Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Kama hiyo radio imeamua kutangaza wanachotangaza wala sina shida na hilo. Linalonisumbua ni aina ya ufadhili ambao radio inauopata lutoka kwa CCM. Je, ni wa kifedha, vifaa, utaalamu wa watu? nataka kujua hivi kwa sababu hata kwa asiye mwana CCM, bado chama hicho kinapata ruzuku kutokana na fedha za walipa kodi wote, hivyo ni vema tukafahamu fedha zetu zinatumikajeNilikuwa na washikaji wakati tunajadili issue za pilitik, ikaja suala la miropoko inayotolewa na Mtangazaji mmoja wa clouds fm ambaye wengi tunamjua. Wakati mjadala unaendelea jamaa mmoja akatueleza kwamba kwa kuwa hii redio imekuwa mstari wa mbele kupitia huyo mtangazaji kuipandisha chati ccm, eti ccm imeamua kuifadhili ili iweze kujitanua sawasawa ikiwezekana mikoa yote.
Lengo la ccm kutoa huo ufadhili kwa hii redio ni kuhakikisha kwamba ikifika 2015 iweze kutumika katika kampeni zake. Hii imetokana na redio husika kusikilizwa na watu wengi tofauti na redio uhuru ambayo imekosa umaarufu na wasikilizaji wa maana. Hii inatokana na ukweli kwamba redio hii imekuwa mstari wa mbele kukisemea ccm, ingawa redio yenyewe sio ya chama.
Wajemeni ni ngumu sana kwa haka kanchi kupata maendeleo maana ingawa tuko ktk mwaka wa pili tangu uchaguzi mkuu, watu wameshaanza kuandaa mashambulizi, ili hali watz bado tupo katika lindi la umasikini.