasio na dini walio maskini wa kutupwa. Lakini watu wanafumba macho na masikio ili wauamini ujinga.

Matatizo tuliyo nayo yanatakiwa yatuunganishe lakini tulivyo wapumbavu, sasa yanatufanya tugawanyike.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa Mwungano wetu ukivunjika kwa Tofauti za udini, hatutakuwa salama. Hata sisi wa huku bara tutadhurika. Nakubaliana na wewe pia kuwa vurugu za Zanzibar zinachangiwa kwa kiasi kikubwa na ugumu wa maisha na kukata tamaa ya wananchi wengi, na hivyo ni rahisi mtu yeyote kujitokeza na kuwaambia wenye maisha magumu kuwa shida zenu zinasababishwa na wabara, zinasababishwa na Wakristo, nao wakakubali na kuwa tayari kuonesha hasira zao.

Swali langu kubwa, na kwa kweli sijaona jitihada ya viongozi wa dini kuwafunza waumini wao juu ya umuhimu wa kutambua kuwa hakuna dini hata moja hapa Tanzania kama Taasisi ambayo inahusika na kuwasababishia waumini wengine ufukara au mateso. Kwa nini viongozi wa kiislam hawalisemi na kulisisitiza hilo? Au nao wanafaidiki na utengano wetu? Kwa nini hawafanyi jitihada ya kuwatenga na kuwatangaza viongozi wa dini wanaohamasisha waumini wao kuwachukia waumini wa dini nyingine?
 
Zanzibar itageuka somalia na huenda haya makundi tayari yana silaha (mafunzo ya kupigana tayari wamepewa na wapo katika makundi ya Majeshi ya Serikali ya Zanzibar yasiyo tiifu kwa Rais wa Muungano)
 
Nimefurahia mchango wako.

Lakini swali langu kubwa, ni kwa nini viongozi wa Dini ya Kiislam, kila kunapotokea matukio ambayo watu wanatumia mwavuli wa Uislam, hawajitokezi kwa nguvu zote au kuwapinga watu hao, au kupinga vikundi hivyo. Ninaposema hivyo, siliangalii suala la Zanzibar pekee yake, hata huku bara kuna wakati baadhi ya watu kila mara wamekuwa wakifanya jitihada za kutaka kuonesha kuwa shida zetu zinasababishwa na Ukristo. Na katika hilo wamejaribu sana kuonesha kuwa waislam wanatengwa katika masula mbalimbali na Wakristo wanapendelewa. Wakati mwingine yamesemwa haya hata kwa mambo ambayo ni dhahiri kabisa kuwa siyo ya kweli. Hapa bara kuna watu walifikia mpaka hatua ya kusema kuwa hata kwenye mitihani Waislam wanadondoshwa kwenye mitihani, huko Zanzibar sasa wanasema wanafunzi wa Zanzibar Wanadondoshwa kwa makusudi na NECTA ambayo kwao wanasema ni ya bara, na taswira inayojengwa kwa Wazanzibar wa kawaida ni kuwa huku Bara watu wote ni Wakristo wenye nia ya kuwagandamiza Waislam. Wakati kila siku watu wanashuhudia waislam na wakristo walio matajiri na waislam, wakristo na wasio na dini walio maskini wa kutupwa. Lakini watu wanafumba macho na masikio ili wauamini ujinga.

Matatizo tuliyo nayo yanatakiwa yatuunganishe lakini tulivyo wapumbavu, sasa yanatufanya tugawanyike.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa Mwungano wetu ukivunjika kwa Tofauti za udini, hatutakuwa salama. Hata sisi wa huku bara tutadhurika. Nakubaliana na wewe pia kuwa vurugu za Zanzibar zinachangiwa kwa kiasi kikubwa na ugumu wa maisha na kukata tamaa ya wananchi wengi, na hivyo ni rahisi mtu yeyote kujitokeza na kuwaambia wenye maisha magumu kuwa shida zenu zinasababishwa na wabara, zinasababishwa na Wakristo, nao wakakubali na kuwa tayari kuonesha hasira zao.

Swali langu kubwa, na kwa kweli sijaona jitihada ya viongozi wa dini kuwafunza waumini wao juu ya umuhimu wa kutambua kuwa hakuna dini hata moja hapa Tanzania kama Taasisi ambayo inahusika na kuwasababishia waumini wengine ufukara au mateso. Kwa nini viongozi wa kiislam hawalisemi na kulisisitiza hilo? Au nao wanafaidiki na utengano wetu? Kwa nini hawafanyi jitihada ya kuwatenga na kuwatangaza viongozi wa dini wanaohamasisha waumini wao kuwachukia waumini wa dini nyingine?
Nitakujibu hivi:-
Uislaam unatulazimisha kudai UHURU, HAKI na USAWA haijalishi nani yupo madarakani na nadhani umeona hata Arab spring inafanywa na watu wanaojiita Waislaam against waislaam wenzao hivyo utakuta Uislaam sii wa kuzaliwa bali unaitumikia vipi UHURU, HAKI na USAWA wa binadamu na viumbe wote. Tunaweza rudi nyuma toka harakati za uhuru wa nchi za kiafrika, Asia au kina Saadam na kadhalika maana swala sii Ukristu ama Upagani ndio hasa sababu ya vuguvugu hili bali mfumo wa utawala unaodhalilisdha wananchi wake kwa kuwanyima uhuru, haki na usawa. Tumelazimishwa kupigania haya kwa viumbe wote na kwa kufanya hivyo ndio uislaam wenyewe.

