Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

Kuna mbegu ya nguruwe warefu hawana mafuta mengi, wanazaa watoto wengi. Inapatikana wapi na kwa bei gani?
 
Wadau kuna threads nyingi humu kuhusu nguruwe zenye information za kutosha kujibu maswali ya kawaida.Pia internet imejaa mambo tele.Ukitaka kupata uhalisi tembelea wafugaji wanaofuga kibiashara.
 
Huu mradi huwa nafarijika sana nikisoma mada za humu ndani, Mimi ni mfugaji maarufu wa hawa viumbe(Avatar yangu inathibitisha) Tatizo langu kubwa ni namna ya kupunguza gharama za chakula kwani hivi viumbe vinakula sana. Na tatizo la pili ni vitoto kufa hasa wakiwa na miezi minne hadi tano.
 
1.Nguruwe anachukua miezi 6 mpaka 12 mpaka kufikia uzito wa kutosha (inategemeanan na malisho)
2.Inategemeana na nafasi yako, ukiwa upo pale full time, wapagazi watatu ni more than enough (kumbuka usipokuwapo watu wanakuwa na uzembe flan). mimi nnao sita chini ya usimamizi mkali.
3.inategemea uko wapi. huku kwetu hata kama haulimi gunia la pumba za mahindi ni Tsh 10,000/=! mashudu ya alizeti gunia ni 20,000/=!
4. Ekari moja wanakaa kwa amani yote. ni vizuri kuwa mbali na makazi ya watu.
5. inategemea uko wapi. kwangu mm nauwezo wa kuuza nguruwe 200 kwa mwezi bila shida. watoto inasumbua kidogo kwa sababu wananunua wafugaji, ukitaka kuwauza kwa urahisi wakuze mpaka miezi mitatu hv.
6. Minyoo na ukurutu. Kikubwa ni chanjo na usafi wa hali ya juu KILA SIKU (nguruwe ni msafi sana akitunzwa, wa kwangu nikimkuta sebuleni nacheka tu-ni WASAFI kama pet)

Nguruwe wanahitaji usimamizi wa karibu sana, uwajue kwa namba ili uweze kufuatilia maendeleo yao kila asubuhi. Ukiona mnyama mmoja amezubaa mwite doctor haraka sana. usiachie wasaidizi kila kitu, kuwa makini na kuhakikisha wanapata milo miwili ya kutosha bila kusahau vegs. nguruwe wanapenda maji-usiwanyime starehe ya kwa kuwabananisha hawatanenepa vya kutosha. Nguruwe ana uwezo wa kuzaa mara mbili kwa mwaka. Mimi sijasoma kilimo na mifugo, ni ubishi tu na kuthubutu vilivyoletwa na maisha magumu. MUHIMU UKUBALI KUKAA SHAMBA, JF UIPATE KWA TTCL NA SOLLAR!
Mkubwa naweza pata number yako ya simu na ww uko wapi maana mimi nataka kufuga kwa wingi
 
a68ff9b4f562c6632658a7c45ecb1e4c.jpg
Naomba number yako ya kwangu ni 0767164257
Kwa kuwa nna uzoefu wa kuendesha mradi wa nguruwe kwa mafanikio,watu wengi huulizia watoto wa nguruwe(piglets) kwa ajili ya kuanza mradi huo.Lakini hiyo sio namna nzuri kiuchumi.Namna sahihi kama unataka kifuga kibiashara ni kuanza na nguruwe wenye mimba!
SOMA HAPA UELEWE!Tutazungumzia chakula hapa kwa kuwa ndio gharama kubwa!
1.ukianza na piglet wa wiki 8,utamnunua kwa 60,000,
-week 4 za mwanzo atakula wastani wa 1kg/siku.Chukulia chakula 300/kg then jumla itakuwa =4x7x1x300=8,400
-kama utampandisha around week 28,week 20 atakula wastani wa 2kg/siku.jumla =20x7x2x300=84,000
-Atabeba mimba kwa siku 114.gharama ya chakula jumla=114x2x300=68,400
-atanyonyesha kwa week8.gharama ya chakula 8x7x6x300=100,800

Jumla kuu ya gharama ya piglet na chakula=261,600
Hii ni baada ya wiki 48(almost mwaka) ndio utaweza kuuza piglets wako wa mwanzo.akizaa 6 say na ukauza wote utapata 360,000


2.ukianza na nguruwe mwenye mimba ya wiki 8 uzao wa kwanza kwa 300,000
-utalea mimba kwa siku 58,gharama ya chakula=58x2x300=34,200
-gharama ya chakula wiki8 za kulea watoto=8x7x6x300=100,800
Jumla kuu ya gharama-435,00
Utaweza kuuza piglet wa kwanza ndani ya wiki 16(miezi4).
Kama umeelewa ndani ya wiki 40 tangu umenunua atakuwa amezaa mara 2 .gharama ya chakula itakuwa ni 304,200.Kama uzao wa kwanza majike uliwalea watakuwa tayari wamebeba mimba.

Gharama ya chakula kwenye mradi ndio kubwa,80%ya gharama zote.Ina maana ukitafuta namna ya kupunguza gharama ya chakula ndipo faida yako inaongezeka
Naweza pata number yako na unafugia wapi ya kwangu ni 0767164257, kwani nataka kuaanza kufuga maeneo ya Tanga nina ekari kama 50 hivi
 
Habari wapendwa

Samahan naomba kujua ufugaji wa nguruwe, malazi yao na matibabu yao.

Pia na ufugaji wa kuku wa kienyeji yaani jinsi ya kumnyang`anya vifaranga,na je nifanye hivo vikiwa vina umri gani?

Naitwa Moi Mwakye kutoka Mbeya.
 
Nguruwe ni Chanzo cha SARATANI (CANCER) YA TUMBO.

Mtamaliza wananchi kwa hawa wanyama nyie watu.
 
..ufugaji wa nguruwe unalipa sana.
mimi nimeanza na watoto kumi mwaka huu,nimeiga huu ujasiriamali,mzee alikuwa anafuga tokea enzi ya ujana wake,katusomesha wote mpaka vyuo vikuu kwa huu ujasiriamali,asante sana mtoa uzi nazidi kujifunza mengi kwa huu uzi,ubarikiwe sana.
 
..ufugaji wa nguruwe unalipa sana.
mimi nimeanza na watoto kumi mwaka huu,nimeiga huu ujasiriamali,mzee alikuwa anafuga tokea enzi ya ujana wake,katusomesha wote mpaka vyuo vikuu kwa huu ujasiriamali,asante sana mtoa uzi nazidi kujifunza mengi kwa huu uzi,ubarikiwe sana.
Hongera sana mkuu, sasa hakikisha kuwa haufugi kama alivyokuwa akifuga mzee wako. Wewe fuga kisasa mpaka mzee wako ajisikie raha kukupeleka shule. Unaweza kufunga drinkers za kisasa ili kurahisisha ufugaji wako wa nguruwe na kuwafanya wawe na afya bora, tunapatikana Dar lakini kama upo mkoani tutakuagizia kwa gharama zetu. Piga simu namba: 0625504952

KARIBU SASA NA UFURAHIE UFUGAJI WA KISASA
 
Habari wapendwa

Samahan naomba kujua ufugaji wa nguruwe, malazi yao na matibabu yao.

Pia na ufugaji wa kuku wa kienyeji yaani jinsi ya kumnyang`anya vifaranga,na je nifanye hivo vikiwa vina umri gani?

Naitwa Moi Mwakye kutoka Mbeya.


Utangulizi
Utunzaji wa nguruwe mara nyingi hutegemea aina ya nguruwe, njia na aina ya ufugaji. Kwa mfano nguruwe jike anayefugwa kwa ajili ya kuzaa anahitaji kutunzwa tofauti na wale wanaonenepeshwa kwa ajili ya nyama. Kadhalika nguruwe wanaweza kufugwa ndani ya banda au nje, kutegemea na ukubwa wa shamba, fedha zilizopo kwa shughuli za ufugaji na aina ya nguruwe.

Utunzaji wa Nguruwe Dume
Achaguliwe dume mwenye sifa bora ikiwa ni pamoja na kutokuwa na kilema au ugonjwa wowote. Dume aliyechaguliwa, atenganishwe na majike ili kuepusha kupanda wakati usiotakiwa. Inabidi nguruwe huyu asinenepeshwe, kwa hiyo alishwe chakula bora kiasi cha kilo mbili hadi tatu kwa siku. Vile vile apewe maji kila siku.

Kama anapanda chini ya mara tatu kwa wiki, alishwe kilo mbili na nusu na kama anapanda zaidi ya mara tatu, alishwe kilo tatu kwa siku. Ikiwa dume ni dhaifu, aongezewe nusu kilo ya chakula na kama amenenepa sana apunguziwe nusu kilo ya chakula kwa siku. Ni muhimu awe na eneo la mita mraba 9.3 ilikuwezakupata mazoezi ya mwili. Ikiwa sehemu ya kupanda imetenganishwa eneo livve la mita mraba saba.

Nguruwe dume anaweza kutumika kwa kupandajike akiwa na umri wa miezi minane hadi tisa. Kwa umri huu anaruhusiwa kupanda jike moja kwa juma. Afikiapo miezi 10 anaruhusiwa kupanda majike mawili hadi matatu kwa juma. Akiwa na umri wa mwaka mmoja au zaidi ana uwezo wa kupanda jike mmoja kila siku kwa majuma mawili hadi matatu, kisha apumzike kwa muda wa majuma mawili. Dume wakubwa wasitumike kupanda jike wadogo kwani wanaweza kuleta madhara kama vile kuwavunja mgongo.

Ni vizuri nguruwe dume mmoja apande jike 15 hadi 20 kwa mwaka. Dume akizeeka au kuwa na ubovu wa miguu, achinjwe mara moja. Ni muhimu dume aogeshwe kwa sabuni na dawa zinazoweza kuua wadudu na vijidudu vinavyoweza kusababisha magonjwa. Banda na vifaa vinavyotumika visafishwe kila siku.

Utunzaji Wa Nguruwe Jike
Ili mfugaji aweze kupata mazao mengi na bora hana budi kuchagua nguruwe jike mwenye sifa zinazotakiwa. Nguruwe huyu ni vizuri awe amezaliwa na mama anayezaa watoto wengi, mwenye kutoa maziwa mengi na mtunzaji mzuri wa watoto. Tabia hizi zinarithiwa hata navizazi vingine vijavyo. Vile vile awe na afyanzuri na chuchu nyingi zisizopungua 12.

Nguruwe jike anaweza kuzaa akiwa na umri wa miezi mitano hadi sita. Ili kumzuia asibebe mimba mapema, ni vizuri atenganishwe na dume afikiapo umri huo.

Afikiapo miezi nane hadi tisa au akiwa na uzito wa kilo 130 ahaweza kupandishwa. Kabla ya kupandishwa nguruwejike apewe kilo 2.5 hadi tatu za chakula kwa siku. Nguruwe asipelekwe kwa dume mpaka atakapoonyesha dalili zajoto.
Maelezo zaidi unaweza pata kupitia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom