maringomashaka
Member
- May 22, 2011
- 16
- 8
In vitro fertilisation (IVF)
Hii ni njia ambayo inatumika kupata mimba kwa wanandoa ambao wanamatatizo ya uzazi. Mara nyingi tatizo linakuwa kwa mwanamke hasa anayekuwa na tatizo la kuziba kwa mirija hasa yote miwili na kushindwa kuruhusu mbegu za kiume kupita ili zikakutane na yai lililopevuka kwa ajili ya kuchavusha mayai. Kwa ufupi kinachofanyika ni kwamba mayai ya mwanamke yanachukuliwa kutoka kwenye mfuko wa uzazi yanapokuwa yamekwisha komaa kwenye hatua yakuweza kuchavushwa na kutunga mimba pindi yanapokutana na mbegu za kiume. Mbegu za mwanaume zinakusanywa pia na kuchanganywa pamoja na mayai haya katika maabara maalumu kwenye chombo maalam ili mayai yaweze kuchavushwa. Baada ya sku kuanzia tatu hadi tano mayai yanakuwa yamechavushwa na kutengeneza mimba changa (zygote) ambayo inapandikizwa katika mfuko wa uzazi wa mwanamke na kuruhusiwa kukua kama mimba ya kawaida.
Utafiti wangu usio wa kisayansi kuhusu uhalali wa njia hii katika misingi ya dini kadhaa hapa nyumbani ikiwa dini mbili kubwa za Kikristu na Kiislam umebainisha kuruhusiwa kwa njia hii kutokana na dharura ya maradhi ya matatizo ya uzazi, kwahiyo haina shaka kuwa ni njia mbadala kama njia ya kawaida ya kupata watoto imeshindikana. Hii inakubalika tu kama wawili hao ni wanandoa, hii ni kwa mtazamo wa kidini zaidi ila ni halali hata kama wawaili hawa hawakufunga ndoa kwakuwa kwa wenzetu wa Magharibi mwanamke anaweza kwenda kununua mbegu kutoka kwenye benki ya mbegu na kupandikizwa.
Kutokana na maendeleo ya kisayansi na teknologia hivi saa, mbegu za mwanaume zinaweza zikahifadhiwa kwenye maabara maalam (sperm bank) na kutumika miaka kadhaa ijayo na kutengeneza mimba.
SWALI:
Chukulia mume amefariki na ameacha mbegu zake za kiume kwenye benki maalamu ya kuhifadhi mbegu za kiume (sperm bank). Baada ya miaka kadhaa ya kifo chake iwe mwaka mmoja au na zaidi mwanamke ameamua azae kwakutumia mbegu za marehemu mume wake, na akafanya hivyo na akafanikiwa kushika mimba na hatimae kuzaa
1.) Kwa mitazamo ya kidini hususani dini hizi zetu mbili (Ukristo na Uislam) je mtoto atakubalika uwa amezaliwa ndani ya ndoa, kutokana na jibu lako ni kwanini iwe hivyo? Kuna maandiko yeyote yaliyojaribu kugusia juu ya hili?
2.). Kwa mtazamo wa kimaadili ya jamii ya Kitanzania, mila na desturi zetu, je kuna uhalali wowote wa mwanamke kutumia mbegu za marehemu mumewe miaka kadhaa baada ya kifo chake? Jamii itaipokeaje? Je kama ni mke wa mtoto wako utaruhusu hilo lifanyoke
3) Kwakuwa Dunia ina badilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknologia na kwakuwa sisi tunaishi kwenye Dunia ya uhalisia, je wewe unashauri nini juu ya hili kwa jamii na viongozi wa dini kwakuwa ukweli ni kwamba haya yametokea, yanatokea na yataendelea kutokea na ni hali halisi tunayoishi nayo kama si wewe, basi ndugu yako wa karibu, rafiki au mwanajamii.
Note: Naomba mchango wenu wa kisayansi, kidini na kijamii juu ya hili. Mawazo yote ni mawazo muhimu na yanaheshimika na kupewa umuhimu sawa kwani hakuna mawazo ya Kipumbavu. Karibuni jamvini.
Hii ni njia ambayo inatumika kupata mimba kwa wanandoa ambao wanamatatizo ya uzazi. Mara nyingi tatizo linakuwa kwa mwanamke hasa anayekuwa na tatizo la kuziba kwa mirija hasa yote miwili na kushindwa kuruhusu mbegu za kiume kupita ili zikakutane na yai lililopevuka kwa ajili ya kuchavusha mayai. Kwa ufupi kinachofanyika ni kwamba mayai ya mwanamke yanachukuliwa kutoka kwenye mfuko wa uzazi yanapokuwa yamekwisha komaa kwenye hatua yakuweza kuchavushwa na kutunga mimba pindi yanapokutana na mbegu za kiume. Mbegu za mwanaume zinakusanywa pia na kuchanganywa pamoja na mayai haya katika maabara maalumu kwenye chombo maalam ili mayai yaweze kuchavushwa. Baada ya sku kuanzia tatu hadi tano mayai yanakuwa yamechavushwa na kutengeneza mimba changa (zygote) ambayo inapandikizwa katika mfuko wa uzazi wa mwanamke na kuruhusiwa kukua kama mimba ya kawaida.
Utafiti wangu usio wa kisayansi kuhusu uhalali wa njia hii katika misingi ya dini kadhaa hapa nyumbani ikiwa dini mbili kubwa za Kikristu na Kiislam umebainisha kuruhusiwa kwa njia hii kutokana na dharura ya maradhi ya matatizo ya uzazi, kwahiyo haina shaka kuwa ni njia mbadala kama njia ya kawaida ya kupata watoto imeshindikana. Hii inakubalika tu kama wawili hao ni wanandoa, hii ni kwa mtazamo wa kidini zaidi ila ni halali hata kama wawaili hawa hawakufunga ndoa kwakuwa kwa wenzetu wa Magharibi mwanamke anaweza kwenda kununua mbegu kutoka kwenye benki ya mbegu na kupandikizwa.
Kutokana na maendeleo ya kisayansi na teknologia hivi saa, mbegu za mwanaume zinaweza zikahifadhiwa kwenye maabara maalam (sperm bank) na kutumika miaka kadhaa ijayo na kutengeneza mimba.
SWALI:
Chukulia mume amefariki na ameacha mbegu zake za kiume kwenye benki maalamu ya kuhifadhi mbegu za kiume (sperm bank). Baada ya miaka kadhaa ya kifo chake iwe mwaka mmoja au na zaidi mwanamke ameamua azae kwakutumia mbegu za marehemu mume wake, na akafanya hivyo na akafanikiwa kushika mimba na hatimae kuzaa
1.) Kwa mitazamo ya kidini hususani dini hizi zetu mbili (Ukristo na Uislam) je mtoto atakubalika uwa amezaliwa ndani ya ndoa, kutokana na jibu lako ni kwanini iwe hivyo? Kuna maandiko yeyote yaliyojaribu kugusia juu ya hili?
2.). Kwa mtazamo wa kimaadili ya jamii ya Kitanzania, mila na desturi zetu, je kuna uhalali wowote wa mwanamke kutumia mbegu za marehemu mumewe miaka kadhaa baada ya kifo chake? Jamii itaipokeaje? Je kama ni mke wa mtoto wako utaruhusu hilo lifanyoke
3) Kwakuwa Dunia ina badilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknologia na kwakuwa sisi tunaishi kwenye Dunia ya uhalisia, je wewe unashauri nini juu ya hili kwa jamii na viongozi wa dini kwakuwa ukweli ni kwamba haya yametokea, yanatokea na yataendelea kutokea na ni hali halisi tunayoishi nayo kama si wewe, basi ndugu yako wa karibu, rafiki au mwanajamii.
Note: Naomba mchango wenu wa kisayansi, kidini na kijamii juu ya hili. Mawazo yote ni mawazo muhimu na yanaheshimika na kupewa umuhimu sawa kwani hakuna mawazo ya Kipumbavu. Karibuni jamvini.