Kwa Wazanzibar, kama nilivyosema toka mwanzo ni kwamba swala hili limeshikiriwa na watu ambao ufahamu wao ni mdogo sana ktk maswala ya kisiasa na bahati mbaya wote ni walalahoi. Umaskini wao na wetu ndio umejenga chuki hizi kiasi kwamba waislaam wanaamini Muislaam mwenzao hawezi kuwadhalilisha ama kuwatendea kinyume cha mamrisho ya dini isipokuwa yule asiyeamini. Na hii inatokana na Masheikh wengi kuutafsiri Uislaam wenyewe kama Ukristu ama Ujew kwa maana kwamba waumini wao wamekuwa Taifa, wamekuwa society inayotambuliwa kwa kumfuata Yesu (wakristu) au Juda (Jews), hivyo nao ktk mfano wa utambulisho huo huo wamejenga fikra za kwamba kuna society ya waislaam kwa kuzaliwa ama ubatizo wa kumfuata Muhammad (SAW).

Na mwisho labda niingie ktk vichwa vya hawa wanaojiita waislaam na kusema kwamba maadam mfumo wa Utalawa wetu ni mfumo unaofuata nchi za magharibi ambazo kwao Wazanzibar ni ukristu, wataendelea kuamini kwamba mfumo huu haukuletwa kuwaendeleza wao kwa sababu historia kuna ukaribu sana baina ya Ukristu na mwongozo wa kimataifa ktk ujenzi wa dola zilizopo. Na maadam wao wanataka Uhuru, haki na usawa katika baadhi ya maswala yanayowagusa lakini Utawala huu umekataa kuwapa haki hizo wataendelea kuamini kwamba ni UKRISTU unaopinga haki zao maana haiwezekani muislaam akakataa kutoa uhuru, haki na usawa ambao ameamrishwa ndani ya kuran. Na nachoweza kusema kwao tazameni Syria, Misri, Libya na nchi nyinginezo za kiislaam kuwa Uislaam sii wa kuzaliwa na wala msifikirie kabisa kwamba kila Muislaam ni muumini wa dini. Utawala dhalimu hauna dini isipokuwa mfumo unalinda maslahi ya utawala uliopo.

Binafsi yangu siwezi kabisa kuweka jitihada za kuwafunza waislaam isipokuwa ktk kile nachokielewa kwa undani maana sielwi kabisa sababu ya kuundwa kwa Muafaka wa MoU ambao unaplipa kanisa mamlaka ya kuendesha ELIMU na AFYA nchini ikiwa nchi yetu haina dini. Hivyo sii rahisi kumshawishi muislaam kutokuwepo mfumo kristu ikiwa mfumo wenyewe unaweka madaraka mikononi mwa kundi moja la kiimani..
 
Binafsi yangu siwezi kabisa kuweka jitihada za kuwafunza waislaam isipokuwa ktk kile nachokielewa kwa undani maana sielwi kabisa sababu ya kuundwa kwa Muafaka wa MoU ambao unaplipa kanisa mamlaka ya kuendesha ELIMU na AFYA nchini ikiwa nchi yetu haina dini. Hivyo sii rahisi kumshawishi muislaam kutokuwepo mfumo kristu ikiwa mfumo wenyewe unaweka madaraka mikononi mwa kundi moja la kiimani..

sas MOU unaiingiza hapa ili iweje ? umeongea maneno mengi mazuri umezunguka ila mwishoni umedisplay your real colour.. sioni tofauti ya wewe na hao mashehe wa uamsho japo unaweza sana kuchanganua mambo na sio kwamba hujui ulifanyalo ila kwa makusudi kabisa unajaribu kupotosha umma kwa kuingiza MOU hapa
 
sas MOU unaiingiza hapa ili iweje ? umeongea maneno mengi mazuri umezunguka ila mwishoni umedisplay your real colour.. sioni tofauti ya wewe na hao mashehe wa uamsho japo unaweza sana kuchanganua mambo na sio kwamba hujui ulifanyalo ila kwa makusudi kabisa unajaribu kupotosha umma kwa kuingiza MOU hapa
Mkuu wangu Bams kaniuliza swali na binafsi yangu kusema kweli sina imani na utawala uliopo hasa ulipofikia kuweka mamlaka ya ELIMU na AFYA mikononi mwa kanisa. Sielewi, na hili linanikwaza kuamini kwamba hakuna UDINI ktk mfumo wa utawala Tanzania. Haya ni mawazo yangu kubaliana nayo ama usikubaliane nayo ndivyo navyolitazama swala zima la Muafaka wa MoU....Kabish...
 
Nitakujibu hivi:-
Uislaam unatulazimisha kudai UHURU, HAKI na USAWA haijalishi nani yupo madarakani na nadhani umeona hata Arab spring inafanywa na watu wanaojiita Waislaam against waislaam wenzao hivyo utakuta Uislaam sii wa kuzaliwa bali unaitumikia vipi UHURU, HAKI na USAWA wa binadamu na viumbe wote. Tunaweza rudi nyuma toka harakati za uhuru wa nchi za kiafrika, Asia au kina Saadam na kadhalika maana swala sii Ukristu ama Upagani ndio hasa sababu ya vuguvugu hili bali mfumo wa utawala unaodhalilisdha wananchi wake kwa kuwanyima uhuru, haki na usawa. Tumelazimishwa kupigania haya kwa viumbe wote na kwa kufanya hivyo ndio uislaam wenyewe.

Kwa Wazanzibar, kama nilivyosema toka mwanzo ni kwamba swala hili limeshikiriwa na watu ambao ufahamu wao ni mdogo sana ktk maswala ya kisiasa na bahati mbaya wote ni walalahoi. Umaskini wao na wetu ndio umejenga chuki hizi kiasi kwamba waislaam wanaamini Muislaam mwenzao hawezi kuwadhalilisha ama kuwatendea kinyume cha mamrisho ya dini isipokuwa yule asiyeamini. Na hii inatokana na Masheikh wengi kuutafsiri Uislaam wenyewe kama Ukristu ama Ujew kwa maana kwamba waumini wao wamekuwa Taifa, wamekuwa society inayotambuliwa kwa kumfuata Yesu (wakristu) au Juda (Jews), hivyo nao ktk mfano wa utambulisho huo huo wamejenga fikra za kwamba kuna society ya waislaam kwa kuzaliwa ama ubatizo wa kumfuata Muhammad (SAW).

Na mwisho labda niingie ktk vichwa vya hawa wanaojiita waislaam na kusema kwamba maadam mfumo wa Utalawa wetu ni mfumo unaofuata nchi za magharibi ambazo kwao Wazanzibar ni ukristu, wataendelea kuamini kwamba mfumo huu haukuletwa kuwaendeleza wao kwa sababu historia kuna ukaribu sana baina ya Ukristu na mwongozo wa kimataifa ktk ujenzi wa dola zilizopo. Na maadam wao wanataka Uhuru, haki na usawa katika baadhi ya maswala yanayowagusa lakini Utawala huu umekataa kuwapa haki hizo wataendelea kuamini kwamba ni UKRISTU unaopinga haki zao maana haiwezekani muislaam akakataa kutoa uhuru, haki na usawa ambao ameamrishwa ndani ya kuran. Na nachoweza kusema kwao tazameni Syria, Misri, Libya na nchi nyinginezo za kiislaam kuwa Uislaam sii wa kuzaliwa na wala msifikirie kabisa kwamba kila Muislaam ni muumini wa dini. Utawala dhalimu hauna dini isipokuwa mfumo unalinda maslahi ya utawala uliopo.

Binafsi yangu siwezi kabisa kuweka jitihada za kuwafunza waislaam isipokuwa ktk kile nachokielewa kwa undani maana sielwi kabisa sababu ya kuundwa kwa Muafaka wa MoU ambao unaplipa kanisa mamlaka ya kuendesha ELIMU na AFYA nchini ikiwa nchi yetu haina dini. Hivyo sii rahisi kumshawishi muislaam kutokuwepo mfumo kristu ikiwa mfumo wenyewe unaweka madaraka mikononi mwa kundi moja la kiimani..

Ninachoona hapa ni kujaribu kuwatafutia sababu ya kwa nini wanafanya haya wanayofanya.. Hakuna excuse yeyote kwangu mimi ambayo inaweza ku-justify ukora wanaoufanya.. Nadhani ni muhimu kwa viongozi wa dini ya kiislam pamoja na waumini wote kulikemea hili kwa nguvu zao zote..! Inasikitisha kuona wewe unajaribu kuwatafutia sababu unless u sympathises with their cause..!
 
Mkandara, nimekupata. Uchomaji wa makanisa Zanzibar haujanza leo, umekuwepo kwa takriban miaka 5 sasa. Nimekuwepo Zanzibar wakati campaign ya kuchoma moto inashika kasi, and I cannot tell hofu waliyonayo wanzanzibari wakristo. Sina maneno ya kueleza juu ya hofu waliyonayo wakristo zanzibar. Sina. Misa za usiku wakati wa x'mas na pasaka huwa ni hofu tupu kwa waumini maana hawana uhakika kama ibada itaisha wakiwa salama. Na hii hali imedumu kwa miaka sasa. Watu wanatembea barabarani lakini mioyoni mwao wanajisikia yatima.

Na tukumbuke wengi wa hawa wakrtisto wana historia ndefu huko visiwani, wamekuwepo tangu wakati wa biashara ya utumwa. Kuna wagoa (catholic), kuna waanglikana, kuna lutheran, n.k wamezaliwa huko, baba zao wamezaliwa huko babu zao wamezaliwa huko sasa leo wanaambiwa hawatakiwi! Waende wapi? Na kwa nini?

Lakini pia jambo kubwa ningetaka kusema ni hili tunapoongelea uislam na ukristo tunaongelea familia zetu. Watanzania wengi wamechanginyika, ndani ya familia kuna waislam na wakristo, hivyo vurugu za kidini tafsiri yake ni ugomvi ndani ya familia zetu. Ndio sababu ni muhimu sana tena sana kwa watu wa dini zote kutoruhusu mtu au kikundi cha watu kuleta mgogoro kwa mgongo wa dini. Wataangamiza familia nyingi nchi hii. Tusiruhusu hili liendelee.

