Uingizaji wa mabaki ya kitimoto nchini Cameroon.

Darwin

JF-Expert Member
May 14, 2008
908
56
Kuna sehemu nimesoma kuhusu hii title.

Wafugaji wengi wa Cameroon wamefilisika kwa kuingizwa kwa wingi nyama ya nguruwe kutoka nchi za Ulaya.

Nyama zenyewe ni mikia ya nguruwe, masikio, vichwa, utumbo na vitu vingi vya ndani ambavyo watu wa Ulaya hawali bali waafrika.

Wanavileta Cameroon matani kwa matani nakuuza kwa bei ya chini kabisa kiasi kwamba wafugaji wa Cameroon wanashindwa na ushindani wa nje hadi kufilisika kwani hawana wanakuwauzia nguruwe zao.

Uingizaji huo wa mabaki ya nguruwe yenye bei nafuu umesababisha kuwakosesha vijana wengi waliokua wanapata ajira kwa wafugaji wa ndani kwa kiasi cha asilimia 67% na wafugaji wengi wa ndani kufilisika.

Haikushia hapo, nchi za Ulaya sasa zinaingiza pia kuku wa bei rahisi ili kuwamaliza kabisa wafugaji wa ndani.

Haya wana forum mnalionaje hili?
 
Ahhaaaa! nasikitika sana maana najua hata hapa kwetu yatakuja tu. Nimeona nchi za Scandinavia wanazalisha kuku kwa wingi na kwa muda mfupi (wiki moja mpaka mbili) na ukimuona ni kuku mkubwa utadhani ana umri wa miaka saba. Sasa hawa wakimwagwa hapa Bpngo wafugaji wetu si watakwisha kabisa Eeeeee Mungu pitisha mbali hii dhahama.

Kuhusu k'moto hapa sijui kama tunahitaji kula masazo maana bado tunazalisha wakutosha na bei bado poa. Kwa mwezi huu Mtukufu ndio bei zitashuka maana walaji wengi wamefunga hahhaaaaaaaaaaaaa
 
Kuna sehemu nimesoma kuhusu hii title.

Wafugaji wengi wa Cameroon wamefilisika kwa kuingizwa kwa wingi nyama ya nguruwe kutoka nchi za Ulaya.

Nyama zenyewe ni mikia ya nguruwe, masikio, vichwa, utumbo na vitu vingi vya ndani ambavyo watu wa Ulaya hawali bali waafrika.

Wanavileta Cameroon matani kwa matani nakuuza kwa bei ya chini kabisa kiasi kwamba wafugaji wa Cameroon wanashindwa na ushindani wa nje hadi kufilisika kwani hawana wanakuwauzia nguruwe zao.

Uingizaji huo wa mabaki ya nguruwe yenye bei nafuu umesababisha kuwakosesha vijana wengi waliokua wanapata ajira kwa wafugaji wa ndani kwa kiasi cha asilimia 67% na wafugaji wengi wa ndani kufilisika.

Haikushia hapo, nchi za Ulaya sasa zinaingiza pia kuku wa bei rahisi ili kuwamaliza kabisa wafugaji wa ndani.

Haya wana forum mnalionaje hili?
Mkuu hata hapo Bongo ipo sasa hivi yaani mataahira wamerushusu ma apple kutoka south Africa wakati ya lushoto yanaoza bure
 
Ahhaaaa! nasikitika sana maana najua hata hapa kwetu yatakuja tu. Nimeona nchi za Scandinavia wanazalisha kuku kwa wingi na kwa muda mfupi (wiki moja mpaka mbili) na ukimuona ni kuku mkubwa utadhani ana umri wa miaka saba. Sasa hawa wakimwagwa hapa Bpngo wafugaji wetu si watakwisha kabisa Eeeeee Mungu pitisha mbali hii dhahama.

Kuhusu k'moto hapa sijui kama tunahitaji kula masazo maana bado tunazalisha wakutosha na bei bado poa. Kwa mwezi huu Mtukufu ndio bei zitashuka maana walaji wengi wamefunga hahhaaaaaaaaaaaaa

Kama sio masazo yanauzwa kwenye maelfu ya pesa utanunua na uache sijui mikia, utumbo, maini yanayouzwa kwa shilingi mia tu?
Kumbuka pia wa Cameroon pia japo yakula ambayo sio masazo lakini walikua wanakula nyama bora.
Kitu ambacho pengine hujakielewa vizuri ni kwamba watu wa ulaya kuna vitu hawali na kwa waafrika wao wanaona ni delikatese.

Ukimkaribisha mtu wa Ulaya maini basi atakuona umemdharau lakini mtu wa afrika ukimkaribisha anaona umemheshimu.

Yaani vile wanavyoona havina thamani kwao ndio wanakuja kuwauzia waafrika kwasababu waafrika wanavithamini

Hio ndio tofauti
 
Mkuu hata hapo Bongo ipo sasa hivi yaani mataahira wamerushusu ma apple kutoka south Africa wakati ya lushoto yanaoza bure


Yaani huu ni ujinga kabisa.

Kwa maana hio watu wa Lushoto nao sio muda watakuja filisika kwa kwa utaahira huu.

Taifa lenyewe linategemea kilimo kwa asilimia kubwa, sasa wale wauzaji wa mazao yakawa na ushindani na wakakosa kuuza si ndio hapo hali za maisha zitazidi kudidimia.

Kumbuka kwamba
Mkulima wa Lushoto kama hapati faida basi hata mpa ajira mtoto wa jirani aje kuchuma ma apple. ma jobbless ndio watazidi kuongezeka.
Watu wa malori nao watakosa kazi kwani hawataenda kuchukua matunda Lushoto.

Uchumi wa nchi utaendeleaje hapo? waliosoma uchumi wanifafafanulie
 
Yaani huu ni ujinga kabisa.

Kwa maana hio watu wa Lushoto nao sio muda watakuja filisika kwa kwa utaahira huu.

Taifa lenyewe linategemea kilimo kwa asilimia kubwa, sasa wale wauzaji wa mazao yakawa na ushindani na wakakosa kuuza si ndio hapo hali za maisha zitazidi kudidimia.

Kumbuka kwamba
Mkulima wa Lushoto kama hapati faida basi hata mpa ajira mtoto wa jirani aje kuchuma ma apple. ma jobbless ndio watazidi kuongezeka.
Watu wa malori nao watakosa kazi kwani hawataenda kuchukua matunda Lushoto.

Uchumi wa nchi utaendeleaje hapo? waliosoma uchumi wanifafafanulie


Jana nimemskia Bw. Luhanjo alipotemebelea Mlimani City kati ya mambo ambayo ameyaongelea ni pamoja na kukanusha kwamba wamiliki wa Mlimani City hawajakataa kununua bidhaa (mazao) za ndani, bali wanaagiza kutoka Afrika Kusini baada ya bidhaa za ndani kushindwa kutoshereza mahitaji ya supermarket yao yaani Mlimani City. Wazee hiyo imekaaje? Tunakubaliana na maneno yake hayo?
 
Jana nimemskia Bw. Luhanjo alipotemebelea Mlimani City kati ya mambo ambayo ameyaongelea ni pamoja na kukanusha kwamba wamiliki wa Mlimani City hawajakataa kununua bidhaa (mazao) za ndani, bali wanaagiza kutoka Afrika Kusini baada ya bidhaa za ndani kushindwa kutoshereza mahitaji ya supermarket yao yaani Mlimani City. Wazee hiyo imekaaje? Tunakubaliana na maneno yake hayo?


Kuleta bidhaa kutoka nchi za nje sioni kwamba ni tabu kama wana uwiano wa bei.
Kwa maana hio wazalishaji wa ndani wasipate ushindani mkubwa mpaka kufilisika.

Kwa maana hio hizo bidhaa za nje zisiwe cheap kushinda za ndani.

Kila mtu anataka urahisi lakini kama bidhaa zetu tunazozalisha hazinunuliwi kutokana na bidhaa za nje ni rahisi hapo ni dhambi
 
Mkuu hata hapo Bongo ipo sasa hivi yaani mataahira wamerushusu ma apple kutoka south Africa wakati ya lushoto yanaoza bure

Umesahau Darwin's nightmare ya mwaka 2004.... Yale Mambo yawezekana hadi leo yanafanyika..
 
Back
Top Bottom