Mradi wa Ufugaji wa ng'ombe

day 24

Member
Dec 21, 2010
13
8
Habari zenu wanajamii,

Kama kuna mtu anafahamu juu ya ufugaji wa ng'ombe wa maziwa naomba tushee utaalam ili nijue faida ya biashara hiyona hasara ya na vitu vinavyotakiwa kuanzia wanapopatikana hao ng'ombe na bei wanazouzia,soko la maziwa na tahadhari zake...naomba msaada wenu tafadhari

Wakuu nawasalimu sana. Napenda kabla ya yote niappreciate michango yenu hasa katika forum hii, imekuwa ikinisaidia sana. Sasa turudi kwenye uzi huo hapo juu:
Naomba mwenye ushauri juu ya jambo hilo anisaidie please, nipo dar natamani kuanza mradi huo januari mwakani. Mpango ni kuwa na ng'ombe bora kama 10 hivi (wenye uwezo wa kutoa minimum of 10 liters/ng,ombe per day), shamba kwa ajili ya kufugia na kuotesha malisho ya mifugo hiyo (about 6 acres). Naomba ushauri kuhusu yafuatayo:

Mbegu bora ya ng'ombe wa maziwa

Eneo lililopo nje kidogo ya mji ambalo naweza kulitumia( kwa kulinunua)

Ushauri wa namna bora ya kufanya mradi huo.

Please kwa anaejua possible costs za eneo na ng'ombe wazuri nitashukuru.


Wapendwa wana JF, heshima kwenu, pia poleni na pilika za maisha.

Back to the topic;

Mwenzenu nimechoshwa na kazi ya kuishi kwa kutegemea mshahara. Nataka kuwa mjasiria mali hasa katika ufugaji wa ng'ombe wa maziwa.

NB: Naomba mniambie zile nyasi za kulishia ngo'ombe wa maziwa ndani (Zero grazing) zile ambazo huwa zinapandwa na kuvunwa -ZINAITWAJE? NAWEZA KUZIPATA WAPI (MBEGU ZA HIZO NYASI) ili nizioteshe mwenyewe huku niliko..maana kununua sitoweza.

Nataka kuanza na ng'ombe watatu wa maziwa approx. kila ngo'mbe anipe lita 12 za maziwa kwa siku = Lita 36....je kwa mlio wazoefu na ufugaji hii hesabu yangu yaweza kutimia au nime-over estimate?

Natangulisha shukrani wadau.


Habari wanajukwaa,
Nataka nianze mradi wa ufugaji wa ng'ombe wa kisasa wa maziwa kwaajili ya biashara,naomba wenye uzoefu wa ufugaji huu wanisaidie kupata somo na mambo ya kuzingatia wakati wa ufugaji.

Pia naomba kujuzwa mbegu bora ni ipi,upatikanaji wake na soko la maziwa likoje.niko Dar es salaam.
Asanteni
 
habari zenu wanajamii,kama kuna mtu anafaham juu ya ufugaji wa ng'ombe wa maziwa naomba tushee utaalam ili nijue faida ya biashara hiyona hasara ya na vitu vinavyotakiwa kuanzia wanapopatikana hao ng'ombe na bei wanazouzia,soko la maziwa na tahadhari zake...naomba msaada wenu tafadhari

Mkuu hili suala, limeshajadiliwa sana hapa, hivyo ingekuwa ni busara kama ungepitia post za nyuma zinazoelezea suala hili hili kwani zitakuwa na msaada kwako na tutaokoa ujazo kwenye server za JF. Unaweza ukazipata hapa chini

1. ngombe wa maziwa
2. natafuta ngombe ankole type
3. kwa wanaopenda ufugaji mkubwa
4. naomba ushauri kufuga ng'ombe wa maziwa na kupack maziwa

Pia kuna hili andiko la FARM AFRIKA linalihusiana na ufugaji bora wa ngombe wa asili. Tafadhali lipitie
 

Attachments

  • pub_ufugaji_bora_wa_ngombe_wa_asili.pdf
    368.5 KB · Views: 2,414
Nilipita mitaa ya Nadanya huko umasaini, nikaona kundi kubwa la ndama mchanganyiko, wakubwa na wadogo. Nikashawishika kuuliza bei. Bei inacheza kati ya laki tatu mpaka laki nne.

Nikasema moyoni, nikiwanunua kumi hawa ndama madume, kisha niwahasi. Baada ya mwaka mmoja ninaweza pata ada ya watoto bila taabu. Kwa sasa dume mmoja mzuri pale Dar anaweza fika milioni moja bila udalali. Kwa wenye maeneo ya kufugia madume yaliyohasiwa hii ni biashara nzuri.
 
Nakukubali sana mkuu! Hivi nikitaka kumiliki hayo madume 200 natakiwa kua na eneo la ukubwa gani?na bei ya kuasi dume 1 ni bei gani?
 
Malila!

Juzi mnadani pale Wilayani Monduli,Dume mmoja kt ya madume walioletwa pale mnadani hakika aliuzwa Tsh. 1,100,000/= na wale wengine walilamba 1M na hata wale wa size ya kati ni laki 8 mwisho.

Ndio kweli nikakubalia na msemo huu

"KIZURI KINAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA"

Yule Dume alikuwa hakosi kg 420 na hadi 50.
Ufugaji dili Kamanda!
 
nakukubali sana mkuu!
Hivi nikitaka kumiliki hayo madume 200 natakiwa kua na eneo la ukubwa gani?na bei ya kuasi dume 1 ni bei gani?

Nimesahau kidogo, ukubwa wa eneo kwa ng`ombe mmoja. LAT akiiona hii maada atatoa jibu na pia anaweza kutoa gharama za kuhasia ng`ombe.
 
Wakuu naomba kuuliza swali. Ng'ombe dume anahasiwa ili iweje? Mimi nilidhani ananunuliwa ili azalishe?
 
Wakuu naomba kuuliza swali. Ng'ombe dume anahasiwa ili iweje? Mimi nilidhani ananunuliwa ili azalishe?

Si kila dume linafaa kwa mbegu, kumbuka dume moja laweza kuhudumia majike mpaka 250 kwa mwaka kama litatumika kitalaamu ( kama sijakosea). Pili dume likihasiwa ( ng`ombe, mbuzi nk) linakuwa haraka na kunenepa sana ktk muda mfupi. Kwa njia hii mkulima anaweza kupata faida haraka. Tunahitaji majike zaidi kuliko madume ktk ufugaji, hata kuku, jogoo ni mmoja kwa matetea matano.
 
Nimesahau kidogo, ukubwa wa eneo kwa ng`ombe mmoja. LAT akiiona hii maada atatoa jibu na pia anaweza kutoa gharama za kuhasia ng`ombe.
Shukrani sana mkuu,ngoja nimsubili LAT.
Pia kuna thread yangu nimeiweka hapa kwenye ujasiriamali inahusu"kufungua duka la mboga na matunda"naomba mawazo yako pale mkuu.
 
Shukrani sana mkuu,ngoja nimsubili LAT.
Pia kuna thread yangu nimeiweka hapa kwenye ujasiriamali inahusu"kufungua duka la mboga na matunda"naomba mawazo yako pale mkuu.
Ngoja niipitie, kama ninalo la kuchangia nitatoa.
 
Malila huu mpango wa kufuga ng'ombe wa nyama na mimi ninao kilichobaki sasa hivi nikuanza utekelezaji tu by 2013 nadhani mradi utakuwa hewani.. lakini mimi nafikiria kufuga ng'ombe wa nyama wa kisasa.. niliona kwa bwama ASAS aisee ng'ombe anakwenda mpaka kg 1000 within a year baada ya castration. ASAS anaimport mbegu kutoka Denmark na kuzihifadhi kwenye vacuum tanks na alisema pia anaziuza kwa wafugaji wengine.
Hawa wakienyeji tatizo ukuaji wake kidogo unachukua muda mrefu lakini kama utapenda unaweza kupata mbegu nzuri ya ng'ombe wakubwa kutoka kanda ya ziwa i.e shinyanga
 
Malila huu mpango wa kufuga ng'ombe wa nyama na mimi ninao kilichobaki sasa hivi nikuanza utekelezaji tu by 2013 nadhani mradi utakuwa hewani.. lakini mimi nafikiria kufuga ng'ombe wa nyama wa kisasa.. niliona kwa bwama ASAS aisee ng'ombe anakwenda mpaka kg 1000 within a year baada ya castration. ASAS anaimport mbegu kutoka Denmark na kuzihifadhi kwenye vacuum tanks na alisema pia anaziuza kwa wafugaji wengine.
Hawa wakienyeji tatizo ukuaji wake kidogo unachukua muda mrefu lakini kama utapenda unaweza kupata mbegu nzuri ya ng'ombe wakubwa kutoka kanda ya ziwa i.e shinyanga



Heko Kamanda!
 
Malila huu mpango wa kufuga ng'ombe wa nyama na mimi ninao kilichobaki sasa hivi nikuanza utekelezaji tu by 2013 nadhani mradi utakuwa hewani.. lakini mimi nafikiria kufuga ng'ombe wa nyama wa kisasa.. niliona kwa bwama ASAS aisee ng'ombe anakwenda mpaka kg 1000 within a year baada ya castration. ASAS anaimport mbegu kutoka Denmark na kuzihifadhi kwenye vacuum tanks na alisema pia anaziuza kwa wafugaji wengine.
Hawa wakienyeji tatizo ukuaji wake kidogo unachukua muda mrefu lakini kama utapenda unaweza kupata mbegu nzuri ya ng'ombe wakubwa kutoka kanda ya ziwa i.e shinyanga

Hawa wa kienyeji wanachelewa, lakini kuna hawa chotara. Mwezi jana nilifanikiwa kumpata mkulima mmoja na aliniuzia dume chotara kwa laki 3 na nusu. Nakubaliana na ww kabisa,lazima kuwa na mbegu kubwa.Kilichobaki kwangu ni kujenga zizi la kisasa ili niwaongeze wengine. Tafadhali,ukifanikiwa kupata mbegu kubwa nishitue.
 
Shukrani sana mkuu,ngoja nimsubili LAT.
Pia kuna thread yangu nimeiweka hapa kwenye ujasiriamali inahusu"kufungua duka la mboga na matunda"naomba mawazo yako pale mkuu.

mkuu hii hapa chini ni appraisal ya mradi wa ng,ombe wa maziwa nadhani unaweza kupata point chache hapa .... nilifanyiwa na jamaa wataalam wapo india ingawa sijaanza hii project

To give you a tentative appraisal for your Dairying plans:

1. the 18 acres of agricultural land will be sufficient to raise & supply green fodder for around 100-115 animals throughout the year; depending on the soil fertility and yields of fodder crops
2. We will need to make arrangements for irrigation because Dairying is an occupation that will need lots of water - for irrigation, for feeding, washing etc. Likewise, arrangements to get electricity or have DG sets will need to be made.
3. The distance to your market being just 8 km, we feel that you have a great advantage since transportation costs will be very limited
Since maize, Corn and Sunflower are already being grown, we feel that the land is suitable for growing other forage/fodder crops like Napier, Lucerne, Berseem, etc.
4. The average milk production from 100 odd animals will most likely be around 800-850 liters per day which is a good quantity to have a small processing plant. Milk could be pasteurised, pouched in HDPE bags and sold in the markets. Also a few popular milk products could be thought of
5. We assume that the price of milk mentioned by you - US $ 0.45/liter is for raw, unpasteurised milk sold loose. We will work out the exact processing/handling/packaging costs later on; but would it be realistic to assume that packed, pasteurised milk can be sold at US$ 1.00 a liter?
6. We would also suggest collection of milk from other farms/farmers to run our processing plant to maximum capacity. We also suggest that the farms be semi-mechanical; i.e. we use a blend of men + machinery.
7. It is also heartening to note that the nearest competitor is 85 km away and the next 245 km away!
8. As Technical Consultants, we will first all need to visit your site and survey from all tecno-commercial aspects. We will study and present a bankable Project feasibility Report. The report will cover Dairy farming and Milk Processing possibilities in your Milk Shed area. A Milk Shed area is the area within a radius of around 40-50 km from the site. Our survey will assess the milk production, bovine health, breeds, milk yields, possibility of cross-breeding with high yielders/ healthy animals of exotic blood, milk processing patterns, milk products demand:supply scenario, etc...
For the above (9), we will need around 10-12 days. We will visit in a team of 2 persons.
We will further assist you in setting up the farm +plant from scratch to operational status for which our fees will be based on the total project cost.
 
Hawa wa kienyeji wanachelewa, lakini kuna hawa chotara. Mwezi jana nilifanikiwa kumpata mkulima mmoja na aliniuzia dume chotara kwa laki 3 na nusu. Nakubaliana na ww kabisa,lazima kuwa na mbegu kubwa.Kilichobaki kwangu ni kujenga zizi la kisasa ili niwaongeze wengine. Tafadhali,ukifanikiwa kupata mbegu kubwa nishitue.

sawa hamna shida nikiwapata ambao hawajachezewa nitakutaarifu. Inatakiwa ucheze vizuri sana na msimu wa njaa, kwenye minada kule mpwapwa kipindi cha njaa unapata ng'o,mbe mkubwa kati ya 60-200,000/=, mbuzi anacheza kati ya 10-20,000/= january na feb njaa inazidi kupamba moto na bei inazidi kuporomoka.. march katikati karanga na mahindi ya kwanza yanaanza kukomaa na kidogo hapa bei inapanda, april mazao yote yanakuwa yamekomaa na bei inazidi kuongezeka... june..july..august-november mahindi, mtama vinasagwa and so ugali mwingi, hapa bei haikamatiki.. wauzaji wanaringa vibaya sana.
Wanyama wazuri utawapata kati ya janu-april, miezi ya june-november wanyama waliopo sokoni ni wale wenye matatizo.

Ukicheza vizuri kisomi na huu msimu wa njaa utatoka mapema sana na hautakuwa na haja ya kusubiri ng'ombe azae mtoto mmoja, kumkuza kwa miaka 4 na kuja kumuuza kwa 1-1.5m. Simply utanunua ndama wa miaka 2 unamkuza kwa mwaka 1.5 unamuingiza sokoni au unanunua wakubwa unawalisha vizuri kisasa wakifikia uzito wa maana wanaingia sokoni

NB: Miaka ya nyuma tulikuwa tunabadili ng'ombe huko vijijini, tulikuwa tunapeleka dume moja la kisasa, wanatupa ng'ombe mpaka 10 wa kienyeji wale wakubwa
 
Mambo vipi wakuu. Ninaomba anayefahamu minada ya mbuzi katika mikoa ya jirani especially Tanga, Morogoro (?), na Dodoma hasa siku za Ijumaa, Jumamosi, na Jumapili anifahamishe please. Kama una information nyingine yeyote kuhusu hili ambayo unadhani inaweza kusaidia unaweza kuchangia. Suggested Format: Mkoa-> Kijiji-> Siku-> Extra info (e.g. range ya bei, quality ya mbuzi, gharama za kusafirisha etc). Asanteni sana.

*On a second thought, nimeona kwamba watu wengine wanaweza kuwa interested na minada hiyo katika mikoa mingine na siku zingine. So, feel free to share the info regardless of the day and the region.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom