Pamoja na mabadiliko ya uongozi Wizara ya maliasili na utalii, ufisadi umeendelea kuitafuna wizara hiyo nyetu na kupoteza matumaini ya wananchi juu ya mstakabali wa wizara hiyo. Hali ni mbaya zaidi baada ya wale waliokuwa wakitarajiwa kutokomeza ufisadi kuibuka na kuwa vinara wa kuu wa ufisadi huo.
Viongozi wakuu wawili wa wizara hiyo ambao wote ni kina mama hivi karibuni wamejikuta katika mgogoro mkubwa hadi kutishiana vifo kutokana na magogo ambayo yanadaiwa ni ya mmoja wa wa akina mama hao kukamatwa na kuzuiwa wakati mwanamama huyo akiwa safarini. Baada ya kupewa taarifa ya kukamatwa mwanamama huyo alimpigia simu mwenzake ili alimalize soo hilo, jambo ambalo mwanamama mwenzake hakukubaliana nalo na hivyo kuamua kufungua sheria ichukue mkondo wake.
Kitendo cha mwanamama huyo kupuuza agizo hilo la bosi wake, kimeleta bifu kali na kuharibu hali ya hewa wizarani hapo. Inasemekana kuwa mwanamama ambaye anahusishwa na magogo hayo alimchimba biti mwenzake ikiwa ni pamoja na kumtishia kumuua. hali iliyosababisha achukue likizo ili kuepusha shari zaidi. Hata hivyo haikuweza kufamika mara moja ni kwa nini mwana mama huyo alitupilia mbali magizo y
la bosi wake huyo ili hali na yeye ni fisadi aliyekubuhu.
Habari za kutishiwa kifo mwana mama huyo aliziripotiwa ikulu, na siku za hivi karibuni watu wanaodaiwa kuwa usalama wa Taifa wamekuwa wakionekana kuzunguka mara kwa mara katika ofisi za wizara hiyo zilizoko mtaa wa samora. Haikuweza kufahamika mara moja wanausalama hao wamekuwa wakifanya nini. Baadhi ya watumishi wa wizara hiyo wameonekana wakisononeshwa na sakata hilo huku wakimtaka raisi JK kuingilia kati na kumuuondoa mmoja wao kabla hali haijawa mbaya zaidi.
"Watauana hawa kweli ohooo" alisikika mmoja wa watumishi hao akiongea. Mtoa habari alizidi kunyetisha kuwa, ugomvi kati ya kina mama hao, ulianzia katika swala la kuhama jengo. Mmoja wa akimama hao ambaye anahusishwa na magogo alitaka wizara hiyo ihamie kwenye jengo lake ambalo limeshakamilika lakini mwenzake alipinga kuwa hakuna kuhamia mpaka furniture mpya zinunuliwe. Inasemekana mama huyo alisha chonga dili la ununuzi wa furniture mpya kwa jengo zima mbazo zina gharimu mamilion ya fedha na hivyo kupata chajuu.
Hatua hiyo ya kulazamisha kuhama jengo inaelezwa ilimchukiza mwana mama huyo na huenda ndo sababu ya kumfanyia fitna mwenzake kwenye swala magogo.
Mimi kilichonishangaza hapa ni jinsi mwana mama huyo alivyo hodari wa kuchangamkia ufisadi. Muda mfupi tu mwana mama huyo kuingia ofisini tayari ameshaanza biashara ya magogo! Loh kweli fisadi ni fisadi tu
Bahati mbaya sina inzi wa kumtuma kuleta details. Wenye inzi tafadhali watumeni inzi wenu watuletee habari zaidi.
Viongozi wakuu wawili wa wizara hiyo ambao wote ni kina mama hivi karibuni wamejikuta katika mgogoro mkubwa hadi kutishiana vifo kutokana na magogo ambayo yanadaiwa ni ya mmoja wa wa akina mama hao kukamatwa na kuzuiwa wakati mwanamama huyo akiwa safarini. Baada ya kupewa taarifa ya kukamatwa mwanamama huyo alimpigia simu mwenzake ili alimalize soo hilo, jambo ambalo mwanamama mwenzake hakukubaliana nalo na hivyo kuamua kufungua sheria ichukue mkondo wake.
Kitendo cha mwanamama huyo kupuuza agizo hilo la bosi wake, kimeleta bifu kali na kuharibu hali ya hewa wizarani hapo. Inasemekana kuwa mwanamama ambaye anahusishwa na magogo hayo alimchimba biti mwenzake ikiwa ni pamoja na kumtishia kumuua. hali iliyosababisha achukue likizo ili kuepusha shari zaidi. Hata hivyo haikuweza kufamika mara moja ni kwa nini mwana mama huyo alitupilia mbali magizo y
la bosi wake huyo ili hali na yeye ni fisadi aliyekubuhu.
Habari za kutishiwa kifo mwana mama huyo aliziripotiwa ikulu, na siku za hivi karibuni watu wanaodaiwa kuwa usalama wa Taifa wamekuwa wakionekana kuzunguka mara kwa mara katika ofisi za wizara hiyo zilizoko mtaa wa samora. Haikuweza kufahamika mara moja wanausalama hao wamekuwa wakifanya nini. Baadhi ya watumishi wa wizara hiyo wameonekana wakisononeshwa na sakata hilo huku wakimtaka raisi JK kuingilia kati na kumuuondoa mmoja wao kabla hali haijawa mbaya zaidi.
"Watauana hawa kweli ohooo" alisikika mmoja wa watumishi hao akiongea. Mtoa habari alizidi kunyetisha kuwa, ugomvi kati ya kina mama hao, ulianzia katika swala la kuhama jengo. Mmoja wa akimama hao ambaye anahusishwa na magogo alitaka wizara hiyo ihamie kwenye jengo lake ambalo limeshakamilika lakini mwenzake alipinga kuwa hakuna kuhamia mpaka furniture mpya zinunuliwe. Inasemekana mama huyo alisha chonga dili la ununuzi wa furniture mpya kwa jengo zima mbazo zina gharimu mamilion ya fedha na hivyo kupata chajuu.
Hatua hiyo ya kulazamisha kuhama jengo inaelezwa ilimchukiza mwana mama huyo na huenda ndo sababu ya kumfanyia fitna mwenzake kwenye swala magogo.
Mimi kilichonishangaza hapa ni jinsi mwana mama huyo alivyo hodari wa kuchangamkia ufisadi. Muda mfupi tu mwana mama huyo kuingia ofisini tayari ameshaanza biashara ya magogo! Loh kweli fisadi ni fisadi tu
Bahati mbaya sina inzi wa kumtuma kuleta details. Wenye inzi tafadhali watumeni inzi wenu watuletee habari zaidi.