Ugonjwa wa homa ya matumbo (Typhoid) na tiba mbadala

Zion Daughter

JF-Expert Member
Jul 9, 2009
8,921
4,235
Kwa yeyote anayejua tiba mbadala ya typhoid please naomba msaada.Nikisema mbadala namaanisha matunda,mizizi,mimea ama vyakula.

Bwana Yesu asifiwe.

===============

Homa ya matumbo

Homa ya matumbo husababishwa na bakteria anayeitwa Salmonella Typhi. Ugonjwa huu huambukizwa kwa mtu kula au kunywa chakula au maji yalio na kinyesi cha mu aliyambukizwa.[SUP][1][/SUP] Bakteria hawa hutoboa na kunyonya chakula kwenye matumbo ya binadamu.

Dalili

  • Homa kali
  • Kutoka kwa majasho mengi
  • Kuharisha (bila ya kutoa damu)
  • Mara nyingine, vitone vyekundu huonekana kwenye mwili.
Kwa kawaida, homa ya matumbo isipotibiwa hugawanyika katika hatua nne, kila hatua ikichukua takriban wiki moja.
Katika wiki ya kwanza:

  • Joto la mwili huongezeka
  • Kichwa huuma
  • Kukohoa
  • Damu kutoka kwa pua, ingawa tukio hili huwa ni nadra kutokea.
  • Maumivu ya tumbo pia huweza kutokea
Katika wiki ya pili:

  • Homa huongezeka
  • Mgonjwa huanza kupagawa, kama mwenda wazimu
  • Vitone vyekundu huanza kutokea kwenye kifua
  • Mgonjwa huharisha, takriban mara sita au nane kwa siku.
  • Kutapika kwa mgonjwa
  • Ini la mgonjwa huvimba
  • Homa ya mgonjwa huongezeka katika wakati wa alasiri kwenye wiki ya kwanza na ya pili.
Wiki ya tatu:

  • Matumbo hutoa damu.
  • Matumbo hutoboka
Wiki ya tatu ikimalizika, homa huanza`kutilia. Hii huendelea hadi wiki ya nne.
Matibabu

Mara nyingi, homa ya matumbo haiuwi binadamu. Dawa kama ampicillin, chloramphenicol, trimethoprim-sulfamethoxazole, Amoxicillin and ciprofloxacin hutumika kutibu wagonjwa katika nchi zilizoendelea.

Hatua za kuzuia kupata homa hii



Daktari akimpa mtu chanjo mjini San Augustine County, Texas




  • Usafi wa mazingara na wa kibinafsi ni hatua bora ya kujikina kutokamana na ugonjwa huu.
  • Homa ya matumbo haiathiri wanyama kwa hivyo maambukizi ni kutoka kwa binadamu mmoja hadi mwingine.
  • Homa hii hueza kuenea kwenye mazingara ambayo kinyesi cha binadamu hutangamana na vyakula vyao. Upishi wa makini na uoshaji mikono ni kingo bora zaidi kwa kuzuia maradhi haya kuenea.
  • Chanjo ni za aina mbili: moja inayotiwa kwa njia ya mdomo iitwayo Ty21a (au Vivotif Berna) na nyingine ya sindano kwa majinaTyphim Viiliyotengenezwa na Sanofi Pasteur au Typherix iliyotengenezwa na GlaxoSmithKline.
Historia

Mnamo mwaka 2004-05, janga la homa ya matumbo lilizuka katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliyoathiri watu 42,000 na kuuwa watu 214 (kulingana na ripoti ya shirika la World Health Organisation).

Waathiriwa maarufu


  • Mary Mallon, aliyejulikana kama Typhoid Mary.
  • Louisa May Alcott, mwandishi wa Little Women.
  • Charles Darwin, mwanasayansi, aliathirika pindi alipoenda nchini Chile mnamo 1835.
  • Eugenia Tadolini, alikufa mjini Paris mnamo 1872.
  • William Wallace Lincoln, mtoto wa tatu wa Abraham Lincoln, ambaye ni rais wa 16 wa Marekani, pamoja na Mary Todd Lincoln, walifariki kutokana na maradhi haya mnamo February 20, 1862.
  • Wilbur Wright, alikufa mnamo May 30, 1912 baada ya kuugua homa hii.
 
Mimi pia nshatafuta iyo mizizi kwakweli,dawa za hospitali mateso matupu na usugu juu...kuna dawa inaitwa maghakaa (kisukuma)sijui kutamka, eti inatibu magonjwa mbalimbali na malaria juu.seriously me naumwa sana malaria na tumbo

jamani dr ndindi sijui yule wa startv nae vipi??
 
acha masihala bwana...
mimi pia nshatafuta iyo mizizi kwakweli,dawa za hospitali mateso matupu na usugu juu...kuna dawa inaitwa maghakaa (kisukuma)sijui kutamka, eti inatibu magonjwa mbalimbali na malaria juu.seriously me naumwa sana malaria na tumbo

jamani dr ndindi sijui yule wa startv nae vipi??

Dr Ndodi ana bei sana.kwa huo ugonjwa wa tumbo peke yake jiandae sio chini ya 1M.Ila dawa zake ni uhakika.
Lakini kwa maleria unaweza kutumia vitunguu saumu,ni dawa nzuri sana.
 
Charity kwani zile za homeoipathic sijui ....samahani spelling mi sijui

jaribu zile ni hazina madhara/side effects nadhani
 
tumia majani ya nyanya pori inaitwa song'imycin kausha kuvulini then loweka kwenye maji salama kunywa kama glasi moja 3x per day for 5days
 
Hiyo typhoid umechunguzwa nini hadi ukaambiwa unayo?

Typhoid is the most over-diagnosed disease in Tanzania after Malaria.

Vituo vya afya huwa wanatumia hiyo diagnosis kutengeneza hela tu. Jaribu kufikiria, huwezi kwenda hospitali ya rufaa hata siku moja ukaambiwa unatyphoid si Muhimbili wala KCMC, Bugando au Mbeya.

Ni zile sehemu ambazo wanataka pesa yako.

Kama mnataka ufafanuzi zaidi nitarudi
 
Tafuteni dawa za kihaya zitawafaa nyote.

tumia majani ya nyanya pori inaitwa song'imycin kausha kuvulini then loweka kwenye maji salama kunywa kama glasi moja 3x per day for 5days

Irighaka kwa kikurya,tafuta kata kata kunywa glas moja kwa siku hasa asubuhi baada ya kula mlo wa kwanza!
Hey, kama mnazo si muwasiliane nae mumpe huyu dada wakuu?

Kutamka tu dawa itasaidia?Hapo kwa haraka mnaongelea kwenda Iringa, Mara na Bukoba, wakati mgonjwa (Charity)yuko Kinyerezi!...Kama mna stock fanyeni ze needful.
 
naungana na hoja ya Injinia hapo juu

Shemeji, Typhoid inataka management hasa baada ya kumaliza dozi ya kwanza, nikiassume kuwa ulikuwa diagnosed kiusahihi

cha kufanya, ukishamaliza dozi jitahidi kunywa maziwa fresh asubuhi na jioni, pia hakikisha usafi wa kwanza maji ya kunywa....make sure maji unayitumia hasa kunywa yamechemshwa kuanzia yale ya kuswakia!

jingine, kawaida ya ratio ya wale wajamaa ni 1:20 so huwa wapo tu..hata ukimaliza dawa, usihangaike kutumia nyingine mara moja..kaa kama mwezi hivi ukiifanyia management itaisha

hospitali zetu nyingi zinachanganya typhoid na malaria vile dalili zinafanana...so kuwa makini sana hapo
 
Nataka kupunguza utumiaji wa dawa za hospitali,nikimaanisha vidonge mpaka hapo itakapokuwa lazima sana.Kwa yeyote anayejua tiba mbadala ya typhoid please naomba msaada.
Nikisema mbadala namaanisha matunda,mizizi,mimea ama vyakula.


Bwana Yesu asifiwe.

Pole sana mamaa.

Dawa mbadala na ya uhakika ni hiyo hapo kwenye red. Itumie tafadhali, afu uniambie.
 
Hiyo typhoid umechunguzwa nini hadi ukaambiwa unayo?

Typhoid is the most over-diagnosed disease in Tanzania after Malaria.

Vituo vya afya huwa wanatumia hiyo diagnosis kutengeneza hela tu. Jaribu kufikiria, huwezi kwenda hospitali ya rufaa hata siku moja ukaambiwa unatyphoid si Muhimbili wala KCMC, Bugando au Mbeya.

Ni zile sehemu ambazo wanataka pesa yako.

Kama mnataka ufafanuzi zaidi nitarudi

Hii nimepimwa kwenye zahanati ya Kazini.Hii ni baada ya mfululizo wa kuumwa tumbo hasa wakati wa usiku kama nimebeba kitu kizito tumboni.Nilishaenda kwenye zahanati hiyo nikapewa dawa zilizonisaidia kiasi.Nilipoona tumbo linaaza tena ndio nikaenda na kukuta sina maleria wala vile vidudu vya kwanza.na ndipo walipochukua uamuzi wa kunipima typhoid na kunikuta nayo.kwa sasa sijaanza kutumia dawa walizonipa hospital ila natumia vitunguu saumu,mpka hapo nikikuta havinisaidii.
Kwa ufupi nadhani hawako kibiashra zaidi ila pengine ujuzi ndio ishu
 
Charity kwani zile za homeoipathic sijui ....samahani spelling mi sijui

jaribu zile ni hazina madhara/side effects nadhani
Nitazipata wapi hizi dia.

tumia majani ya nyanya pori inaitwa song'imycin kausha kuvulini then loweka kwenye maji salama kunywa kama glasi moja 3x per day for 5days
Dah,hizi nyanya pori ndio nyanya chungu?

Irighaka kwa kikurya,tafuta kata kata kunywa glas moja kwa siku hasa asubuhi baada ya kula mlo wa kwanza!
Hii irighaka itabidi nimtafute Mwita maranya.

naungana na hoja ya Injinia hapo juu

Shemeji, Typhoid inataka management hasa baada ya kumaliza dozi ya kwanza, nikiassume kuwa ulikuwa diagnosed kiusahihi

cha kufanya, ukishamaliza dozi jitahidi kunywa maziwa fresh asubuhi na jioni, pia hakikisha usafi wa kwanza maji ya kunywa....make sure maji unayitumia hasa kunywa yamechemshwa kuanzia yale ya kuswakia!

jingine, kawaida ya ratio ya wale wajamaa ni 1:20 so huwa wapo tu..hata ukimaliza dawa, usihangaike kutumia nyingine mara moja..kaa kama mwezi hivi ukiifanyia management itaisha

hospitali zetu nyingi zinachanganya typhoid na malaria vile dalili zinafanana...so kuwa makini sana hapo
asante shemeji.ntajitahidi hilo la usafi ila maziwa??????????japokuwa .........
 
Pole sana mamaa.

Dawa mbadala na ya uhakika ni hiyo hapo kwenye red. Itumie tafadhali, afu uniambie.
Dah! asante sana hun.wewe ndio unaujua ukweli ambao utaniweka huru completely.Ni YESU tu.
Asante kwa kuelewa umuhimu wa hili jina lipitalo majina yote.
 
usijali ntakupeleka mwenyewe my dear
nimewahi kuzitumia ni nzuri hazikunipa tabu yoyote sio kama kemikali za hospitali
 
pole sana ila angalia sana Typhod mara nyingi wataalamu wanasema joto la mwili linapopanda kwa kitu chochote kile wakikupima typhodi watakwambia unayo ni vyema kuwa makini hasa kwa wanaotafuta pesa. bora kupima tena. na inawezekana tumbo lako kuuma ukawa pia unatatizo jingine binafsi nilikuwa na sumbuliwa na tumbo na kila mara hosipitali walikuwa wanaiambia niina typhodi at last kumbe ilikuwa ni dalili ya apendex.
 
Back
Top Bottom