Katika taarifa ya habari (ITV) Changamoto mbalimbali zimetolewa kuhusu ugawaji wa vitalu vya uwindaji. Swali langu wana JF. Hivi umuhimu wa kugawa vitalu ni nini? Serikali inapata nini hasa ukilinganisha na kutogawa vitalu hivyo. Hivi ina maana wanyama wanapaswa kupunguzwa? Mbona kuna kung'ang'ania sana hivyo vitalu? Hasa kwa watu wa nje.....Kama kuna waliosomea wildlife watujuze; ili watanzania tujue namna gani tunapaswa kulinda rasilimali zetu. Hivi na nchi nyingine wanafanya the same?? Kuna siri gani katika vitalu hivi????