Uhuru wetu hautoki kwa Kikwete au Rais yeyote; Rais hawezi kuwa "Dikteta kidogo"

Okay sawa Mzee! mamlaka unayo lakini kwenye hili swala la katiba busara lazima itawale.
 
The board -rais

CEO-rais

Director of Finance-rais

Human Resource Manager-rais

Production Manager-rais

Marketing Manager-rais

Night Watchman -rais

Duh! eh bana.
 
Ninaendelea kuonesha makosa ya kimantiki na kifalsafa ya hotuba ya Rais Kikwete jana. Mojawapo ya mambo ambayo aliyadai akikanusha kuwa yeye si Dikteta ni kauli hii ambayo sidhani kama watu waliielewa uzito wake. Rais alidai kitu kingine ambacho nacho pia hana!




Rais amedai vitu ambavyo vinahitaji kukataliwa mara moja kwa sababu tukivukubali tu tunampa nguvu ambazo hana.

1. Rais ndiye anayetoa uhuru wa kutembea, vyombo vya habari na hata kuwa (the freedom to be)
2. Rais ndiye anayetoa uhuru kwa watu, vyama vya siasa tena "mkubwa mno"
3. Anaweza kuingilia kati uhuru huo kwa kuwa "dikteta" kidogo.

Ndugu zangu, Uhuru wa Watanzania hautoki kwa Rais - awe Kikwete au yeyote mwingine. Katiba yetu inasema hivi kuhusu uhuru wetu: (Ibara ya 12:1)



Maneno hayo yanaweza kuonekana ni shallow au hollow lakini ni makubwa sana. Yanatueleza kwamba kila Mtu (mimi, wewe, mtoto, mzee, kijana, msomi, mjinga, kichaa, mwenye akili sana, mlevi, mzinzi hata shoga!) huzaliwa 'HURU NA SAWA'! Kwa maneno mengine uhuru wetu hautokani na rais au chama cha siasa unatokana na kuzaliwa kwetu kama BINADAMU. Ndio maana tunasema "binadamu wote huzaliwa huru na wote ni sawa".

Kwa hiyo, hoja ya kuwa uhuru wetu unatoka kwa rais au kwamba RAis anafikiria kuwa sisi tuko huru kwa sababu kaamua kutugea uhuru haina msingi, ni ya kukataliwa na kwa mara nyingine haina msingi wa Kikatiba (lacks constitutional basis whatoever).

NI kutoka katika kutambua kuwa sote tunazaliwa huru ndipo Katiba sasa inatambua uhuru huo na kuuhakikisha (the constitution recognizes and guarantee that freedom). Kumbe wananchi wanazaliwa wakiwa huru na kwa kutumia katiba yao wanajihakikishia uhuru huo - Rais hatoi wala kuhakikisha uhuru huo bali anasimamia kuwa uhuru huo hauondolewo - iwe na maadui wa ndani au wa nje - na hii ina maanisha hata na yeye mwenyewe!

Je ni uhuru gani tunazaliwa nao ambao hauwezi kuondolewa kiholela kama Rais alivyoashiria? Nitataja tu kama Katiba inavyoanisha sasa:

Uhuru wa kuwa hai (rais hawezi kuja na kumwambia polisi 'mpige huru risasi' halafu mtu akapigwa risasi kwa vile 'rais kasema'). Ili kuhakikisha hili Katiba imeweka wazi kuwa "itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kukamatwa, kufungwa, kufungiwa, kuwekwa kizuizini, kuhamishwa kwa nguvu au kunyang'anywa uhuru wake". Kwa maneno mengine ni kuwa kauli ya Rais anaweza kuwa dikteta kidogo na kuzuia uhuru wawatu haina msingi ni ya kuikataa kwani hana madaraka wala uwezo huo (nililisema hili siku ile aliposema Bungeni kuwa angeweza kuagiza Dr. Slaa akamatwe na akakamatwa)!

Uhuru wa mawazo na maoni - kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,
kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Kwa maneno mengine ni kuwa hakuna mtu anayeweza kumlazimisha mtu mwingine kufikiri au kuwa na maoni anayoyataka yeye! Kiila mtu anahaki ya kufikiri na kujenga maoni ayapendayo yeye bila kulazimishwa. Hii ina maana kuwa uhuru huu hautoki kwa Rais. Rais hawezi kutuambia kuwa sote tunatakiwa kufikiria hivi au vile na tukifikiri tofauti basi ni makosa!

Uhuru wa imani
- Katiba inatambua kuwa kila mtu ana uhuru wa kuamini au kutoamini dini yoyote. Na katiba yetu inaenda mbali zaidi na kusema kuwa mtu anayo haki ya kubadilisha imani yake. Kwa maneno mengine mtoto aliyezaliwa katika familia ya kikristu akiamua kuwa Muislamu serikali au mtu yeyote hawezi kwenda na kumlazimisha abadili. Wanaweza kumshawishi au kumuonesha makosa lakini mwisho wa siku uamuzi ni wake. Na mtu akiamua kutoamini Mungu au akiamini minazi hakuna mtu wa kumlazimisha kuwa abadili imani! Rais hawezi kulazimisha watu waamini vyovyote apendavyo yeye.


Hiyo ni mifano michache tu. Kwa ufupi ni kuwa kauli ya Rais kuwa yeye ndiye anatoa uhuru na kuwa anaweza kuuondoa uhuru huo wa kuwa "dikteta kidogo" haina msingi. Uhuru wetu hautoki kwa Rais. Period.


Ndugu Mwanakijiji..kwanza nimekugongea like na pili naomba niweke wazi hotuba ya juzi/jana sikuielewa inaelekezwa wapi mfano kwa wazee wa dar? wanasiasa? au watanzania wote hakuwa wazi kabisa...na mbaya zaidi ni pale nilipo gundua kwamba kinachoimaliza ccm ni ulevi wa madaraka wa kupindukia, wamekuwa wakiwatishia watanzania kwa kauli tofauti kama jana aliposema au awe dikteta kidogo? au ile kauli ya mkiandamana mtabadilishana majengo ya serikali yani Muhimbili Moi na kwenye ofisi za kova alafu unaambiwa demokrasia mara mimi sio dikteta..hivi ni vitisho ambavyo sisi watanzania tumevizoea na kuvivumilia mpaka wanakula wake za watu kwenye kampeni kama ilivokuwa igunga ila iko siku tutajikuta watanzania tunaambiwa na ccm wanaume wote leo kalindeni sungusungu mtuachie wake zenu ndani na ninadhani pia hilo tutalivumilia kama tunaweza kuibiwa, kutishiwa kupotezwa nk na watu tuliowapa dhamana wenyewe na tunavumilia tuendelee kuvumilia hivo hivo mpaka yesu arudi....
 
Ukisoma maneno yake hayo hapo juu yeye mwenyewe anaamini kuwa ni dikteta mkarimu (Benevolent dictator)... vinginevyo tusingekuwa huru hivi. Tumshukuru kwa kutupa uhuru wetu.

Kiukweli rhisi wetu ni dikteta la kutupwa. MMK ni sahihii kabisa kuwa yeye jk anajiona ni dikteta mkarimu, na hii aliidhihirisha pale alipodai kuwa ajaribu kuwa diktete kidogo.

Kwa definition ya jk udiktete ni ukatili na hata hilo analo na sasa linazidi kujionyesha, tuone nguvu nyingi zinzotumiwa na serikali yake dhidi ya wananchi wake, vifo vinavyosababishwa na serikali yake kwa wale ambao wanaonekana tishio kwake nk

Udikteta ni hali ya kulazimisha tendo na au mawazo kwa kuamini wewe/kikudi peke yako usahihi au kwa kulinda maslahi yako/yenu. Udikteta ukifika hatu ya juu kiuwezo kama kwa yeye kuwa rahisi au kwa kutishia maslahi husaidiwa na ukatili ili kuthibiti changa moto zake. jk anazungumzia ukatili na hivyo japo mengi ya ukatili yamefanyika yeye anaona hiyo haitoshi hivyo yeye kuwa dikteta mwnye huruma. Usemi wa Mwalimu kuwa ukianza kula nyama ya mtu huwezi acha ni wa kweli, ukila mmoja unaona ulistahili ule mia. Ninge penda kumuliza jk kama kuna dikteta aliyeamini kuwa ni dikteta hata kama wwatu wote duniani husema kuwa ni dikteta. Je unatofauti gani na na hao wasioamini.

Udikteata wa jk katika mwaka moja huu wa uongozi samahani wa utawala wake kwa kurudi nyuma (retrospective) na zilolizo muhimu (major). Kulazimisha sheria ya uundaji wa katiba,kwa kumlinda na kushindwa kuchukua hatua na labda kubariki na kushiriki kwa ufisadi wa Jairo, hatua alizochukua dhidi ya wenye mawazo na msimao tofauti na hasa mauaji ya watanzania wasio na hatia wala silaha katika sehemu mbali mbali za Tanzania, kuweka marafiki na watoto, mashemeji, washikaji na mahawara kwenye utendaji wa serikali, chaguzi mbalimbali kwa upendeleo wa chama chake, kuulinda na kuuhifadhi mfumo wa kidikteta kama tume ya uchaguzi nk, na muhimu alivyo chakachua urahisi wake wakati wa uchaguzi uliopita.

Kwa kuhitimisha jk ni dikteta kwelikweli
 
Sasa wewe unaetaliwa na Kikwete tukuiteje? mjanja?

Aaaaaaghrrr!
We bb umekuja kwa usafırı ganı tena?
Kumbe mods wanahongeka ee!
Umewapa nn wakakutoa kıfungonı sı ulıkataa dhamana?!
 
Aaaaaaghrrr!
We bb umekuja kwa usafırı ganı tena?
Kumbe mods wanahongeka ee!
Umewapa nn wakakutoa kıfungonı sı ulıkataa dhamana?!

Wanasheria wote waliomo JF basi nisimjuwe hata mmoja? unanchekesha!
 
ByFaizaFoxy:
Kwa nini basi raisiang'ang'anie kilakitu:
anaunda tume yakukusanya maoni
anawapa hadiduza rejea
anaundasecretariate
anaunda bunge lakatiba
anapewa maoniyaliyokusanywa
anaamua nini chakufanya baada yakupokea maoni
wanachi wanapigakura kamawanataka katiba:
tumeimechaguliwa naraisi
Kwani watuwengine na auvyombo vinginehaviwezi kufanyakazi hiyo? Mpakakazi zote afanyeyeye
Anayelipa mpulizafilimbi ndieyeanayechaguawimbo, tunauhakika gani kamaRais hatachaguawimbo anaoutakakatika mazingirayaliyotajwa hapojuu?
Maoni yoyote yawananchi kwamfumo wakulimbikiza kiasihiki hayawezikuonekana kuwa niyao
kila kitu rais
kupumua-rais
kukojoa rais
kusoma rais
hata kwenda hajakubwa-rais
KUMBE SOMETIMES FF ANATUMIA AKILI
NAONA UMEANZA KUFUNGUKA
 
Udikteta tumeuacha zamani, wakati unarundikwa ndani bila hata kujuwa lini utatoka, mpaka apende Nyerere.

Udikteta tumeuacha wakati gazeti ni Daily news na la chama.

Hivi ni nani anaopinga kuwa zama za Udikteta tumeshaondokana nazo huko, chama kilikuwa kimoja, magazeti anayotaka nyerere tu. Radio anazotaka nyerere tu. TV hakuna. Jela unafungwa kwa amri tu ya Nyerere, au unapotezwa na hujulikani umeenda wapi? Nani asiojuwa kisa cha kuadhiriwa Hanga uwanjani na Nyerere na hajaonekana tena baada ya hapo> kama si udikteta ni nini ule?

Faiza,
Hoja hapa ni kuwa jk hawezi kuwa dikteta hata kama angependa kuwa hivyo. Zamani sio leo, anachosema Mwanakijiji ni kuwa rais hawezi kuwa dikteta kidogo eti kwa sababu anataka kutufundisha kwa vitendo tofauti ya kuwa dikteta na kutokuwa. Ubavu huo kwa nyakati hizi haupo. Conclussion ni kwamba jk alichemka kwa matamshi hayo. Siku hizi wakubwa hawatishiwi nyau. Alianza kwa kuchekacheka sasa hivi anataka kuchimba mkwara, too late.
 
ByMzeeMwanakijiji:
Ooh ok,nimekupata.Kipengele gani chaKaitba hii ili huumjadala ufe kuwandivyo kinavyotakamchakato uwe?
MWANAKIJIJI NAVYO KUFAHAMU SIDHANI KAMA UMEFIKIA LEVEL YA KUBISHANA NA FF, NAONA UNAMJENGEA JINA TU. INSHORT JAMAA NI MWEUPE KICHWANI.
 
Tafadhali sana wacha kuchakachuwa jina langu kwenye post yako. Hayo uliyoyabandikia jina langu si maneno yangu naomba post # ngapi kama u mkweli.

Tafadhali moderators, mtu anafikia kuchakachuwa maneno ya watu na kubandika jina kwenye post ambayo si yangu na bado mnamuwachia. Nini hii? Tazameni huyu ntamaholo alivyochakachuwa post #103 na kuya "quote" hayo maandiko na kuyawekea jina langu. Tafadhali naomba haki itendeke.

Huu ni ukosefu wa ustaarabu wa hali ya juu na nnatumai moderators mtachukuwa hatua kali kwa watu kama hawa.
Acha kulia lia mama.
Huyu mzee hapa ndo kiboko yako tu!!
mail
 
mimi nilishuhudia rais anadanganya eti cdm waliahidi katiba ndani ya siku mia, aibu kweli
 
Tunashukuru mwanakijiji kwa kuliona hilo na kuliweka hewani. Hapa ndio ninapo waonea huruma wale watu wanaosema wanahitaji huruma ya Rais, matokeo yake tunapata mambo ya akina Jairo, upumbavu mtupu. Labda aseme anaotaka kuwa ondolea uhuru ni akina Jairo wanaoivuruga Tanzania kwa kutumia kodi za wananchi kwenda kucheza Disco Dodoma.
 
Back
Top Bottom