Ugonjwa wa Pumu (Bronchial Asthma): Chanzo, dalili na tiba

Hata Mimi nasikia dawa za miti shamba zinatibu, tusubiri kama atakuwepo mwenye kujua atusaidie maana ni kwa faida ya wengi.
 
Hakuna mtishamba uliothibitika kutibu pumu(asthma).kama kweli ni pumu ajaribu kuepuka vichochezi mfano vumbi,baridi,harufu kali(paints)
 
Mimi ni mdau wa afya...kwa taaluma yangu nafahamu kuwa hakuna tiba ya Pumu (kwamba haitibiki ikakoma isitokee tena). Pumu inafanana na allergy jinsi inavyotokea, kunakuwa na kianzishi (allergen/trigger) halafu njia ya hewa ina'respond' kwa kubana haswa wakati wa kutoa hewa nje. Kikohozi na mafua ni moja ya vianzishi. Wakati mwingine Pumu inaweza ikaacha yenyewe (hasa inayoanzia utotoni) lakini sio mara zote.

Dawa zilizopo sasa na kupatikana hospitali au madukani husimamisha 'attack' inapotokea kwa kupanua njia za hewa ili mgonjwa apumue kawaida, hazitibu kuponyesha tatizo moja kwa moja.

Sijasikia bado dawa ya kienyeji iliyothibitishwa kuwa inapunguza kutokea kwa pumu au kutibu pumu kabisa. Kwa maelezo zaidi unaweza kwenda Muhimbili kitengo cha dawa asilia watakufahamisha.

Thanx mdau na wote mliochangia.
Unajua mitaani kuna mengi, eti wanadai kunadawa ya kutapisha na athma inakwisha kabisa
 
pumu ya mtoto mara nyingi huisha yenyewe pia niliwahi kusikia kuna dawa ya miti shamba!cha msingi tafuta kichocheo cha yeye kubanwa na kukiondoa pia kuendelea kumwelimisha mtoto mazingira ambayo yatamsababishia kubanwa then pumu itakuwa historia kwake!kila la kheri mkuu
 
Before cjakupa ushauri zaidi kwa sasa anatumia dawa gani? Je ana umri gani? I have two asthmatic kids so i have little advice for you.

Pole sana.
 
Before cjakupa ushauri zaidi kwa sasa anatumia dawa gani? Je ana umri gani? I have two asthmatic kids so i have little advice for you.

Pole sana.

Ana miaka mitatu, mwanzoni kabla ya kujua alikua akibanwa tunaenda hospital daktari akimcheki anasema nimonia anamuandikia kristapeni sindano za masaa,nadhani unajua zinavyouma, amechoma sana hadi makalio yana vinundu kwa ndani.
Baada ya kujua sasa akibanwa anaandikiwa salbutamol syrap inamsaidia sana.
 
Magome ya msufi achemshiwe na kupewa kwa siku zaidi ya mara mbili. (anywe kama anavyokunywa maji haina madhara) na atapona kabisa kama ni mtoto hata kama inasababishwa na mzio. Kwa mtu mzima inapunguza tu kasi ya shambulizi.
 
ana miaka mitatu, mwanzoni kabla ya kujua alikua akibanwa tunaenda hospital daktari akimcheki anasema nimonia anamuandikia kristapeni sindano za masaa,nadhani unajua zinavyouma, amechoma sana hadi makalio yana vinundu kwa ndani.
Baada ya kujua sasa akibanwa anaandikiwa salbutamol syrap inamsaidia sana.

Well, poleni sana.

Salbutamol ni nzuri kama itabidi inabid aanze kutumia inhalers. Watoto wangu walianza kutumia inhalers walipokua na miezi tisa. Yao ni mbaya sana huwa wanabanwa mpaka wanawekwa kwenye nebulizer. Ni beta umcheki dr,kama upo dar naweza kukuelekeza dr mzuri sana.

Kitu kingine kilichowasaidia watoto ni dawa ya pumu nilinunua pale muhimbili tradition clinic. Tangu walipotumia imepunguza frequency of attacks.

Halafu mjitahidi sana kuondoa vumbi la ndani ya nyumba, mapazia, vitanda, matres iwe covered na kitu ya plastic kuzuia vumbi. Manukato kwenye sabuni,mafuta,dawa za kudekia, air freshner, perfumes. Angalieni vyakula anavyokula unaweza kuta vina allergens
 
magome ya msufi achemshiwe na kupewa kwa siku zaidi ya mara mbili. (anywe kama anavyokunywa maji haina madhara) na atapona kabisa kama ni mtoto hata kama inasababishwa na mzio. Kwa mtu mzima inapunguza tu kasi ya shambulizi

Noted.
Hivi dar misufi inapatikana kweli?
 
well,poleni sana.

Salbutamol ni nzuri kama itabidi inabid aanze kutumia inhalers. Watoto wangu walianza kutumia inhalers walipokua na miezi tisa. Yao ni mbaya sana huwa wanabanwa mpaka wanawekwa kwenye nebulizer. Ni beta umcheki dr,kama upo dar naweza kukuelekeza dr mzuri sana.

Kitu kingine kilichowasaidia watoto ni dawa ya pumu nilinunua pale muhimbili tradition clinic. Tangu walipotumia imepunguza frequency of attacks.

Halafu mjitahidi sana kuondoa vumbi la ndani ya nyumba,mapazia,vitanda,matres iwe covered na kitu ya plastic kuzuia vumbi. Manukato kwenye sabuni,mafuta,dawa za kudekia,air freshner,perfumes.angalieni vyakula anavyokula unaweza kuta vina allergens

Mkuu kwanza nakushukuru sana kwa ushauri wako ulionipa through experience ya watoto wako, pole sana naamini Mungu atawasimamia daima.

Mimi naishi Dar hivyo naomba unielekeze kwa huyo dr kwani naamini atamsaidia pia.

Wazo la kwenda muhimbili tradition clinic nimelipenda pia lakini nadhani nianze na huyo dr kwanza.

Thanx again bro
 
Kuna bibi mmoja anaitwa bi mbaazi,alitibu pumu yangu nilivyokuwa mdogo,sasahivi sina tena pumu,kuna maji(sijui ya nini) anakupa kwenye chupa unakunywa mara tatu kwa siku,anaweza kukaa miaka bila ya kupata tena pumu, au isirudi kabisa.

I'm almost 30 and at that time i was between 10 and 14 years old.

Sijui sasavhivi anaishi wapi, ila mara ya mwisho kumuona ni kwenye michezo ya kuigiza ya mzee janguo,mtafute mzee janguo akwambie huyo bibi anapatikana wapi. nakwambia hivi kwasababu aliitibu pumu yangu.
 
Nilitumia sana salbutamol, ni nzuri sana kwa kutuliza tu, tena zinatuliza haraka sana, ila haziponyi pumu,mpaka dakika hii ninapoandika siamini kwamba pumu yangu iliisha, kwahiyo pembeni ya kitanda changu kuna pakti ya salbutamol, na popote ninaposafiri lazima nibebe salbutamol in case of anything nisipate kuwasumbua watu.
 
kuna bibi mmoja anaitwa bi mbaazi,alitibu pumu yangu nilivyokuwa mdogo,sasahivi sina tena pumu,kuna maji(sijui ya nini) anakupa kwenye chupa unakunywa mara tatu kwa siku,anaweza kukaa miaka bila ya kupata tena pumu, au isirudi kabisa.

I'm almost 30 and at that time i was between 10 and 14 years old.

sijui sasahivi anaishi wapi, ila mara ya mwisho kumuona ni kwenye michezo ya kuigiza ya mzee janguo,mtafute mzee janguo akwambie huyo bibi anapatikana wapi. nakwambia hivi kwasababu aliitibu pumu yangu

Mzuanda maaelezo yako yametia matumaini sana ndungu yangu kuwa siku moja atapona.

Nikikwama kabisa ipo siku ntamtafuta, nime note sehemu.

Thanx
 
Noted.
Hivi dar misufi inapatikana kweli?
nadhani kuna misufi miwili mitatu maeneo ya Kinondoni, na pia maeneo ya ukonga ipo. lakini mingi zaidi ilikuwa maeneo ya Kawe na Lugalo humo kama bado imo sijui unafanyaje!!!Pia pale karibu na Drive-in cimena zamani sijui siku hizi pana jina gani vile!? (Yale maji wanayopewa watu na wakapona na kupata nafuu kubwa - ndio hiyo dawa yenyewe ila huwa wanaifanya siri ili biashara iendelee) Akishapona mwanao nawe wasaidie wengine mkuu.
 
Wadau naombeni mawazo yenu nina mtoto wa dada yangu anasumbuliwa sana na kifua, haipiti miezi miwili lazima atabanwa na kifua sana.

Baada ya uchunguzi ikaja gundulika baba yake anamatatizo ya pumu na kwakuwa ugojwa huu ni wa kurithi, basi amemuachia na mwanae.
Katika harakati za matibabu kuna nesi akamwambia sister pumu kwa hospitali haina dawa ila kuna mitishamba yaani dawa za kienyeji zinaponesha pumu na hasa akiwa bado mdogo.

Je, kuna yeyote mwenye experiance na hili au amewahi sikia tufahamishane.
Nawasilisha.

Yupo DR mmoja anatibu pumu kwa kutumia dawa za kisasa na inapona kabisa nimeshuhudia watu wengi wakipona.
 
Mimi mwenyewe nina pumu mpaka kesho niliangaika sana wakati nipo bongo maana ilikuwa inanishika mara kwa mara na mimi zaidi joto ndio lilikuwa linanisumbua maana kama ndani kukiwa na joto kinabana sana sasa hapo inabidi nitoke nilale nje nikitoka tu kwenda kulala nje after 30mins kinakata...Kitu kingine ambacho kilikuwa kinanisumbua ni mafuta ya mawese labda mtu akiwa anapika nikipata tu ule moshi hali inakuwa mbaya sana na vumbi pia....ila huku nilipo kuna hali ya baridi ila mpaka sasa nimekamatwa na pumu mara 2 tu toka nifike...so inategemea....
 
Ndugu inatibika,

I used to be asthmatic...Ilinitesa sana nilipokuwa mdogo, sindano za masaa, vidonge vile vya salbutamol, kukosa shule..afu baadae nilipokua kidogo zikaja hizi inhalers. Zilisadia wen i had an attack..lakini hazikuponyesha!

Siku moja rafiki yangu (tukiwa form 5 majengo sec. Moshi)akaniambia wewe na hizo dawa si utakuwa addict? akanipa stori ya brother ake alikuwa na pumu na hakutumia dawa yeyote!

The only thing alifanya ni kwenda gym, mazoezi ya kufa mtu na sasa ivi u will neva believe, amepona. So, nikasema y nt giv it a try maana mi nlichoka enzi izo unapiga PCM afu unashindwa kwenda shule, inauma!

Nikaingia gym, palepale maeneo ya Majengo kila siku..mdgomdogo (samtymz unakata tamaa), weekends naenda kukimbia au kucheza mpira uwanja wa ushirika (now MUCCoBS)..na bado kifua kilikua kinabana. But hata sijui nisemeje, after sometime, nilijikuta tu kimeacha! since then..trust me..sijapatwa attack yoyote na sijaacha mazoezi!

Observation:
Watoto wengi wenye pumu wanakuwa reserved and antisocial..hali hiyo inawafanya wasiparticipate in sporting and other extracurricular activities. Little do they know that their chests need the exercise to expand. So, kwa ushauri tu, hakikisha wanao wanafanya mazoezi frequently..wasiogope kupata ataack because in the long itaisha.

Hakikisha hawawi addicted!!! please!!! Nilipata wanafunzi wawili nilipoenda chuoni, yani wao wakipanda ngazi floor moja tu wanapuliza kale kakitu..mpaka nikawaonea huruma. but wao walikuwa beyond help! don't let your kid reach that stage..It can be controlled.
One last thing, check on their diet..more fat means more attacks!
Thanks.

***Above all, hakikisha unawaombea sana kwa Mungu maana yeye anaweza yote!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom