Utamaduni
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 1,279
- 597
Kuna taarifa ambazo zinazagaa sana mtaani ambazo nimezipata jana. Kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco wanakula dili na wafanyabiashara kwa kuwauzia umeme nje ya system ya Tanesco. kwa mfano katika siku ya jana LUKU vending Station ziligoma katika maeneo yote ya jijini Dar es Salaam na katika kugoma huko ndipo wanafanya ufisadi wao kwa kuuza luku kimagendo. ni hivi, wahusika hao ndio wanaosababisha mitambo ya luku igome (technically) na katika muda huo wa luku machine kugoma, wahusika wanaokula dili hilo huuza umeme kwa bei ya kutupwa kwa makampuni na hata watu binafsi kitendo ambacho hawawezi kukamatwa kwani pindi network yao inaporudi tanesco hawawezi kugundua nini kimefanyika. inasemekana umeme wanaouuza ni wa bei ghali kuanzia 1 mil na kuendelea na huuza kwa bei ya maelewano kati ya mnunuzi na muuzaji bila kujali rate ya Tanesco na hela yote kuishia mifukoni mwao.
hii ni habari iliyonishitua kidogo, katika ukame wa pesa ulionao tanesco bado kuna watu wanafanya kitu kama hiki, kama kweli, kwa yeyote mwenye taarifa kamili juu ya hili tunaomba atufahamishe na kwa yeyote anayejua jinsi mashine za luku zinavyo'oparate atuambie.
Je? ni kweli kuna kitu kama hiki cha kuuza luku kiholela?
Je? wahusika hao ni kina nani?
hii ni habari iliyonishitua kidogo, katika ukame wa pesa ulionao tanesco bado kuna watu wanafanya kitu kama hiki, kama kweli, kwa yeyote mwenye taarifa kamili juu ya hili tunaomba atufahamishe na kwa yeyote anayejua jinsi mashine za luku zinavyo'oparate atuambie.
Je? ni kweli kuna kitu kama hiki cha kuuza luku kiholela?
Je? wahusika hao ni kina nani?