Mjomba wa taifa
JF-Expert Member
- Apr 20, 2012
- 231
- 161
Watanzania wamechoka kusikia habari za rushwa iliyotolewa katika ununuzi wa rada ya nchi. Suala hili limejadiliwa Bungeni zaidi ya miaka 4 sasa bila kuona wahusika wanachukuliwa hatua badala yake Serikali imekuwa ikipoza machungu ya rushwa hiyo kwa kuipachika majina ya kupotezea kama "chenji ya rada" wengine wameibatiza na kuiita "ni vijisenti" .
Wabunge wamekuwa wakitumia pesa za nchi kulijadili suala hili pasipo ukomo miaka yote.
OMBI:Kama wahusika wa ufisadi huu imeshindikana kuwachukulia hatua basi wabunge fungeni midomo yenu tumechoka kusikia makelele yanayodhihaki wananchi huku mafisadi wanaendelea kutamba mitaani. Pangeni ziara muende kutembea nje ya nchi na starehe zote za dunia, tukutane majimboni uchaguzi ujao 2012.
Wabunge wamekuwa wakitumia pesa za nchi kulijadili suala hili pasipo ukomo miaka yote.
OMBI:Kama wahusika wa ufisadi huu imeshindikana kuwachukulia hatua basi wabunge fungeni midomo yenu tumechoka kusikia makelele yanayodhihaki wananchi huku mafisadi wanaendelea kutamba mitaani. Pangeni ziara muende kutembea nje ya nchi na starehe zote za dunia, tukutane majimboni uchaguzi ujao 2012.