Ugonjwa wa malaria sasa wapata chanjo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,316
33,125


malaria-mbu.jpg
Boniface Meena
WANASAYANSI nchini wako katika hatua za mwisho kukamilisha kinga ya ugonjwa wa malaria baada ya utafiti kuonyesha kuwa chanjo mpya iitwayo RTS,S ambayo inaweza kukinga ugonjwa huo kwa asilimia 50.

Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Afya Ifakara, Dk Salim Abdulla alipokuwa akizungumza katika warsha kuhusu matokeo ya utafiti wa chanjo hiyo.

Dk Abdulla alisema utafiti huo pia umeonyesha kuwa chanjo hiyo mpya inaweza kuwakinga watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano na kinamama wajawazito kwa asilimia 47.

“Tuko katika awamu ya tatu ya utafiti huo na hali inaonyesha kuwa chanjo hiyo ni salama,” alisema Dk Abdulla.

Dk Abdulla alisema kuwa utafiti huo umefanyika katika maeneo mawili nchini; Korogwe mkoani Tanga na Bagamoyo, Pwani. Majaribio ya utafiti huo yalihusisha watoto 3,300.

“Taratibu zilizotumika zilikuwa sawa na watoto walioshiriki walipata huduma bora zaidi na kulikuwa na uchache wa vifo tofauti na tafiti nyingine,” alisema Dk Abdulla.

Alisema kuwa chanjo hiyo pia inaweza kupunguza maambukizi ya malaria kali kwa asilimia 47 na kwa asimilia hiyohiyo kwa malaria ya kawaida.

“Mtoto akipata chanjo hii au mama mjamzito anaweza kupata kinga ya kutokupata malaria,” alisema.

Alisema watoto waliotumika katika utafiti huo walikuwa wakiangaliwa afya zao kwa asilimia 99.9 ili kufanikisha matokeo ya chanjo hiyo.

Alisema awamu hiyo ya tatu ya utafiti wa chanjo hiyo ni ya mwisho kabla dawa kuanza kusambazwa nchini kwa ajili ya matumizi.

Awali, akifungua warsha hiyo, Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando alisema wajibu mkubwa wa Serikali katika kupambana na malaria ni kuhakikisha upatikanaji wa kutosha wa huduma zote za kinga na tiba.

“Ugonjwa wa malaria unaweza kukingwa na mojawapo ya njia madhubuti ni kutumia chanjo,” alisema Dk Mmbando.

Alisema takwimu kutoka vituo vya huduma za afya nchini zinabainisha kuwa takribani watu 20,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na ugonjwa wa malaria na wengi wanaofariki ni watoto walio chini ya umri wa miaka mitano na kina mama wajawazito.

“Hata hivyo, utafiti unaonyesha kuwa asilimia 60 hadi 80 ya vifo hutokea nyumbani kabla ya wagonjwa kufikishwa katika vituo vya afya, hivyo idadi halisi ya vifo vinavyotokana na malaria ni zaidi ya 80,000 kila mwaka,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo ni dhahiri kuwa chanjo hiyo mpya imekuja wakati mwafaka na itasaidia kukabiliana na tatizo hilo sugu na kuutokomeza kabisa ugonjwa wa malaria.

Dk Mmbando alisema upatikanaji wa chanjo hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kupambana na malaria, ugonjwa unaoongoza kwa kusababisha vifo nchini.

“Hatuna sababu ya ugonjwa wa malaria kuendelea kututesa na kudhoofisha maendeleo ya nchi yetu. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kupambana na malaria katika nafasi yake.”

Alisema pamoja na upatikanaji wa kinga hiyo, bado njia zilizokuwa zikitumika kukabiliana na malaria zitaendelea kutumika.


Chanzo: Ugonjwa wa malaria sasa wapata chanjo
 
  • a2cd7d236e6af217fb0e6a7067004ade.jpg

n this 2005 photo made available by the University of Notre Dame via the CDC, an Anopheles funestus mosquito takes a blood meal from a human host. The quest for the world's first malaria vaccine appears to have taken a big step. The first results from a late-stage test in seven African countries were released Tuesday, Oct. 18, 2011. They show the experimental shots cut the number of cases of malaria in half in young children. In Africa, the ...

Health140520110713286-1.jpg


A bug which kills the malaria parasite has been discovered living in mosquitoes

photo_1319009599527-1-0.jpg



Un técnico de laboratorio prepara unas muestras de sangre de unos voluntarios el 30 de octubre de 2009 en un instituto de Bagamoyo, en Tanzanian, en el marco de una fase de prueba de una vacuna contra la malaria.



2011-10-18T023912Z_01_NOOTR_RTRMDNP_2_India-599484-1-pic0.jpg





  • In this 2005 photo made available by the University of Notre Dame via the CDC, an Anopheles funestus mosquito takes a blood meal from a human host. The quest for the world's first malaria vaccine appears to have taken a big step. The first results from a late-stage test in seven African countries were released Tuesday, Oct. 18, 2011. They show the experimental shots cut the number of cases of malaria in half in young children. In Africa, the ... more

2011-10-19T061848Z_01_NOOTR_RTRMDNP_2_India-599767-1-pic0.jpg






  • Billionaire philanthropist Bill Gates speaks at the Global Alliance for Vaccines and Immunisation (GAVI) conference in London June 13, 2011. REUTERS/Paul Hackett/Files


  • 000_Par6222886.jpg

An exhibition displays mosquito nets in Paris in April 2011 as part as events organised for the 4th World Malaria Day. Nearly a third of all nations in which malaria is endemic are working to eliminate the disease within a decade, according to a new report released Monday in the United States. (AFP Photo/Pierre Verdy)




4096496w.jpg




  • In this 2005 photo made available by the University of Notre Dame via the CDC, an Anopheles funestus mosquito takes a blood meal from a human host. The quest for the world's first malaria vaccine appears to have taken a big step. The first results from a late-stage test in seven African countries were released Tuesday, Oct. 18, 2011. They show the experimental shots cut the number of cases of malaria in half in young children. In Africa, the ... more
    e64d4e9d592fd717fb0e6a7067000ccc.jpg
TO GO WITH ENFERMEDADES CRONICAS - FILE - In this Sept. 7, 2011 file photo, patients who had experienced heart attacks rest on beds while being held under observation in the emergency room of a heart hospital in Beijing, China. Heart disease, cancer, and respiratory disease have replaced hepatitis, diarrhea and malaria as desk work replaces farming, cars replace bicycles, and smoking remains stubbornly popular. (AP Photo/Alexander F. Yuan, File)



2011-08-18T193736Z_01_NOOTR_RTRMDNP_2_India-588538-1-pic0.jpg



A street vendor selling mosquito net tents, rests in one as he waits for customers in Ghaziabad, Uttar Pradesh April 15, 2011. REUTERS/Parivartan Sharma/Files




A child is given an injection as part of a malaria vaccine trial at a clinic in the Kenya coastal town of Kilifi, November 23, 2010. REUTERS/Joseph Okanga


2011-10-18T171926Z_01_BTRE79H1C4H00_RTROPTP_2_LEONE-MALARIA.JPG



A boy inside a mosquito net in a mud hut in Mallay village, southern Sierra Leone, April 8, 2008. REUTERS/Katrina Manson







  • 000_Par2495637.jpg
A south Sudanese woman lays on a bed in 2009, at a health clinic in Terekeka, 51 miles north of Juba, where the population is exposed to malaria. A vaccine against malaria has been shown to reduce African children's risk of acquiring the disease by about half, according to the first results of an ongoing phase III trial released Tuesday. (AFP Photo/Tony Karumba)


HUYU MDUDU MBU NI KIBOKO YA WANADAMU KWELI ANAUWA ILE MBAYA YAKE.

WANADAMU WANATENGENEZA SILAHA KUUWANA WENYEWE KWA WENYEWE LAKINI WANASHINDWA NA HUYU MDUDU MBU MDOGO ALIYEUMBWA NA MWENYEEZI MUNGU AMA KWELI KAZI IPO HAPO.



 
Back
Top Bottom