platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,363
- 11,149
Ni mwaka 2011 kuna rafiki yangu niliefahamiana wakati nilipoenda Kigoma. Baada ya kusita kwingi akanihadithia kisa chake kinachomsononesha mpaka leo.
Aliishi na mke wake kwa muda wa miaka 3 na kupata mtoto mmoja, jamaa ni mfanyabiashara wa kawaida na mara nyingi huwa anasafiri kwenda Mwanza,kahama na Dar kununua bidhaa na kuzipeleka Kigoma kama kawaida.
Siku asiyoisahau maishani alirudi nyumbani majira ya saa 6 usiku nyumbani kwake baada ya kukatisha safari kwa sababu gari ya mizigo aliyokuwa anaitumia iliharibika njiani.Bila hofu yeyote akagonga hodi mara kama tano hivi,ya sita akaja shemeji yake ambaye ni mdogo wa mkewe kumfungulia - Akastuka! Hii haikuwa kawaida,akauliza "dada yako yuko wapi?" mdogo mtu hana jibu(umri km miaka 7 hivi). Kuingia ndani hajamkuta mkewe bali mwanae amelala kitandani.
Alipandwa na hasira huku akitetemeka,akachukua kisu na kutoka nje......swali likawa anaenda kumtafuta wapi? akili ikamtuma aende guest iliyokuwa umbali wa mita kama 500 toka pale anapoishi,akajivuta mpaka pembeni mwa guest ile, tena swali likamjia amuulize mlinzi? hapana.Akaka pembeni huku anatazama mlango wa guest.
Saa 7......8..9 mpaka saa kumi hajaona mtu anatoka nje na ghafla mvua ya manyunyu ikawa inapuliza huku akivumilia.Akili yote imemtuma ni pale ndipo alipo mke wake, na mawazo lukuki kichwani.
Ilipotimu saa 12 mlinzi akafungua mlango na geti.Jamaa akapata fursa ya kuingia...........akavuka mlango wa kwanza..wa pili akasikia unafunguliwa.Lahaula alietoka wa kwanza ni mkewe,kijasho kikamtoka.Akamshika mkono na kumrudisha chumbani.
Lengo lilikuwa ni kuua....huku akitoa machozi akamuuliza mgoni wake "wewe ***********umetumia kondomu" akajibu ndio.
Mgoni karibia kuzirai............jamaa akamvuta mke wake "nikuue wewe ***?" .Mkewe akaomba sana msamaha.
Kifupi jamaa alitoka ndani na kuishia kwake na kumfungashia virago mkewe.Mpaka leo hajasahau kilichompata na imemuwia vigumu kuponya majeraha ya moyo na hajui ni vipi alishindwa kutimiza lengo alipofika Guest,kila anapokumbuka hana hamu ya kuoa tena.Nasaha za wazee wa pande zote mbili hazikusaidia kuokoa ndoa hiyo.
Aliishi na mke wake kwa muda wa miaka 3 na kupata mtoto mmoja, jamaa ni mfanyabiashara wa kawaida na mara nyingi huwa anasafiri kwenda Mwanza,kahama na Dar kununua bidhaa na kuzipeleka Kigoma kama kawaida.
Siku asiyoisahau maishani alirudi nyumbani majira ya saa 6 usiku nyumbani kwake baada ya kukatisha safari kwa sababu gari ya mizigo aliyokuwa anaitumia iliharibika njiani.Bila hofu yeyote akagonga hodi mara kama tano hivi,ya sita akaja shemeji yake ambaye ni mdogo wa mkewe kumfungulia - Akastuka! Hii haikuwa kawaida,akauliza "dada yako yuko wapi?" mdogo mtu hana jibu(umri km miaka 7 hivi). Kuingia ndani hajamkuta mkewe bali mwanae amelala kitandani.
Alipandwa na hasira huku akitetemeka,akachukua kisu na kutoka nje......swali likawa anaenda kumtafuta wapi? akili ikamtuma aende guest iliyokuwa umbali wa mita kama 500 toka pale anapoishi,akajivuta mpaka pembeni mwa guest ile, tena swali likamjia amuulize mlinzi? hapana.Akaka pembeni huku anatazama mlango wa guest.
Saa 7......8..9 mpaka saa kumi hajaona mtu anatoka nje na ghafla mvua ya manyunyu ikawa inapuliza huku akivumilia.Akili yote imemtuma ni pale ndipo alipo mke wake, na mawazo lukuki kichwani.
Ilipotimu saa 12 mlinzi akafungua mlango na geti.Jamaa akapata fursa ya kuingia...........akavuka mlango wa kwanza..wa pili akasikia unafunguliwa.Lahaula alietoka wa kwanza ni mkewe,kijasho kikamtoka.Akamshika mkono na kumrudisha chumbani.
Lengo lilikuwa ni kuua....huku akitoa machozi akamuuliza mgoni wake "wewe ***********umetumia kondomu" akajibu ndio.
Mgoni karibia kuzirai............jamaa akamvuta mke wake "nikuue wewe ***?" .Mkewe akaomba sana msamaha.
Kifupi jamaa alitoka ndani na kuishia kwake na kumfungashia virago mkewe.Mpaka leo hajasahau kilichompata na imemuwia vigumu kuponya majeraha ya moyo na hajui ni vipi alishindwa kutimiza lengo alipofika Guest,kila anapokumbuka hana hamu ya kuoa tena.Nasaha za wazee wa pande zote mbili hazikusaidia kuokoa ndoa hiyo.