Kwanza sikujua kwamba hii thread niiweka wapi, watakaokereka wanisamehe
ataka ukahaba uhalalishwe
Diwani wa Kata ya Makuburi jijini Dar es Salaam, Busee Gabbas, ameitaka Serikali na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, kuhalalisha biashara ya ukahaba ili kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi pamoja na kuongeza mapato la taifa.
Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitoa mchango wake kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Wilaya ya Kinondoni, lililokutana kwa lengo la kuangalia matatizo na mafanikio ya miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema kinachotakiwa kwa serikali ni kuhahalalisha biashara hiyo na kutenga maeneo maalumu ambayo makahaba watakuwa wakiyatumia kwa biashara zao kwa uhakika.
Alisema pia kutengwa kwa maeneo ya kufanyia biashara hiyo,
kutawawezesha wateja kujua sehemu ya kupata huduma hiyo bila kificho, tofauti na ilivyo sasa.
Alisema kitendo cha kuzuia biashara hiyo, kunaigharimu serikali fedha nyingi kufanya misako kwa watu wanaojihusisha na biashara hiyo na kusababisha ongezeko la maambukizi ya ukimwi.
Ni wakati muafaka kwa halmashauri yetu na Serikali kuhalalisha ukahaba ili tuweze kujiongezea mapato lakini pia kutasaidia kupunguza maambukizi ya ukimwi, alisema Gabbas.
Alisema kuruhusu ukahaba si jambo geni kwani mataifa yaliyoendelea, yanafanya hivyo kwa kuitambua na kutenga maeneo maalum lakini pia hujipatia kipato kutokana na kukusanya kodi kutoka kwa makahaba.
Alisema halmashauri inapaswa iwape leseni ya kufanya biashara watu wenye nia ya kufanya biashara hiyo na yenyewe ijuhusishe katika kukusanya mapato.
Alisema askari au mgambo wanapofanya msako wa makahaba
wanatumia fedha nyingi za walipa kodi ambazo zingeweza kutumika katika shughuli nyingine za maendeleo kama biashara hiyo itaruhusiwa.
Si siri kuwa tunapoteza fedha nyingi katika misako ya makahaba ila hali tungeruhusu tungepata fedha badala ya kutoa, alisema Gabbas.
ataka ukahaba uhalalishwe
Diwani wa Kata ya Makuburi jijini Dar es Salaam, Busee Gabbas, ameitaka Serikali na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, kuhalalisha biashara ya ukahaba ili kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi pamoja na kuongeza mapato la taifa.
Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitoa mchango wake kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Wilaya ya Kinondoni, lililokutana kwa lengo la kuangalia matatizo na mafanikio ya miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema kinachotakiwa kwa serikali ni kuhahalalisha biashara hiyo na kutenga maeneo maalumu ambayo makahaba watakuwa wakiyatumia kwa biashara zao kwa uhakika.
Alisema pia kutengwa kwa maeneo ya kufanyia biashara hiyo,
kutawawezesha wateja kujua sehemu ya kupata huduma hiyo bila kificho, tofauti na ilivyo sasa.
Alisema kitendo cha kuzuia biashara hiyo, kunaigharimu serikali fedha nyingi kufanya misako kwa watu wanaojihusisha na biashara hiyo na kusababisha ongezeko la maambukizi ya ukimwi.
Ni wakati muafaka kwa halmashauri yetu na Serikali kuhalalisha ukahaba ili tuweze kujiongezea mapato lakini pia kutasaidia kupunguza maambukizi ya ukimwi, alisema Gabbas.
Alisema kuruhusu ukahaba si jambo geni kwani mataifa yaliyoendelea, yanafanya hivyo kwa kuitambua na kutenga maeneo maalum lakini pia hujipatia kipato kutokana na kukusanya kodi kutoka kwa makahaba.
Alisema halmashauri inapaswa iwape leseni ya kufanya biashara watu wenye nia ya kufanya biashara hiyo na yenyewe ijuhusishe katika kukusanya mapato.
Alisema askari au mgambo wanapofanya msako wa makahaba
wanatumia fedha nyingi za walipa kodi ambazo zingeweza kutumika katika shughuli nyingine za maendeleo kama biashara hiyo itaruhusiwa.
Si siri kuwa tunapoteza fedha nyingi katika misako ya makahaba ila hali tungeruhusu tungepata fedha badala ya kutoa, alisema Gabbas.