How about UAMSHO
Ninaamini kwa dhati kabisa toka ndani ya moyo wangu, viongozi wa juu wa UAMSHO hawakumtuma mtu yoyote wa dini yoyote kuchoma makanisa. Hiyo ni imani yangu. Lakini, watu waliohusika kuchoma moto wamekuwa wanahudhuria mihadhara inayoratibiwa na UAMSHO. Tukumbuke kila mtu ana utashi wake na viongozi wa UAMSHO walishiriana na viongozi wa juu toka CUF Zanzibar (sio CUF bara) wana nafasi ya peke ya kujenga amani na mshikamano Zanzibar.

Ila nataka kila mtanzania anayesoma hapa awe wa dini yoyote ile na hata asiye na dini atambue kuwa Wakristo wanaoshi Zanzibar hawana amani kabisa. Ninaomba muelewe safari ya kwenda kanisani kuabudu kwao ni safari ya mashaka na huzuni kubwa. Mtu akidondoka hata kitabu wakati wa ibada watu wanashtuka sana. Na hii hali imeluwepo kwa miaka kama 5.lakini pia wapo wenye asili ya bara, hawa nao hawako salama. Nimesoma posts za watu hapa lakini niseme kwa kifupi watu wenye asili ya bara hawako salama Zanzibar.

Tume ya katiba mpya inakuja kama jamii moja tuamue nini hatma ya nchi hizi mbili. Muda wa kufumbia macho matatizo haupo tena. Wakati huo huo ningetarajia kusikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikemea kwa dhati mambo yanayoendelea. Kimya chake kinazidisha hofu na unyonge kwa waathirika.
 
Ninachoona hapa ni kujaribu kuwatafutia sababu ya kwa nini wanafanya haya wanayofanya.. Hakuna excuse yeyote kwangu mimi ambayo inaweza ku-justify ukora wanaoufanya.. Nadhani ni muhimu kwa viongozi wa dini ya kiislam pamoja na waumini wote kulikemea hili kwa nguvu zao zote..! Inasikitisha kuona wewe unajaribu kuwatafutia sababu unless u sympathises with their cause..!
Umenisoma lakini hukuelewa ndio maana kwenda shule sii kuelimika. Nimeeleza wazi chimbuko la frustration za hawa jamaa ambao najua wanafikiria nini. Unaweza sana kuwapuuza watu na kuwakwaza ktk madai yaojapokuwa yanaweza kuwa hayana maana kabisa. Wao kwa fikra zao watatafuta sababu na nakuhakikishia Wazanzibar wanaamini wananyimwa haki zao kwa sababu haki hizi zinafungamana na imani yao ya dini na haiwezekani muislaam mwingine awanyime isipokuwa mkristu. Ni mawazo potovu lakini ndivyo wanavyoamini na kama kweli hatuna pingamizi na madai yao kwa nini tunawanyima?

Ni majuzi tu Chadema walitaka kufanya maandamano na wakakazwa na sheria gandamizi kupinga maandamano hayo kwa sababu ambazo wao hawakuzielewa isipokuwa mikwara ya CCM. Kwa nini wafikirie ni CCM ili hali aliyekataa ni mkuu wa polisi?.. Je kuna ukweli wowote kwamba CCM inahusika.. Hivyo iwe kweli ama sii kweli huwezi kumzuia mtu kufikiria nje ya kile hasa kilichofanyika.

Kama Wazanzibar hawautaki Muungano kwa fikra kwamba tuna mfumo kristu sisi tunaung'ang'ania wa nini?. Kwani hao viongozi wao kina Shein, Maalim Seif, Jussa, Bilal wanashindwa vipi kuwaelimisha wananchi wao hadi iwe swala la masheikh ikiwa wao ndio wanaowajaza ujinga hawa wananchi walalahoi kwamba umaskini wao unatokana na bara na kwanini wao bado wapo ktk uongozi wa taifa ambalo wanaamini ni la kikristu?. Hapa ndipo husema hakuna hatari kubwa kama kutumia dini ktk Siasa na ukiusoma ujumbe wa CUF leo hii utagundua kwamba wanajificha nyuma ya pazia kusema ukweli wao wamesimama wapi.
 
Nadhani watu wanapaswa waishi maisha ya maelewano na kuvumiliana ili kuleta amani. Ni aibu kwa matendo yaliyotokea iwe ni kwa sababu yeyote ile. Dini zote zinamuamini Mungu na kuhubiri upendo na amani lakini mtu akikurupuka akapata mzuka wa kuchoma nyumba ya ibada ya mwenzake ni kufilisika kimaadili, Sio bahati mbaya kwamba ni makanisa tu ndo yanayopata haya masahibu.
Ustaarabu unaota mbawa pale unapopata munkari na kupandisha mori kwamba Mungu wako ndo Mungu wa Kweli na Mungu wengine si Mungu!!! Imani ya dini ni suala binafsi wala halipaswi kuyumbisha nchi maana nchi haina dini na waumini wa dini zote ni raia wake!!! Mungu hajatoa tangazo kwamba "fulani" ndo msemaji wake kwa hio Watu walioleta hizi hujuma wasijipe "cheo" ambacho hawana" na Kama Mungu angekuwa anatangaza wasemaji wake kwa vyovyote hatawachagua wao!@!!!!
Tunategemea kwamba serikali zote zitachukua hatua kuwafikisha kwenye sheria waliohusika na kuhakikisha jambo hili la aibu halitokei tena!!!! Hili ni jambo la kikatiba la haki ya kila raia kuabudu kwa imani inayoitaka na pia ni suala la usalama wa mali za raia wake!!!! Govern-up URT and SMZ!!!
 
Mkuu wangu Bams kaniuliza swali na binafsi yangu kusema kweli sina imani na utawala uliopo hasa ulipofikia kuweka mamlaka ya ELIMU na AFYA mikononi mwa kanisa. Sielewi, na hili linanikwaza kuamini kwamba hakuna UDINI ktk mfumo wa utawala Tanzania. Haya ni mawazo yangu kubaliana nayo ama usikubaliane nayo ndivyo navyolitazama swala zima la Muafaka wa MoU....Kabish...

Mkandara, mimi sina tatizo kabisa na mtu ambaye anaeleza kutokufurahia MOU kati ya serikali na kanisa juu ya utoaji huduma za Afya na Elimu. Kutofurahia jambo fulani hakutengenezi uadui maana kuna uwezekano kabisa kuwa makubaliano yaliyofanywa kati ya serikali na kanisa, wale waliofanya waliona ni jambo jema kwa Watanzania wote. Serikali ilikuwa imeshindwa kutoa huduma nzuri za Afya na Elimu kwa maeneo yote ya Tanzania, huku Kanisa likiwa na huduma hizo za kiwango cha juu katika baadhi ya maeneo. Serikali ililiomba kanisa liruhusu huduma zake zitumike na watu wote, wenye uwezo wa kulipia na wasio na uwezo. Mhitaji huduma akifika kwenye huduma hizo apewe bure au kwa gharama kidogo kama ilivyo kwa huduma za umma. Kanisa halikuwa na kipingamizi lakini lilikuwa halina uwezo kubeba mzigo wa gharama, na ndipo serikali ikakubali kuchangia gharama za uendeshaji wa huduma hizo ambazo zinatumika na Watanzania wote bila ubaguzi. Lakini kama makubaliano haya yanawakwaza baadhi ya Watanzania, sioni tatizo kama yatavunjwa, na huduma hizo (vyuo, hospitali na shule) zikawa chini ya makanisa. Lakini ifahamike kuwa ni lazima kutakuwa na ubaguzi wa kiwango fulani maana huduma hizi zinagharimiwa kwa sadaka za Wakristo makanisani, itakuwa siyo haki mkristo anayechangia uendeshaji wa huduma hizi kila siku atozwe sawasawa na yule ambaye huwa hachangii chochote (asiye mwumini). Na ifahamike kuwa hata kama utakuwa na fedha ya kulipia bado unaweza ukakosa huduma kwa sababu ukubwa wa Taasisi hizo ni lazima utapungua kwa kutegemea uwezo wa wanaogharamia. Kwanza kwa watu wanaoishi ziliko huduma hizi, wengi wao wanalalamika kuwa ubora wa huduma umeshuka sana tangu serikali ilipoingiza mkono wake. Serikali mpaka sasa inahaha kuingiza hospitali nyingine za kanisa kwenye mfumo huo lakini katika maeneo mbalimbali kanisa limegoma kuzidi kuzijumuisha hospitali nyingine zaidi kwenye makubaliano hayo kwaajili ya kulinda ubora. Kule jimboni Njombe, kanisa limegoma kuiingiza hospitali ya Ikonda kwenye utaratibu huo, na leo wagonjwa wengi waliokuwa wakienda Peramiho kabla ya MOU, wanasafiri mamia ya kilometa kufuata huduma Ikonda. Mtu asifikirie kuwa MOU ikivunjika, kanisa litaathirika, na kinyume chake ni kuwa huduma katika taasisi zake zitakuwa bora zaidi.

Mkandala, nakuomba uwe na wivu wa kutafuta mafanikio. Sijui wewe uko wapi, lakini maeneo mengi ya Tanzania hakuna hospitali nzuri na kubwa za serikali wala Bakwata lakini kanisa linazo. Na maeneo hayo yana Waislam unataka waumini wa Kiislam wanaoishi maeneo hayo na ambao hawana uwezo wa kulipia watibiwe wapi? Au unataka watibiwe kwenye hospitali za Kanisa kwa kulipiwa na kanisa badala ya serikali yao ambayo inakusanya kodi?

Lakini kwa ufupi ni kwamba, unathibitisha kuwa baadhi ya Waislam wana chuki dhidi ya ukristo. Na kama hiyo MOU kama ni tatizo kwa nini msiongee na viongozi wenu wa kidini, mkatoa sababu na kisha mkawaona wakuu wa serikali? Kwa sababu yeyote ile sioni busara ya kuyachoma makanisa, je, ni hiyo MOU iliyokusudia kuwapa huduma bora Watanzania kwa gharama nafuu?
 
Mkandara, nimekupata. Uchomaji wa makanisa Zanzibar haujanza leo, umekuwepo kwa takriban miaka 5 sasa. Nimekuwepo Zanzibar wakati campaign ya kuchoma moto inashika kasi, and I cannot tell hofu waliyonayo wanzanzibari wakristo. Sina maneno ya kueleza juu ya hofu waliyonayo wakristo zanzibar. Sina. Misa za usiku wakati wa x'mas na pasaka huwa ni hofu tupu kwa waumini maana hawana uhakika kama ibada itaisha wakiwa salama. Na hii hali imedumu kwa miaka sasa. Watu wanatembea barabarani lakini mioyoni mwao wanajisikia yatima.

Na tukumbuke wengi wa hawa wakrtisto wana historia ndefu huko visiwani, wamekuwepo tangu wakati wa biashara ya utumwa. Kuna wagoa (catholic), kuna waanglikana, kuna lutheran, n.k wamezaliwa huko, baba zao wamezaliwa huko babu zao wamezaliwa huko sasa leo wanaambiwa hawatakiwi! Waende wapi? Na kwa nini?

Lakini pia jambo kubwa ningetaka kusema ni hili tunapoongelea uislam na ukristo tunaongelea familia zetu. Watanzania wengi wamechanginyika, ndani ya familia kuna waislam na wakristo, hivyo vurugu za kidini tafsiri yake ni ugomvi ndani ya familia zetu. Ndio sababu ni muhimu sana tena sana kwa watu wa dini zote kutoruhusu mtu au kikundi cha watu kuleta mgogoro kwa mgongo wa dini. Wataangamiza familia nyingi nchi hii. Tusiruhusu hili liendelee.

How about UAMSHO
Ninaamini kwa dhati kabisa toka ndani ya moyo wangu, viongozi wa juu wa UAMSHO hawakumtuma mtu yoyote wa dini yoyote kuchoma makanisa. Hiyo ni imani yangu. Lakini, watu waliohusika kuchoma moto wamekuwa wanahudhuria mihadhara inayoratibiwa na UAMSHO. Tukumbuke kila mtu ana utashi wake na viongozi wa UAMSHO walishiriana na viongozi wa juu toka CUF Zanzibar (sio CUF bara) wana nafasi ya peke ya kujenga amani na mshikamano Zanzibar.

Ila nataka kila mtanzania anayesoma hapa awe wa dini yoyote ile na hata asiye na dini atambue kuwa Wakristo wanaoshi Zanzibar hawana amani kabisa. Ninaomba muelewe safari ya kwenda kanisani kuabudu kwao ni safari ya mashaka na huzuni kubwa. Mtu akidondoka hata kitabu wakati wa ibada watu wanashtuka sana. Na hii hali imeluwepo kwa miaka kama 5.lakini pia wapo wenye asili ya bara, hawa nao hawako salama. Nimesoma posts za watu hapa lakini niseme kwa kifupi watu wenye asili ya bara hawako salama Zanzibar.

Tume ya katiba mpya inakuja kama jamii moja tuamue nini hatma ya nchi hizi mbili. Muda wa kufumbia macho matatizo haupo tena. Wakati huo huo ningetarajia kusikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikemea kwa dhati mambo yanayoendelea. Kimya chake kinazidisha hofu na unyonge kwa waathirika.
Mkuu wangu FJM hakuna sababu ya kuuma maneno hapa. Hawa UAMSHO ni wahuni ambao kwa madai yao yasiyokuwa na mbele isipokuwa kwa kutumia dini ndio chimbuko la uharifu wote. Wapigwe marufuku kama watakavyopigwa marufuku vyama ama vyombo vyovyote vitakavyotumia dini ktk madai ya Kijumuiya (kisiasa). Nitakwambai tu ya kwamba ktk dhehebu (kanisa) la Sunni hatuna kitu JUMUIYA inayoongozwa na Sheikh fulani au Ayatollah isipokuwa tunaamini sote tupo ktk nafasi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu, hivyo mwenye kutenda mema na yale tulolazimishwa ndiye mbora mbele ya bwana. Hatumwabudu mtu wala kutawalia kiimani na uongozi wa mtu fulkani ila wapo wenye elimu zaidi na walimu wetu ktk maswala ya dini basi.

Hawa watu wenye kueneza UDINI iwe kina Jussa sijui wengine wakidai mbele ya mihadhara wakituita sisi Wabara bomba la mavi ndio chachu ya matatizo yote haya kutokana na chimbuko la tofauti za kiimani. Kama unakumbuka mwaka 2003 niliwahi kusema hizi imani potovu zinazoingia nchini hasa nikakemea matumizi ya Alqaeda na kanisa jipya na Evanjeliko kutoka Marekani kuwa madhehebu haya yatakuja tuletea matatizo makubwa nchini na yapigwe marufuku haraka. Kuna mtu akijiita Broccolli alikuja juu na kunambia Evanjeliko sio kanisa bali ni hali ya kutetelea kulitangaza jina la bwana (crusade) - nijamjibu kwamba afanye uchunguzi vizuri ya kwamba limeundwa kanisa wanaojiita Evanjeliko na hawa ni hatari kabisa ktk maswala ya freedom of Faith kama yalivyo madhehebu ya Ala Shaabab na Boko Haram (Tea Party), leo hii haya yameota mizizi na sasa tunajiuma na kusaga meno.

Hwa watu wasakwe na kutupwa ndani na vijiwe vyao vyote vipigwe marufuku maana wanachofundisha ni chuki tupu nakokwenda siko na yatatupeleka kubaya zaidi. Hatuhitaji vikundi vya migawahani nchini (Tea party) Tanzania.
 
Hii hoja ya MOU imekuwa inapigiwa kelele sana. Kanisa halishindwi hata kidogo kuendesha hospitali au shule zake. Na kanisa halikuingukia serikali ili ipate ruzuku. Serikali haina uwezo wa kutoa huduma sehemu nyingi nchini na sasa wanatoa ruzuku kwa kanisa ili litoe huduma hiyo kwa wananchi. BAKWATA au jumuiya yoyote ya dini yoyote wengefanya hivyo pengine hii nchi ingepiga hatua zaidi ya sasa.
 
Mkandara, mimi sina tatizo kabisa na mtu ambaye anaeleza kutokufurahia MOU kati ya serikali na kanisa juu ya utoaji huduma za Afya na Elimu. Kutofurahia jambo fulani hakutengenezi uadui maana kuna uwezekano kabisa kuwa makubaliano yaliyofanywa kati ya serikali na kanisa, wale waliofanya waliona ni jambo jema kwa Watanzania wote. Serikali ilikuwa imeshindwa kutoa huduma nzuri za Afya na Elimu kwa maeneo yote ya Tanzania, huku Kanisa likiwa na huduma hizo za kiwango cha juu katika baadhi ya maeneo. Serikali ililiomba kanisa liruhusu huduma zake zitumike na watu wote, wenye uwezo wa kulipia na wasio na uwezo. Mhitaji huduma akifika kwenye huduma hizo apewe bure au kwa gharama kidogo kama ilivyo kwa huduma za umma. Kanisa halikuwa na kipingamizi lakini lilikuwa halina uwezo kubeba mzigo wa gharama, na ndipo serikali ikakubali kuchangia gharama za uendeshaji wa huduma hizo ambazo zinatumika na Watanzania wote bila ubaguzi. Lakini kama makubaliano haya yanawakwaza baadhi ya Watanzania, sioni tatizo kama yatavunjwa, na huduma hizo (vyuo, hospitali na shule) zikawa chini ya makanisa. Lakini ifahamike kuwa ni lazima kutakuwa na ubaguzi wa kiwango fulani maana huduma hizi zinagharimiwa kwa sadaka za Wakristo makanisani, itakuwa siyo haki mkristo anayechangia uendeshaji wa huduma hizi kila siku atozwe sawasawa na yule ambaye huwa hachangii chochote (asiye mwumini). Na ifahamike kuwa hata kama utakuwa na fedha ya kulipia bado unaweza ukakosa huduma kwa sababu ukubwa wa Taasisi hizo ni lazima utapungua kwa kutegemea uwezo wa wanaogharamia. Kwanza kwa watu wanaoishi ziliko huduma hizi, wengi wao wanalalamika kuwa ubora wa huduma umeshuka sana tangu serikali ilipoingiza mkono wake. Serikali mpaka sasa inahaha kuingiza hospitali nyingine za kanisa kwenye mfumo huo lakini katika maeneo mbalimbali kanisa limegoma kuzidi kuzijumuisha hospitali nyingine zaidi kwenye makubaliano hayo kwaajili ya kulinda ubora. Kule jimboni Njombe, kanisa limegoma kuiingiza hospitali ya Ikonda kwenye utaratibu huo, na leo wagonjwa wengi waliokuwa wakienda Peramiho kabla ya MOU, wanasafiri mamia ya kilometa kufuata huduma Ikonda. Mtu asifikirie kuwa MOU ikivunjika, kanisa litaathirika, na kinyume chake ni kuwa huduma katika taasisi zake zitakuwa bora zaidi.

Mkandala, nakuomba uwe na wivu wa kutafuta mafanikio. Sijui wewe uko wapi, lakini maeneo mengi ya Tanzania hakuna hospitali nzuri na kubwa za serikali wala Bakwata lakini kanisa linazo. Na maeneo hayo yana Waislam unataka waumini wa Kiislam wanaoishi maeneo hayo na ambao hawana uwezo wa kulipia watibiwe wapi? Au unataka watibiwe kwenye hospitali za Kanisa kwa kulipiwa na kanisa badala ya serikali yao ambayo inakusanya kodi?

Lakini kwa ufupi ni kwamba, unathibitisha kuwa baadhi ya Waislam wana chuki dhidi ya ukristo. Na kama hiyo MOU kama ni tatizo kwa nini msiongee na viongozi wenu wa kidini, mkatoa sababu na kisha mkawaona wakuu wa serikali? Kwa sababu yeyote ile sioni busara ya kuyachoma makanisa, je, ni hiyo MOU iliyokusudia kuwapa huduma bora Watanzania kwa gharama nafuu?
Sasa hapa ndipo nisipokubaliana nanyi kabisa. Kama kweli serikali ilishindwa kwa nini leo wanajenga Hospital na Mashule?..Shule za kata za nini kujenga na serikali ikiwa serikali ilishashindwa toka zamani. Kwa nini kushindwa kwa serikali ktk sektra hizo leo hii mnailaumu serikali na sio kanisa ama viongozi waliopewa jukumu hilo?. Majuzi tu wamefukuzwa naibu waziri wa Afya ili hali kuna ufisadi mkubwa sana kwa waliopewa mamalka na bohari ya madawa na vyombo vinavyochukua jukumu la quote n qoute - Kuendeleza ELIMU na AFYA nchini badala yake leo tunazalisha makabuntas kuliko wakati wowote wa utawala wa Nyerere. Hii ilipangwa na ndio maana swala la kuondoa muafaka huu lisiwe sababu ya kwanza badala ya kuwafukuza mawaziri ambao hawana mamlaka zaidi ya yale waliokabidhiwa.
 
ukiunganisha dots hapa utakuja kujua kuwa makanisa huko zanzibar ni kweli yamechomwa na waislamu ambao wamemezesha maneno ya chuki kuanzia MOu na mfumo kristo na mambo mengine kama hayo ..wakiwa wamejisahau kuwa utawala wote kwa sasa hivi upo mikononi mwa waislamu bara na visiwani ..

kipindi kile lawama zote walimtupia Mkapa ila sasa hivi kwa unafiki wao hawataki kabisa kumtupia Kikwete lawana kwa unafiki wao ila nina uhakika raisi angekuwa ni wa dini tofauti na yao angebeba lawama zote ama msishangae Pinda akibebeshwa lawama zote huku wakimuangalia kikwete na Bilal bila kuwarushia neno lolote ..

hawa ndugu zetu ni kazi sana kuishi nao .wamefikia hatu sasa shule zenyewe hawasomi halafu hapo hap[o wanalaumu wizara ya elimu ambayo ipo chini ya ndugu zao waislamu na kwa ujinga ukiwabana wataanza kumlaumu hata Nyerere ambaye hayupo ni marehemu ..ndio mwalimu alikuwa na mapungufu yake ila sasa kila kitu kipo mikononi mwenu badilisheni sasa pelekeni watoto shule acheni kulalama hawataki wao kila siku ni mihadhara tu na kulalamika kuwa wanaonewa.
wakristo wanaendelea kwa sababu ambazo kama kuna anayezihitaji nitazitaja ....
 
Bams,
Sikuweza kuendeleakukujibu hoja yako kwa sababu niliingiliwa na virusi ktk PC kiasi kwamba nimechukua muda mrefu kusafisha..
Hata hivyo tuendelee ktk hili, swala la makanisa kuweza kupeleka shule na mahospital hadi vijijini ni kazi waliyopewa hivyo sikutegemea wangeshindwa lakini tunatazama kipimo cha uwezo wao kulingana na mahitaji ya shule nchini. Hawakupewa mamalka hayo jana wala juzi bali ni miaka 20 iliyopita hivyo unashangaa vipi kwamba wameweza kufikisha shule hizo vijijini ilihali sijui Bakwata hawakuweza kama vile nao wamepewa jukumu hilo.

Kwanza kabisa lazima ufahamu sikubaliani na taasisi yoyote ya dini kukabidhiwa mamlaka yoyote yanayohusiana na utawala wa nchi hii iwe wizara au idara wao maswala yao ni ya kidini tu. Na watakapo wekeza ktk elimu au Afya ni msaada wao kama wanavyoamrishwa na dini na sii kuwatoza wananchi walalahoi ada kubwa ambazo hawawezi kuzimudu. Hii sii misaada bali ni biashara na kwa dini kuingia ktk biashara hakika inaondoa uzito wote wa kiimani.

Leo hii PPF au NSSF wanajenga majumba mjini kwa sababu wanashirikiana na serikali, hivi ni vyombo vya serikali na vinapoendelea wawekezaji wake ambao ni wana PPF au NSSF hufaidika pia japokuwa wanaopanga ktk majumba haya ni siii wanachama ama viuongozi wa serikali tu. Hivyo, kuwezeshwa kwa vyombo hivi huwezi kusema hata wewe unaweza kujenga majumba haya unaruhusiwa wakati chombo hiki hiki wakipewa Waislaam (Bakwata) utasema tofauti..

Mfano mwingine JK ameshindwa kutuletea maendeleo hivyo tunapomsema yeye na chama chake CCM kushindwa kutuletea maendeleo huwezi kusema kwani Chadema wameleta nini? mbona JK kajenga mabarabara hadi vijijini Chadema mmejenga nini?. haya kweli majibu ama ndio kupenda sana!

Mkuu wangu hakuna wivu isipokuwa ni kinyume cha Uhuru, haki na usawa kuweka mamlaka ya wizara muhimu sana nchini hasa tukiwa maskini tukipambana na adha kubwa ya Ujinga umaskini na maradhi - chini ya mokono wa chombo cha dini. Hawa ndio wanakuwa kama wadhamini na watawala kwa agizo kubwa la kitaifa. Ni makosa makubwa na haya yataleta madhara makubwa sana mbeleni. Nimeyasema sana hapa JF na itakuja siku mtanikumbuka.

Saint Ivuga, Mkuu wangu bora miye nayesema ukweli linalonikwaza kuliko kuweka unafiki na kuchekelea kitu ambacho sikubaliani nacho - Mficha maradhi kifo humuumbua, Now You know!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom